Yohana 16:1-33
16 “Nimewaambia ninyi mambo haya ili msikwazike.+
2 Watu watawafukuza ninyi katika sinagogi.+ Kwa kweli, saa inakuja wakati ambapo kila mtu anayewaua ninyi atafikiri amemtolea Mungu utumishi mtakatifu.+
3 Lakini watafanya mambo haya kwa sababu hawamjui Baba wala hawanijui.+
4 Hata hivyo, nimewaambia ninyi mambo haya ili, saa ya mambo haya itakapofika, mpate kukumbuka niliwaambia mambo haya.+
“Hata hivyo, mambo haya sikuwaambia hapo kwanza, kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.
5 Lakini sasa ninaenda kwake aliyenituma,+ na bado hakuna hata mmoja wenu anayeniuliza, ‘Unaenda wapi?’
6 Lakini kwa sababu nimewaambia mambo haya huzuni+ imejaa mioyoni mwenu.
7 Hata hivyo, ninawaambia ninyi kweli, ninaenda zangu kwa faida yenu. Kwa maana nisipoenda zangu, msaidizi+ hatakuja kwenu kamwe; bali nikienda zangu, nitamtuma kwenu.
8 Naye atakapofika ataupa ulimwengu uthibitisho wenye kusadikisha kuhusu dhambi na kuhusu uadilifu na kuhusu hukumu:+
9 kwanza, kuhusu dhambi,+ kwa sababu hawaniamini;+
10 kisha kuhusu uadilifu,+ kwa sababu ninaenda kwa Baba nanyi hamtaniona tena;
11 kisha kuhusu hukumu,+ kwa sababu mtawala wa ulimwengu huu amehukumiwa.+
12 “Bado nina mambo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili kwa sasa.+
13 Hata hivyo, huyo atakapofika, roho ya ile kweli,+ atawaongoza ninyi ndani ya kweli yote, kwa maana hatasema kwa msukumo wake mwenyewe, bali mambo anayoyasikia atasema, naye atawatangazia mambo yanayokuja.+
14 Huyo atanitukuza,+ kwa sababu atapokea lililo langu na kulitangaza kwenu.+
15 Yote aliyo nayo Baba ni yangu.+ Ndiyo sababu nilisema yeye hupokea lililo langu na kulitangaza kwenu.
16 Baada ya muda kidogo hamtaniona tena,+ na, tena, baada ya muda kidogo mtaniona.”
17 Kwa hiyo baadhi ya wanafunzi wake wakaambiana: “Hili analotuambia linamaanisha nini, ‘Baada ya muda kidogo hamtaniona, na, tena, baada ya muda kidogo mtaniona,’ na, ‘kwa sababu ninaenda kwa Baba’?”
18 Kwa hiyo walikuwa wakisema: “Hili analosema linamaanisha nini, ‘muda kidogo’? Sisi hatujui analoongea juu yake.”
19 Yesu alijua+ walikuwa wanataka kumuuliza, kwa hiyo akawaambia: “Je, mnaulizana kati yenu wenyewe juu ya hili, kwa sababu nilisema, Baada ya muda kidogo hamtaniona, na, tena, baada ya muda kidogo mtaniona?
20 Kwa kweli kabisa ninawaambia, Ninyi mtalia na kuomboleza, bali ulimwengu utashangilia; mtahuzunika,+ lakini huzuni yenu itageuzwa kuwa shangwe.+
21 Mwanamke, anapokuwa akizaa, ana huzuni, kwa sababu saa yake imefika;+ lakini baada ya kuzaa mtoto mchanga, haikumbuki tena dhiki kwa sababu ya shangwe ya kwamba mtu amezaliwa ulimwenguni.
22 Kwa hiyo, ninyi pia, sasa, kwa kweli, mna huzuni; lakini nitawaona ninyi tena na mioyo yenu itashangilia,+ na hakuna mtu atakayeichukua shangwe yenu kutoka kwenu.
23 Na siku hiyo+ hamtaniuliza swali kamwe. Kwa kweli kabisa ninawaambia, Mkimwomba Baba jambo lolote+ atawapa katika jina langu.+
24 Mpaka wakati huu wa sasa ninyi hamjaomba hata jambo moja katika jina langu. Ombeni nanyi mtapokea, ili shangwe yenu ipate kujazwa.+
25 “Nimewaambia ninyi mambo haya kwa mifano.+ Saa inakuja wakati ambapo hakika sitasema nanyi tena kwa mifano, bali nitawaeleza waziwazi kuhusu Baba.
26 Siku hiyo mtaomba katika jina langu, nami siwaambii kwamba nitamwomba Baba kuwahusu ninyi.
27 Kwa maana Baba mwenyewe anawapenda ninyi, kwa sababu mmenipenda+ na mmeamini kwamba mimi nilitoka nikiwa mwakilishi wa Baba.+
28 Mimi nilitoka kwa Baba na nimekuja ulimwenguni. Na zaidi ya hayo, ninauacha ulimwengu nami ninaenda kwa Baba.”+
29 Wanafunzi wake wakasema: “Unaona! Sasa unasema waziwazi, nawe husemi kwa mifano.
30 Sasa tunajua kwamba unajua mambo yote+ na huhitaji kuulizwa swali na yeyote.+ Kwa hili sisi tunaamini kwamba ulitoka kwa Mungu.”+
31 Yesu akawajibu: “Je, mnaamini sasa?
32 Tazameni! Saa inakuja, kwa kweli, imekuja, wakati mtakapotawanyika na kwenda kila mmoja kwenye nyumba+ yake nanyi mtaniacha peke yangu; na bado siko peke yangu, kwa sababu Baba yuko pamoja nami.+
33 Nimewaambia mambo haya ili kupitia kwangu mpate kuwa na amani.+ Ulimwenguni mna dhiki, lakini jipeni moyo! Mimi nimeushinda ulimwengu.”+