Yohana 15:1-27
15 “Mimi ndiye mzabibu wa kweli,+ na Baba yangu ndiye mkulima.+
2 Kila tawi ndani yangu lisilozaa matunda yeye huliondolea mbali,+ na kila tawi linalozaa matunda yeye hulisafisha,+ lipate kuzaa matunda zaidi.+
3 Tayari ninyi ni safi kwa sababu ya neno ambalo nimewaambia.+
4 Kaeni katika muungano pamoja nami, na mimi katika muungano pamoja nanyi.+ Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa matunda likiwa peke yake lisipokaa katika mzabibu, vivyo hivyo ninyi hamwezi, msipokaa katika muungano pamoja nami.+
5 Mimi ndiye mzabibu, ninyi ndio matawi. Yule ambaye hukaa katika muungano pamoja nami, na mimi katika muungano pamoja naye, huyo huzaa matunda mengi;+ kwa sababu bila mimi hamwezi kufanya lolote kamwe.
6 Ikiwa yeyote hakai katika muungano pamoja nami, huyo hutupwa nje kama tawi na hukauka; na watu hukusanya matawi hayo na kuyatupa ndani ya moto nayo yanateketezwa.+
7 Mkikaa katika muungano pamoja nami na maneno yangu yakae ndani yenu, ombeni lolote mnalotaka nalo litatukia kwenu.+
8 Baba yangu hutukuzwa katika hili, kwamba mwendelee kuzaa matunda mengi na kujionyesha kuwa wanafunzi wangu.+
9 Kama vile Baba alivyonipenda+ nami nilivyowapenda ninyi, kaeni katika upendo wangu.
10 Mkishika amri zangu,+ mtakaa katika upendo wangu, kama vile mimi nilivyoshika amri za Baba+ na kukaa katika upendo wake.
11 “Mambo haya nimewaambia, ili shangwe yangu ipate kuwa ndani yenu na shangwe yenu ipate kujaa.+
12 Hii ndiyo amri yangu, kwamba mpendane kama vile nilivyowapenda ninyi.+
13 Hakuna aliye na upendo mkuu kuliko huu, kwamba mtu aitoe nafsi yake kwa ajili ya rafiki zake.+
14 Ninyi ni rafiki zangu ikiwa mnafanya ninalowaamuru ninyi.+
15 Siwaiti ninyi tena watumwa, kwa sababu mtumwa hajui yale ambayo bwana wake anafanya. Lakini nimewaita ninyi rafiki,+ kwa sababu mambo yote ambayo nimeyasikia kutoka kwa Baba yangu nimewajulisha ninyi.+
16 Ninyi hamkunichagua mimi, bali mimi niliwachagua, nami niliwaweka ninyi msonge mbele na kuendelea kuzaa matunda+ na kwamba matunda yenu yapate kukaa; ili hata mkimwomba Baba jambo gani katika jina langu, apate kuwapa hilo.+
17 “Mambo haya ninawaamuru ninyi, kwamba mpendane.+
18 Ikiwa ulimwengu unawachukia ninyi, mnajua kwamba umenichukia mimi kabla ya kuwachukia ninyi.+
19 Kama mngekuwa sehemu ya ulimwengu, ulimwengu ungependa kilicho chake.+ Sasa kwa sababu ninyi si sehemu ya ulimwengu, bali nimewachagua ninyi kutoka ulimwenguni,+ kwa sababu hiyo ulimwengu unawachukia ninyi.+
20 Kumbukeni neno nililowaambia, Mtumwa si mkuu kuliko bwana wake. Ikiwa wamenitesa mimi, watawatesa ninyi pia;+ ikiwa wamelishika neno langu, watalishika lenu pia.
21 Lakini watawatendea mambo yote haya kwa ajili ya jina langu, kwa sababu hawamjui aliyenituma.+
22 Kama singekuja na kuwaambia, hawangekuwa na dhambi;+ lakini sasa hawana sababu ya kujitetea kwa ajili ya dhambi yao.+
23 Anayenichukia anamchukia Baba yangu pia.+
24 Kama singefanya kati yao kazi ambazo hakuna mwingine aliyezifanya,+ hawangekuwa na dhambi;+ lakini sasa wameniona na pia wamenichukia mimi na vilevile Baba yangu.+
25 Lakini ni ili neno lililoandikwa katika Sheria yao lipate kutimizwa, ‘Walinichukia bila sababu.’+
26 Wakati atakapofika msaidizi ambaye nitawapelekea ninyi kutoka kwa Baba,+ roho ya ile kweli, ambayo inatoka kwa Baba, huyo atatoa ushahidi juu yangu;+
27 nanyi, mtatoa ushahidi,+ kwa sababu mmekuwa pamoja nami kutoka wakati nilipoanza.