Yohana 12:1-50

12  Basi, siku sita kabla ya pasaka, Yesu alifika Bethania,+ alikokuwa Lazaro+ ambaye Yesu alikuwa amemfufua kutoka kwa wafu.  Kwa hiyo wakamwandalia mlo wa jioni huko, na Martha+ alikuwa akihudumu,+ lakini Lazaro alikuwa mmoja wa wale waliokuwa wameketi mezani pamoja naye.+  Kwa hiyo, Maria akachukua ratili moja ya mafuta yenye marashi, nardo+ halisi, ghali sana, na kuipaka miguu ya Yesu, naye akaikausha miguu yake kwa kuifuta kwa nywele zake.+ Nyumba ikajaa harufu ya mafuta yenye marashi.  Lakini Yuda Iskariote,+ mmoja wa wanafunzi wake, aliyekuwa karibu kumsaliti, akasema:  “Kwa nini mafuta haya yenye marashi+ hayakuuzwa kwa dinari mia tatu na kupewa maskini?”+  Ingawa hivyo, alisema hilo si kwa sababu aliwahangaikia maskini, bali kwa sababu yeye alikuwa mwizi+ na alikuwa na sanduku la pesa+ na alikuwa akichukua pesa zilizowekwa ndani yake.  Kwa hiyo Yesu akasema: “Mwacheni, ili ashike mwadhimisho huu kwa kufikiria siku ya maziko yangu.+  Kwa maana mna maskini+ pamoja nanyi sikuzote, lakini mimi hamtakuwa pamoja nami sikuzote.”  Kwa hiyo umati mkubwa wa Wayahudi wakapata kujua kwamba alikuwa huko, nao wakaja, si kwa sababu ya Yesu tu, bali pia wamwone Lazaro, aliyemfufua kutoka kwa wafu.+ 10  Sasa wakuu wa makuhani wakakata shauri kumuua Lazaro pia,+ 11  kwa kuwa wengi kati ya Wayahudi walikuwa wakienda huko na kumwamini Yesu+ kwa sababu yake. 12  Siku iliyofuata umati mkubwa waliokuwa wamekuja kwenye sherehe, waliposikia kwamba Yesu alikuwa akija Yerusalemu, 13  wakachukua matawi ya mitende+ na kutoka nje wakutane naye. Nao wakaanza kupaaza sauti:+ “Mwokoe, tunaomba!+ Aliyebarikiwa ni yule anayekuja katika jina la Yehova,+ naam, mfalme+ wa Israeli!” 14  Lakini Yesu alipompata mwana-punda,+ akaketi juu yake, kama vile ilivyoandikwa: 15  “Usiogope, binti Sayuni. Tazama! Mfalme wako anakuja,+ akiwa ameketi juu ya mwana wa punda.”+ 16  Mambo haya wanafunzi wake hawakuyajali hapo kwanza,+ lakini Yesu alipotukuzwa,+ ndipo walipokumbuka kwamba mambo haya yalikuwa yameandikwa juu yake na kwamba walimtendea mambo hayo.+ 17  Basi umati uliokuwa pamoja naye alipomwita Lazaro+ kutoka kaburini na kumfufua kutoka kwa wafu ukaendelea kutoa ushahidi.+ 18  Kwa ajili ya hili umati huo, kwa sababu ulisikia alikuwa amefanya ishara+ hiyo, ukakutana naye pia. 19  Kwa hiyo Mafarisayo+ wakasema kati yao wenyewe: “Ninyi mnaona kwamba hamfanikiwi kamwe. Oneni! Ulimwengu umemfuata.”+ 20  Sasa kulikuwa na baadhi ya Wagiriki+ kati ya wale waliopanda kwenda kuabudu kwenye sherehe. 21  Kwa hiyo, hao walimkaribia Filipo+ ambaye alikuwa wa kutoka Bethsaida ya Galilaya, nao wakaanza kumwomba, wakisema: “Bwana, tunataka kumwona Yesu.”+ 22  Filipo akaja akamwambia Andrea. Andrea na Filipo wakaja, wakamwambia Yesu. 23  Lakini Yesu akawajibu, akisema: “Saa imekuja Mwana wa binadamu atukuzwe.+ 24  Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, Mbegu ya ngano isipoanguka katika udongo na kufa, hiyo hubaki ikiwa mbegu moja tu; lakini ikifa,+ ndipo hiyo huzaa matunda mengi. 25  Yule anayeipenda sana nafsi yake huiangamiza, lakini yule anayeichukia nafsi+ yake katika ulimwengu huu atailinda kwa ajili ya uzima wa milele.+ 26  Ikiwa yeyote anataka kunihudumia, acha anifuate, na mahali nilipo hapo ndipo mhudumu wangu atakapokuwa pia.+ Ikiwa yeyote anataka kunihudumia, Baba atamheshimu huyo.+ 27  Sasa nafsi yangu inataabika,+ nami nitasema nini? Baba, niokoe kutoka katika saa hii.+ Hata hivyo, ndiyo sababu nimekuja kwenye saa hii. 28  Baba, litukuze jina lako.” Kwa hiyo sauti+ ikaja kutoka mbinguni: “Nimelitukuza na pia nitalitukuza tena.”+ 29  Kwa hiyo umati waliosimama huku na huku na kusikia hilo wakaanza kusema kumekuwa na mngurumo. Wengine wakaanza kusema: “Malaika amesema naye.” 30  Yesu akajibu, akasema: “Sauti hii imetokea, si kwa ajili yangu, bali kwa ajili yenu.+ 31  Sasa ulimwengu huu unahukumiwa; sasa mtawala wa ulimwengu+ huu atatupwa nje.+ 32  Na bado mimi, nikiinuliwa+ kutoka duniani, nitavuta watu wa namna zote kwangu.”+ 33  Kwa kweli hili alikuwa akilisema ili kutoa ishara ni kifo cha namna gani alikuwa karibu kufa.+ 34  Kwa hiyo umati wakamjibu: “Sisi tulisikia kutoka katika Sheria kwamba Kristo hudumu milele;+ basi kwa nini unasema kwamba lazima Mwana wa binadamu ainuliwe?+ Huyo Mwana wa binadamu ni nani?”+ 35  Kwa hiyo Yesu akawaambia: “Nuru itakuwa kati yenu kwa muda kidogo zaidi. Tembeeni wakati mna nuru, ili giza+ lisiwazidi nguvu; na yule ambaye hutembea katika giza hajui anakoenda.+ 36  Wakati mna nuru, iweni na imani katika nuru, ili muwe wana wa nuru.”+ Yesu alisema mambo hayo akaenda zake na kujificha mbali nao. 37  Lakini ijapokuwa alikuwa amefanya ishara nyingi sana mbele yao, hawakuwa wanamwamini, 38  hata kwamba neno la nabii Isaya likatimizwa ambalo alisema: “Yehova, ni nani aliyeliamini jambo ambalo tumesikia?+ Na kwa habari ya mkono wa Yehova, umefunuliwa kwa nani?”+ 39  Wao hawakuamini kwa sababu tena Isaya alisema: 40  “Ameyapofusha macho yao naye ameifanya mioyo yao iwe migumu,+ ili wasione kwa macho yao na kulielewa wazo kwa mioyo yao na kugeuka nami niwaponye.”+ 41  Isaya alisema mambo haya kwa sababu aliona utukufu wake,+ naye alisema juu yake. 42  Hata hivyo, wengi hata kati ya watawala kwa kweli walimwamini,+ lakini kwa sababu ya Mafarisayo wakawa hawamkiri, ili wasifukuzwe katika sinagogi;+ 43  kwa maana waliupenda utukufu wa wanadamu kuliko hata utukufu wa Mungu.+ 44  Hata hivyo, Yesu akapaaza sauti na kusema: “Yule ambaye huniamini huamini, si mimi tu, bali pia yule aliyenituma;+ 45  na yule ambaye hunitazama humtazama pia yule aliyenituma.+ 46  Nimekuja nikiwa nuru ulimwenguni,+ ili kila mtu anayeniamini asipate kukaa katika giza.+ 47  Lakini ikiwa yeyote anasikia maneno yangu na hayashiki, simhukumu; kwa maana nilikuja, si kuuhukumu ulimwengu,+ bali kuuokoa ulimwengu.+ 48  Yule ambaye hunipuuza wala hapokei maneno yangu ana wa kumhukumu. Neno+ ambalo nimesema ndilo litakalomhukumu katika siku ya mwisho; 49  kwa sababu sijasema kutokana na msukumo wangu mwenyewe, bali Baba mwenyewe aliyenituma amenipa amri kuhusu jambo la kutangaza na la kusema.+ 50  Pia ninajua kwamba amri yake inamaanisha uzima wa milele.+ Kwa hiyo mambo ninayosema, kama vile Baba alivyoniambia, ndivyo ninavyoyasema.”+

Maelezo ya Chini