Yohana 1:1-51

1  Hapo mwanzo+ Neno+ alikuwako, na Neno alikuwa pamoja na Mungu,+ na Neno alikuwa mungu.+  Hapo mwanzo+ huyo alikuwa pamoja na Mungu.+  Vitu vyote vilikuja kuwako kupitia kwake,+ na bila yeye hakuna hata kitu kimoja kilichokuja kuwako. Kile ambacho kimekuja kuwako  kupitia kwake kilikuwa uzima,+ na uzima ndio uliokuwa nuru+ ya wanadamu.  Na nuru inang’aa katika giza,+ lakini giza halijaizidi nguvu.  Kulitokea mtu aliyetumwa awe mwakilishi wa Mungu:+ jina lake lilikuwa Yohana.+  Mtu huyo alikuja kwa ajili ya ushahidi, ili atoe ushahidi+ juu ya nuru,+ kusudi watu wa namna zote wapate kuamini kupitia kwake.+  Yeye hakuwa nuru hiyo,+ bali alikusudiwa atoe ushahidi+ juu ya nuru hiyo.  Nuru+ ya kweli ambayo humpa nuru+ mtu wa kila namna,+ ilikuwa karibu kuja ulimwenguni. 10  Alikuwa ulimwenguni,+ nao ulimwengu ulikuja kuwako kupitia kwake,+ lakini ulimwengu haukumjua. 11  Alikuja nyumbani kwake mwenyewe, lakini watu wake mwenyewe hawakumkaribisha.+ 12  Hata hivyo, wengi kadiri ileile waliompokea,+ aliwapa mamlaka ya kuwa watoto wa Mungu,+ kwa sababu walikuwa wakionyesha imani katika jina lake;+ 13  nao walizaliwa, si kutokana na damu au kutokana na mapenzi ya mwili au kutokana na mapenzi ya mwanadamu, bali kutokana na Mungu.+ 14  Kwa hiyo Neno akawa mwili,+ akakaa katikati yetu, nasi tukautazama utukufu wake, utukufu kama ule ulio wa mwana mzaliwa-pekee+ kutoka kwa baba; naye alikuwa amejaa fadhili nyingi zisizostahiliwa na kweli.+ 15  (Yohana alitoa ushahidi juu yake, ndiyo, kwa kweli alipaaza sauti​—​huyu ndiye aliyesema hilo​—​akisema: “Yule anayekuja nyuma yangu amekwenda mbele yangu, kwa sababu alikuwako kabla yangu.”)+ 16  Kwa maana sisi sote tulipokea kutokana na wingi alio nao,+ hata fadhili zisizostahiliwa juu ya fadhili zisizostahiliwa.+ 17  Kwa sababu Sheria ilitolewa kupitia Musa,+ fadhili zisizostahiliwa+ na kweli+ zilikuja kupitia Yesu Kristo. 18  Hakuna mwanadamu ambaye amemwona Mungu wakati wowote;+ mungu mzaliwa-pekee+ aliye kifuani+ pa Baba, ndiye ambaye ameeleza juu yake.+ 19  Basi huu ndio ushahidi wa Yohana wakati Wayahudi walipowatuma makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu wakamuulize: “Wewe ni nani?”+ 20  Naye alikiri wala hakukana, bali akakiri: “Mimi siye Kristo.”+ 21  Nao wakamuuliza: “Wewe ni nani, basi? Je, wewe ndiye Eliya?”+ Naye akasema: “Mimi siye.” “Je, wewe ndiye Yule Nabii?”+ Naye akajibu: “Hapana!” 22  Kwa hiyo wakamwambia: “Wewe ni nani? ili tupate kuwajibu wale waliotutuma. Unasema nini juu yako mwenyewe?”+ 23  Akasema: “Mimi ni sauti ya mtu anayepaaza sauti nyikani, ‘Nyoosheni njia ya Yehova,’ kama vile nabii Isaya alivyosema.”+ 24  Sasa wale waliotumwa walikuwa wametoka kwa Mafarisayo. 25  Kwa hiyo walimuuliza na kumwambia: “Kwa nini, basi, unabatiza+ ikiwa wewe mwenyewe siye Kristo au Eliya au Yule Nabii?” 26  Yohana akawajibu, akisema: “Mimi ninabatiza katika maji. Kuna mmoja ambaye amesimama katikati+ yenu msiyemjua,+ 27  yule anayekuja nyuma yangu, lakini ambaye kamba ya kiatu chake sistahili kuifungua.”+ 28  Mambo hayo yalitendeka Bethania ng’ambo ya Yordani, ambako Yohana alikuwa akibatizia.+ 29  Siku iliyofuata alimwona Yesu akimjia, naye akasema: “Ona, Mwana-Kondoo+ wa Mungu ambaye huondolea mbali dhambi+ ya ulimwengu!+ 30  Huyu ndiye niliyesema juu yake, Nyuma yangu anakuja mwanamume ambaye yuko mbele yangu, kwa sababu alikuwako kabla yangu.+ 31  Hata sikumjua, lakini nilikuja nikibatiza katika maji ili apate kufunuliwa kwa Israeli.”+ 32  Yohana pia alitoa ushahidi, akisema: “Niliona roho ikishuka kama njiwa kutoka mbinguni, nayo ikakaa juu yake.+ 33  Hata sikumjua, bali Yule aliyenituma+ nibatize katika maji aliniambia, ‘Yeyote yule ambaye utaona roho ikishuka na kukaa juu yake, huyo ndiye ambaye hubatiza katika roho takatifu.’+ 34  Nami nimeona, na nimetoa ushahidi kwamba huyo ndiye Mwana wa Mungu.”+ 35  Tena siku iliyofuata Yohana alikuwa amesimama na wawili kati ya wanafunzi wake, 36  na alipomtazama Yesu akitembea akasema: “Ona, Mwana-Kondoo+ wa Mungu!” 37  Na wanafunzi hao wawili wakamsikia akisema, nao wakamfuata Yesu. 38  Ndipo Yesu akageuka na, alipowaona wakimfuata, akawaambia: “Mnatafuta nini?” Wakamwambia: “Rabi, (ambalo linapotafsiriwa humaanisha, Mwalimu,) unakaa wapi?” 39  Akawaambia: “Njooni, nanyi mtaona.”+ Basi wakaenda wakaona ni wapi alikokuwa akikaa, nao wakakaa pamoja naye siku hiyo; ilikuwa karibu saa kumi. 40  Andrea+ ndugu ya Simoni Petro alikuwa mmoja kati ya wale wawili waliosikia aliyoyasema Yohana nao wakamfuata Yesu. 41  Kwanza huyu alimpata ndugu yake mwenyewe, Simoni, na kumwambia: “Tumempata Masihi”+ (ambalo linapotafsiriwa humaanisha, Kristo).+ 42  Akampeleka kwa Yesu. Yesu alipomtazama+ akasema: “Wewe ni Simoni+ mwana wa Yohana;+ utaitwa Kefa” (ambalo linatafsiriwa Petro).+ 43  Siku iliyofuata alitamani kuondoka kwenda Galilaya. Kwa hiyo Yesu akamkuta Filipo+ na kumwambia: “Uwe mfuasi wangu.”+ 44  Basi Filipo alikuwa mtu wa Bethsaida,+ kutoka jiji la Andrea na Petro. 45  Filipo akamkuta Nathanaeli+ na kumwambia: “Tumempata yule ambaye Musa, katika Sheria,+ na Manabii,+ aliandika juu yake, Yesu, mwana wa Yosefu,+ kutoka Nazareti.” 46  Lakini Nathanaeli akamwambia: “Je, kitu chochote kilicho chema kinaweza kutoka Nazareti?”+ Filipo akamwambia: “Njoo uone.” 47  Yesu akamwona Nathanaeli akimjia na kusema juu yake: “Ona, Mwisraeli kwa uhakika, ambaye hamna udanganyifu ndani yake.”+ 48  Nathanaeli akamwambia: “Umepataje kunijua?” Yesu akajibu, akamwambia: “Kabla ya Filipo kukuita, ulipokuwa chini ya mtini, nilikuona.” 49  Nathanaeli akamjibu: “Rabi, wewe ndiye Mwana wa Mungu,+ wewe ndiye Mfalme+ wa Israeli.” 50  Yesu akajibu, akamwambia: “Je, unaamini kwa sababu nilikuambia nilikuona chini ya mtini? Utaona mambo makubwa zaidi kuliko haya.” 51  Akazidi kumwambia: “Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, Mtaona mbingu imefunguliwa na malaika+ za Mungu wakipanda na kushuka mpaka kwa Mwana wa binadamu.”+

Maelezo ya Chini