Yohana 1:1-51
1 Hapo mwanzo+ Neno+ alikuwako, na Neno alikuwa pamoja na Mungu,+ na Neno alikuwa mungu.+
2 Hapo mwanzo+ huyo alikuwa pamoja na Mungu.+
3 Vitu vyote vilikuja kuwako kupitia kwake,+ na bila yeye hakuna hata kitu kimoja kilichokuja kuwako.
Kile ambacho kimekuja kuwako
4 kupitia kwake kilikuwa uzima,+ na uzima ndio uliokuwa nuru+ ya wanadamu.
5 Na nuru inang’aa katika giza,+ lakini giza halijaizidi nguvu.
6 Kulitokea mtu aliyetumwa awe mwakilishi wa Mungu:+ jina lake lilikuwa Yohana.+
7 Mtu huyo alikuja kwa ajili ya ushahidi, ili atoe ushahidi+ juu ya nuru,+ kusudi watu wa namna zote wapate kuamini kupitia kwake.+
8 Yeye hakuwa nuru hiyo,+ bali alikusudiwa atoe ushahidi+ juu ya nuru hiyo.
9 Nuru+ ya kweli ambayo humpa nuru+ mtu wa kila namna,+ ilikuwa karibu kuja ulimwenguni.
10 Alikuwa ulimwenguni,+ nao ulimwengu ulikuja kuwako kupitia kwake,+ lakini ulimwengu haukumjua.
11 Alikuja nyumbani kwake mwenyewe, lakini watu wake mwenyewe hawakumkaribisha.+
12 Hata hivyo, wengi kadiri ileile waliompokea,+ aliwapa mamlaka ya kuwa watoto wa Mungu,+ kwa sababu walikuwa wakionyesha imani katika jina lake;+
13 nao walizaliwa, si kutokana na damu au kutokana na mapenzi ya mwili au kutokana na mapenzi ya mwanadamu, bali kutokana na Mungu.+
14 Kwa hiyo Neno akawa mwili,+ akakaa katikati yetu, nasi tukautazama utukufu wake, utukufu kama ule ulio wa mwana mzaliwa-pekee+ kutoka kwa baba; naye alikuwa amejaa fadhili nyingi zisizostahiliwa na kweli.+
15 (Yohana alitoa ushahidi juu yake, ndiyo, kwa kweli alipaaza sauti—huyu ndiye aliyesema hilo—akisema: “Yule anayekuja nyuma yangu amekwenda mbele yangu, kwa sababu alikuwako kabla yangu.”)+
16 Kwa maana sisi sote tulipokea kutokana na wingi alio nao,+ hata fadhili zisizostahiliwa juu ya fadhili zisizostahiliwa.+
17 Kwa sababu Sheria ilitolewa kupitia Musa,+ fadhili zisizostahiliwa+ na kweli+ zilikuja kupitia Yesu Kristo.
18 Hakuna mwanadamu ambaye amemwona Mungu wakati wowote;+ mungu mzaliwa-pekee+ aliye kifuani+ pa Baba, ndiye ambaye ameeleza juu yake.+
19 Basi huu ndio ushahidi wa Yohana wakati Wayahudi walipowatuma makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu wakamuulize: “Wewe ni nani?”+
20 Naye alikiri wala hakukana, bali akakiri: “Mimi siye Kristo.”+
21 Nao wakamuuliza: “Wewe ni nani, basi? Je, wewe ndiye Eliya?”+ Naye akasema: “Mimi siye.” “Je, wewe ndiye Yule Nabii?”+ Naye akajibu: “Hapana!”
22 Kwa hiyo wakamwambia: “Wewe ni nani? ili tupate kuwajibu wale waliotutuma. Unasema nini juu yako mwenyewe?”+
23 Akasema: “Mimi ni sauti ya mtu anayepaaza sauti nyikani, ‘Nyoosheni njia ya Yehova,’ kama vile nabii Isaya alivyosema.”+
24 Sasa wale waliotumwa walikuwa wametoka kwa Mafarisayo.
25 Kwa hiyo walimuuliza na kumwambia: “Kwa nini, basi, unabatiza+ ikiwa wewe mwenyewe siye Kristo au Eliya au Yule Nabii?”
26 Yohana akawajibu, akisema: “Mimi ninabatiza katika maji. Kuna mmoja ambaye amesimama katikati+ yenu msiyemjua,+
27 yule anayekuja nyuma yangu, lakini ambaye kamba ya kiatu chake sistahili kuifungua.”+
28 Mambo hayo yalitendeka Bethania ng’ambo ya Yordani, ambako Yohana alikuwa akibatizia.+
29 Siku iliyofuata alimwona Yesu akimjia, naye akasema: “Ona, Mwana-Kondoo+ wa Mungu ambaye huondolea mbali dhambi+ ya ulimwengu!+
30 Huyu ndiye niliyesema juu yake, Nyuma yangu anakuja mwanamume ambaye yuko mbele yangu, kwa sababu alikuwako kabla yangu.+
31 Hata sikumjua, lakini nilikuja nikibatiza katika maji ili apate kufunuliwa kwa Israeli.”+
32 Yohana pia alitoa ushahidi, akisema: “Niliona roho ikishuka kama njiwa kutoka mbinguni, nayo ikakaa juu yake.+
33 Hata sikumjua, bali Yule aliyenituma+ nibatize katika maji aliniambia, ‘Yeyote yule ambaye utaona roho ikishuka na kukaa juu yake, huyo ndiye ambaye hubatiza katika roho takatifu.’+
34 Nami nimeona, na nimetoa ushahidi kwamba huyo ndiye Mwana wa Mungu.”+
35 Tena siku iliyofuata Yohana alikuwa amesimama na wawili kati ya wanafunzi wake,
36 na alipomtazama Yesu akitembea akasema: “Ona, Mwana-Kondoo+ wa Mungu!”
37 Na wanafunzi hao wawili wakamsikia akisema, nao wakamfuata Yesu.
38 Ndipo Yesu akageuka na, alipowaona wakimfuata, akawaambia: “Mnatafuta nini?” Wakamwambia: “Rabi, (ambalo linapotafsiriwa humaanisha, Mwalimu,) unakaa wapi?”
39 Akawaambia: “Njooni, nanyi mtaona.”+ Basi wakaenda wakaona ni wapi alikokuwa akikaa, nao wakakaa pamoja naye siku hiyo; ilikuwa karibu saa kumi.
40 Andrea+ ndugu ya Simoni Petro alikuwa mmoja kati ya wale wawili waliosikia aliyoyasema Yohana nao wakamfuata Yesu.
41 Kwanza huyu alimpata ndugu yake mwenyewe, Simoni, na kumwambia: “Tumempata Masihi”+ (ambalo linapotafsiriwa humaanisha, Kristo).+
42 Akampeleka kwa Yesu. Yesu alipomtazama+ akasema: “Wewe ni Simoni+ mwana wa Yohana;+ utaitwa Kefa” (ambalo linatafsiriwa Petro).+
43 Siku iliyofuata alitamani kuondoka kwenda Galilaya. Kwa hiyo Yesu akamkuta Filipo+ na kumwambia: “Uwe mfuasi wangu.”+
44 Basi Filipo alikuwa mtu wa Bethsaida,+ kutoka jiji la Andrea na Petro.
45 Filipo akamkuta Nathanaeli+ na kumwambia: “Tumempata yule ambaye Musa, katika Sheria,+ na Manabii,+ aliandika juu yake, Yesu, mwana wa Yosefu,+ kutoka Nazareti.”
46 Lakini Nathanaeli akamwambia: “Je, kitu chochote kilicho chema kinaweza kutoka Nazareti?”+ Filipo akamwambia: “Njoo uone.”
47 Yesu akamwona Nathanaeli akimjia na kusema juu yake: “Ona, Mwisraeli kwa uhakika, ambaye hamna udanganyifu ndani yake.”+
48 Nathanaeli akamwambia: “Umepataje kunijua?” Yesu akajibu, akamwambia: “Kabla ya Filipo kukuita, ulipokuwa chini ya mtini, nilikuona.”
49 Nathanaeli akamjibu: “Rabi, wewe ndiye Mwana wa Mungu,+ wewe ndiye Mfalme+ wa Israeli.”
50 Yesu akajibu, akamwambia: “Je, unaamini kwa sababu nilikuambia nilikuona chini ya mtini? Utaona mambo makubwa zaidi kuliko haya.”
51 Akazidi kumwambia: “Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, Mtaona mbingu imefunguliwa na malaika+ za Mungu wakipanda na kushuka mpaka kwa Mwana wa binadamu.”+