Yeremia 9:1-26

9  Laiti kichwa changu kingekuwa maji, na macho yangu yangekuwa chemchemi ya machozi!+ Ndipo ningelia usiku na mchana kwa ajili ya waliouawa wa binti ya watu wangu.+  Laiti ningekuwa na mahali pa kukaa wasafiri+ katika nyika! Ndipo ningewaacha watu wangu na kwenda mbali nao, kwa maana wote ni wazinzi,+ kusanyiko kuu la wanaofanya hila;+  nao wanapinda ulimi wao uwe upinde wao katika uwongo;+ lakini katika uaminifu hawajaonyesha kuwa ni wenye nguvu katika nchi. “Kwa maana walienda kutoka ubaya mpaka ubaya, nao walinipuuza hata mimi,”+ asema Yehova.  “Jihadharini kila mmoja na rafiki yake,+ wala msimtegemee ndugu hata kidogo.+ Kwa maana kila ndugu hakika atanyakua mahali pa mwingine,+ na kila rafiki atatembea huku na huku akiwa mchongezi,+  nao wanaendelea kumchezea kila mmoja rafiki yake;+ nao hawasemi ukweli hata kidogo. Wameufundisha ulimi wao kusema uwongo.+ Wamejichosha tu katika kufanya kosa.+  “Unaketi katikati ya udanganyifu.+ Kupitia udanganyifu wamekataa kunijua mimi,”+ asema Yehova.  Kwa hiyo Yehova wa majeshi amesema hivi: “Tazama, ninawayeyusha, nami lazima niwachunguze,+ kwa sababu nitatendaje vinginevyo kwa ajili ya binti ya watu wangu?+  Ulimi wao ni mshale unaoua.+ Huo umesema udanganyifu. Kwa kinywa chake, mtu anaendelea kusema amani pamoja na mwenzake; lakini ndani yake anaweka mavizio yake.”+  “Kwa sababu ya mambo hayo, je, nisiwatoze wao hesabu?” asema Yehova. “Au, je, nafsi yangu isijilipizie kisasi juu ya taifa ambalo liko hivyo?+ 10  Nitapaaza kilio na maombolezo juu ya milima, na wimbo wa huzuni+ juu ya viwanja vya malisho; kwa maana vitakuwa vimeteketezwa+ hivi kwamba hakuna mwanadamu anayepita katikati na kwa kweli watu hawataisikia sauti ya mifugo.+ Kiumbe kinachoruka cha mbinguni na mnyama watakuwa wamekimbia; watakuwa wameenda.+ 11  Nami nitafanya Yerusalemu kuwa rundo la mawe,+ mapango ya mbwa-mwitu;+ na majiji ya Yuda nitayafanya kuwa mahame yenye ukiwa, bila mkaaji.+ 12  “Ni mwanadamu yupi ambaye ana hekima, ili aelewe jambo hili, yule ambaye kinywa cha Yehova kimesema naye, ili aseme jambo hili?+ Kwa nini nchi iangamie, kwa kweli iteketezwe kama nyika bila yeyote wa kupita katikati?”+ 13  Na Yehova akasema: “Kwa sababu wameiacha sheria yangu ambayo nilitoa iwe mbele yao, na kwa sababu hawakuitii sauti yangu wala kutembea ndani yake,+ 14  lakini waliendelea kufuata ukaidi wa moyo+ wao na sanamu za Baali,+ ambazo baba zao walikuwa wamewafundisha;+ 15  kwa hiyo Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Tazama, mimi ninawafanya wao, yaani, watu hawa, kula pakanga,+ nami nitawafanya kunywa maji yaliyotiwa sumu;+ 16  nami nitawatawanya kati ya mataifa ambayo wao wala baba zao hawakuyajua,+ nami nitatuma upanga uwafuate mpaka nitakapowaangamiza.’+ 17  “Yehova wa majeshi amesema hivi, ‘Jiendesheni kwa uelewaji, na kuwaita wanawake wanaoimba nyimbo za huzuni,+ ili waje; na iteni wanawake stadi, ili waje,+ 18  na ili wafanye haraka na kufanya maombolezo juu yetu. Macho yetu na yatiririke machozi, macho yetu yanayong’aa na yatiririke maji.+ 19  Kwa maana ni sauti ya maombolezo ambayo imesikiwa kutoka Sayuni:+ “Jinsi tulivyoporwa!+ Jinsi tulivyoona aibu! Kwa maana tumeiacha nchi; kwa maana wameyatupilia mbali makao yetu.”+ 20  Lakini lisikieni neno la Yehova, enyi wanawake, na sikio lenu lichukue neno la kinywa chake. Kisha mwafundishe binti zenu maombolezo,+ na kila mwanamke amfundishe mwenzake wimbo wa huzuni.+ 21  Kwa maana kifo kimekuja kupitia madirisha yetu; kimeingia ndani ya minara ya makao yetu, ili kumkatilia mbali mtoto kutoka barabarani, vijana kutoka katika viwanja vya watu wote.’+ 22  “Sema, ‘Yehova asema hivi: “Maiti za wanadamu zitaanguka kama mbolea juu ya uso wa uwanja na kama mafungu ya nafaka iliyokatwa hivi karibuni nyuma ya mvunaji, bila yeyote wa kukusanya.”’”+ 23  Yehova amesema hivi: “Mtu mwenye hekima asijigambe kwa sababu ya hekima yake,+ wala mwanamume mwenye nguvu asijigambe kwa sababu ya nguvu zake.+ Mtu tajiri asijigambe kwa sababu ya utajiri wake.”+ 24  “Lakini yule anayejigamba na ajigambe kwa sababu ya jambo hili, kuwa na ufahamu+ na kuwa na ujuzi kunihusu mimi, kwamba mimi ni Yehova,+ Yeye anayeonyesha fadhili zenye upendo, haki na uadilifu duniani;+ kwa maana mimi hupendezwa na mambo hayo,”+ asema Yehova. 25  “Tazama! Siku zinakuja,” asema Yehova, “nami nitamtoza hesabu kila mtu aliyetahiriwa lakini ambaye bado yumo katika hali ya kutotahiriwa,+ 26  juu ya Misri+ na juu ya Yuda+ na juu ya Edomu+ na juu ya wana wa Amoni+ na juu ya Moabu+ na juu ya wote wenye nywele zilizokatwa kwenye vipaji vya nyuso wanaokaa nyikani;+ kwa maana mataifa yote hayakutahiriwa, na nyumba yote ya Israeli hawakutahiriwa moyoni.”+

Maelezo ya Chini