Yeremia 7:1-34
7 Neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Yehova, likisema:
2 “Simama katika lango la nyumba ya Yehova, nawe utangaze hapo neno hili,+ na kusema, ‘Sikieni neno la Yehova, ninyi nyote wa Yuda, mnaoingia katika malango haya ili kumwinamia Yehova.
3 Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi: “Fanyeni njia zenu na matendo yenu kuwa mema, nami nitaendelea kuwakalisha mahali hapa.+
4 Msiyategemee maneno ya uwongo,+ mkisema, ‘Hekalu la Yehova, hekalu la Yehova, hili ni hekalu la Yehova!’
5 Kwa maana ikiwa hakika mtazifanya njia zenu na matendo yenu kuwa mema, ikiwa hakika mtatenda haki kati ya mtu na mwenzake,+
6 ikiwa hamtamkandamiza mkaaji mgeni, mvulana asiye na baba na mjane,+ nanyi hamtamwaga damu isiyo na hatia mahali hapa,+ hamtaifuata miungu mingine ili kujiletea wenyewe msiba,+
7 mimi, nami, hakika nitaendelea kuwakalisha mahali hapa, katika nchi ambayo niliwapa mababu zenu, kutoka wakati usio na kipimo mpaka wakati usio na kipimo.”’”+
8 “Tazama, mnayategemea maneno ya uwongo—hakika haitakuwa na faida yoyote kamwe.+
9 Je, inawezekana kuwe wizi,+ uuaji+ na uzinzi+ na kuapa kwa uwongo+ na kumfukizia Baali moshi+ wa dhabihu na kuifuata miungu mingine ambayo hamkuijua,+
10 nanyi mje na kusimama mbele zangu katika nyumba hii ambayo jina langu limeitwa juu yake,+ na kusema, ‘Hakika tutakombolewa,’ huku mkiyafanya machukizo haya yote?
11 Je, nyumba hii ambayo jina langu limeitwa juu yake,+ imekuwa pango tu la wanyang’anyi machoni penu?+ Tazama, mimi mwenyewe pia nimeona jambo hilo,” asema Yehova.+
12 “‘Hata hivyo, nendeni, sasa, mahali pangu palipokuwa katika Shilo,+ ambapo nilifanya jina langu likae hapo pale mwanzoni,+ na kuona nilivyopafanya kwa sababu ya ubaya wa watu wangu Israeli.+
13 Na sasa kwa sababu mliendelea kufanya kazi hizi zote,’ asema Yehova, ‘nami nikaendelea kusema nanyi, nikiamka mapema na kusema,+ lakini hamkusikiliza,+ nami nikaendelea kuwaita, lakini hamkujibu,+
14 nitaitendea pia nyumba ambayo jina langu limeitwa juu yake,+ ambayo mnaitegemea,+ na mahali ambapo niliwapa ninyi na mababu zenu, kama nilivyotendea Shilo.+
15 Nami nitawatupa ninyi nje kutoka mbele za macho yangu,+ kama nilivyowatupa nje ndugu zenu wote, uzao wote wa Efraimu.’+
16 “Nawe usisali kwa ajili ya watu hawa, wala usipaaze kilio cha kusihi kwa ajili yao wala sala wala kuniomba,+ kwa maana sitakusikiliza.+
17 Je, wewe huoni yale wanayofanya katika majiji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu?+
18 Wana wanaokota kuni, na akina baba wanawasha moto, na wake wanakanda unga ili kumfanyia ‘malkia wa mbingu’ keki za dhabihu;+ na miungu mingine inamiminiwa matoleo ya kinywaji+ kusudi wanitie uchungu.+
19 ‘Je, wananitia mimi uchungu?’ asema Yehova.+ ‘Je, si wao wenyewe, kusudi watie nyuso zao aibu?’+
20 Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Tazama! Hasira yangu na ghadhabu yangu zinamwagwa juu ya mahali hapa,+ juu ya mwanadamu na juu ya mnyama wa kufugwa, na juu ya mti wa shambani+ na juu ya mazao ya udongo; nayo itateketeza, wala haitazimwa.’+
21 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Ongezeni hayo matoleo yenu mazima ya kuteketezwa kwenye dhabihu zenu na kula nyama.+
22 Kwa maana sikusema na mababu zenu, wala sikuwaamuru wao katika siku nilipowatoa katika nchi ya Misri, kuhusu mambo ya toleo zima la kuteketezwa na dhabihu.+
23 Lakini niliwaamuru neno hili, nikisema: “Tiini sauti yangu,+ nami nitakuwa Mungu wenu,+ nanyi mtakuwa watu wangu; na mtembee katika njia+ yote ambayo nitawaamuru ninyi, ili iwe vema kwenu.”’+
24 Lakini hawakusikiliza, wala hawakutega sikio lao,+ bali wakatembea katika mashauri kwa ukaidi wa moyo wao mbaya,+ hivi kwamba wakawa watu wa kuelekea nyuma wala si mbele,+
25 tangu siku ile mababu zenu walipotoka katika nchi ya Misri mpaka leo hii;+ nami niliendelea kuwatumia ninyi watumishi wangu wote manabii, nikiamka mapema kila siku na kuwatuma.+
26 Lakini hawakunisikiliza, nao hawakutega sikio lao,+ bali waliendelea kufanya shingo yao kuwa ngumu.+ Walitenda vibaya zaidi kuliko mababu zao!+
27 “Nawe utawaambia maneno haya yote,+ lakini hawatakusikiliza; nawe utawaita, lakini hawatakujibu.+
28 Nawe utawaambia, ‘Hili ndilo taifa ambalo watu wake hawakuitii sauti ya Yehova Mungu wake,+ nao hawakushika nidhamu.+ Uaminifu umeangamia, nao umekatiliwa mbali kutoka katika kinywa chao.’+
29 “Nyoa nywele zako ambazo hazijakatwa na kuzitupilia mbali,+ na kuimba wimbo wa huzuni+ juu ya vilima vilivyo wazi, kwa maana Yehova amekikataa+ naye atakiacha kizazi ambacho amekighadhibikia.+
30 ‘Kwa maana wana wa Yuda wamefanya mambo mabaya machoni pangu,’ asema Yehova. ‘Wameyaweka machukizo yao katika nyumba ambayo jina langu limeitwa juu yake, ili kuitia unajisi.+
31 Nao wamejenga mahali pa juu pa Tofethi,+ palipo katika bonde la mwana wa Hinomu,+ ili kuwateketeza wana wao na binti zao katika moto,+ jambo ambalo sikuamuru wala halikuingia moyoni mwangu.’+
32 “‘Kwa hiyo, tazama! siku zinakuja,’ asema Yehova, ‘wakati halitaitwa tena Tofethi na bonde la mwana wa Hinomu, bali bonde la uuaji;+ nao watazika katika Tofethi bila ya kuwa na nafasi ya kutosha hapo.+
33 Na maiti za watu hawa zitakuwa chakula cha viumbe vinavyoruka vya mbinguni na cha wanyama wa dunia, pasipo mtu yeyote wa kuwatetemesha.+
34 Nami nitaikomesha sauti ya kufurahi na sauti ya kushangilia kutoka katika majiji ya Yuda na kutoka katika barabara za Yerusalemu sauti ya bwana-arusi na sauti ya bibi-arusi;+ kwa maana nchi itakuwa mahali palipofanywa ukiwa.’”+