Yeremia 6:1-30
6 Kimbilieni usalama, enyi wana wa Benyamini, kutoka katikati ya Yerusalemu; nanyi mpige baragumu+ katika Tekoa.+ Na mwinue ishara ya moto katika Beth-hakeremu;+ kwa sababu msiba umetazama chini kutoka upande wa kaskazini, mshindo mkubwa.+
2 Binti Sayuni amefanana kweli na mwanamke mwenye kupendeza na aliye laini.+
3 Wachungaji na makundi yao walimjia. Walisimamisha mahema yao pande zote juu yake.+ Kila mmoja alilisha sehemu yake.+
4 Wametakasa vita juu yake:+ “Simameni, na acheni tupande katikati ya mchana!”+
“Ole wetu, kwa maana mchana umepungua, kwa maana vivuli vya jioni vinaendelea kurefuka!”
5 “Simameni, twende wakati wa usiku, tukaiharibu minara ya makao yake.”+
6 Kwa maana Yehova wa majeshi amesema hivi: “Kateni miti+ na mjenge boma la kuzingira+ Yerusalemu. Yeye ni jiji ambalo lazima litozwe hesabu.+ Yeye ni ukandamizaji mtupu katikati yake.+
7 Kama tangi linavyoweka maji yake yakiwa baridi, ndivyo yeye alivyouweka ubaya wake ukiwa baridi. Jeuri na uporaji zimesikiwa ndani yake;+ ugonjwa na tauni ziko mbele za uso wangu sikuzote.
8 Urekebishwe,+ Ee Yerusalemu, ili nafsi yangu isije ikaondoka kwako ikiwa imechukizwa;+ ili nisije nikakuweka uwe mahame yenye ukiwa, nchi isiyokaliwa.”+
9 Yehova wa majeshi amesema hivi: “Bila shaka wataokota mabaki ya Israeli kama mzabibu.+ Rudisha mkono wako nyuma kama mtu anayekusanya zabibu juu ya vikonyo vya mzabibu.”
10 “Nitasema na nani na kumpa nani onyo, ili wasikie? Tazama! Sikio lao halijatahiriwa, hivi kwamba hawawezi kusikiliza.+ Tazama! Neno la Yehova limekuwa shutuma+ kwao, na katika neno hilo wao hawawezi kupendezwa.+
11 Nami nimejawa na ghadhabu ya Yehova. Nimechoka kujizuia.”+
“Imwage wakati uleule juu ya mtoto aliye barabarani+ na juu ya kikundi cha vijana walio rafiki za karibu; kwa maana wao pia watakamatwa, mwanamume pamoja na mke wake, mzee pamoja na mtu mwenye siku nyingi.+
12 Na nyumba zao hakika zitapewa wengine ili wazimiliki, na mashamba na wake vilevile.+ Kwa maana nitanyoosha mkono wangu juu ya wakaaji wa nchi,” asema Yehova.+
13 “Kwa maana kuanzia aliye mdogo zaidi kati yao mpaka aliye mkubwa zaidi kati yao, kila mmoja anajipatia pato lisilo la haki;+ na kuanzia nabii mpaka kuhani, kila mmoja anatenda kwa uwongo.+
14 Nao wanajaribu kuponya kijuujuu kuvunjika kwa watu wangu,+ wakisema, ‘Kuna amani! Kuna amani!’ wakati hakuna amani.+
15 Je, waliona aibu kwa sababu jambo walilokuwa wamefanya lilikuwa chukizo?+ Jambo moja ni kwamba hakika wao hawaoni aibu yoyote; jambo lingine ni kwamba hawajapata kujua hata jinsi ya kufedheheka.+ Kwa hiyo wataanguka katikati ya wale wanaoanguka;+ watajikwaa wakati nitakapowatoza hesabu,” Yehova amesema.
16 Yehova amesema hivi: “Simameni tuli katika njia, na kuona, na kuuliza juu ya barabara za zamani za kale, mahali ambapo sasa pana njia nzuri;+ na mtembee ndani yake,+ na kustarehesha nafsi zenu.”+ Lakini waliendelea kusema: “Hatutatembea.”+
17 “Nami nilisimamisha walinzi juu yenu,+ ‘Isikilizeni sauti ya baragumu!’”+ Lakini waliendelea kusema: “Hatutaisikiliza.”+
18 “Kwa hiyo sikieni, enyi mataifa! Nawe ujue, Ee kusanyiko, jambo litakalokuwa katikati yao.
19 Sikiliza, Ee dunia! Tazama, ninaleta msiba juu ya watu+ hawa kama matunda ya fikira zao,+ kwa maana hawakuyasikiliza maneno yangu; na sheria yangu—pia waliendelea kuikataa.”+
20 “Ina faida gani kwangu kwamba mnaleta ubani kutoka Sheba+ na kane nzuri kutoka katika nchi ya mbali? Matoleo yenu mazima ya kuteketezwa hayaleti furaha,+ na dhabihu zenu hazikunipendeza mimi.”+
21 Kwa hiyo Yehova amesema hivi: “Tazama, ninawawekea watu hawa vikwazo,+ nao hakika watajikwaa juu yake, akina baba na wana pamoja; jirani na mwenzake—wataangamia.”+
22 Yehova amesema hivi: “Tazama! Kikundi cha watu kinakuja kutoka nchi ya kaskazini, na kuna taifa kubwa litakaloamshwa kutoka sehemu za mbali zaidi za dunia.+
23 Watashika upinde na mkuki.+ Ni katili, nao hawatakuwa na huruma. Sauti yao itavuma kama bahari,+ nao watapanda juu ya farasi.+ Limejipanga katika utaratibu wa vita kama mwanamume wa vita juu yako, Ee binti Sayuni.”+
24 Tumesikia habari zake. Mikono yetu imelegea.+ Taabu imetushika, maumivu ya kuzaa kama ya mwanamke anayezaa.+
25 Usiende nje shambani, wala usitembee njiani; kwa maana kuna upanga wa adui, kuna woga pande zote.+
26 Ee binti ya watu wangu, vaa nguo ya gunia+ na ugaegae katika majivu.+ Omboleza kama kumwombolezea mwana wa pekee, kilio cha uchungu;+ kwa sababu mporaji atakuja juu yetu kwa ghafula.+
27 “Nimekufanya wewe kuwa mpimaji wa madini katikati ya watu wangu, mtu anayefanya uchunguzi kamili; nawe utaangalia nawe utaichunguza njia yao.+
28 Wote ni watu wakaidi zaidi,+ wanaotembea wakiwa wachongezi+—shaba na chuma. Wote ni wenye kuharibu.+
29 Mivukuto+ imeunguzwa. Risasi inatoka ndani ya moto wao.+ Mtu ameendelea kusafisha sana kwa ubatili tu, na wale wabaya hawakutengwa.+
30 Hakika watu watawaita fedha iliyokataliwa,+ kwa maana Yehova amewakataa.”+