Yeremia 51:1-64
51 Yehova amesema hivi: “Tazama, ninaamsha upepo wenye kuharibu juu ya Babiloni+ na juu ya wakaaji wa Leb-kamai;+
2 nami nitatuma Babiloni wapepetaji ambao kwa hakika watampepeta na kuifanya nchi yake kuwa tupu;+ kwa maana kwa kweli watakuwa juu yake pande zote katika siku ya msiba.+
3 “Yeye anayekanyaga upinde wake na asikanyage.+ Na yeyote asisimame akiwa amevaa vazi lake la chuma.
“Nanyi msiwahurumie vijana wake.+ Liangamizeni jeshi lake lote.+
4 Nao wataanguka wakiwa wameuawa katika nchi ya Wakaldayo+ na wakiwa wamechomwa katika barabara zake.+
5 “Kwa maana Israeli na Yuda+ hawajafanywa wajane kutoka kwa Mungu wao, kutoka kwa Yehova wa majeshi.+ Kwa maana nchi ya hao imejawa na hatia machoni pa Mtakatifu wa Israeli.+
6 “Kimbieni kutoka katikati ya Babiloni,+ na kila mmoja wenu aiponye nafsi yake mwenyewe.+ Msifanywe kuwa wasio na uhai kupitia kosa lake.+ Kwa maana ni wakati wa kisasi cha Yehova.+ Kuna tendo ambalo anamlipa.+
7 Babiloni amekuwa kikombe cha dhahabu mkononi mwa Yehova,+ yeye anailewesha dunia yote.+ Mataifa yamekunywa kutokana na divai yake.+ Ndiyo sababu mataifa yanaendelea kutenda kiwazimu.+
8 Kwa ghafula Babiloni ameanguka, hivi kwamba amevunjwa.+ Pigeni mayowe juu yake.+ Chukueni zeri kwa ajili ya maumivu yake.+ Huenda akapona.”
9 “Tungemponya Babiloni, lakini yeye hakuponyeka. Mwacheni,+ nasi twende kila mmoja kwenye nchi yake mwenyewe.+ Kwa maana hukumu yake imefika mpaka mbinguni, nayo imeinuliwa mpaka kwenye anga lenye mawingu.+
10 Yehova ametuletea matendo ya uadilifu.+ Njooni na acheni sisi tusimulie katika Sayuni kazi ya Yehova Mungu wetu.”+
11 “Isugueni mishale.+ Jazeni ngao za mviringo. Yehova ameiamsha roho ya wafalme wa Wamedi,+ kwa sababu wazo lake liko juu ya Babiloni,+ ili kumharibu. Kwa maana hicho ni kisasi cha Yehova, kisasi kwa ajili ya hekalu lake.+
12 Inueni ishara+ juu ya kuta za Babiloni. Yatieni malindo nguvu.+ Wekeni walinzi. Watayarisheni wale wanaovizia.+ Kwa maana Yehova ametunga wazo naye pia hakika atafanya lile alilosema juu ya wakaaji wa Babiloni.”+
13 “Ee mwanamke unayekaa juu ya maji mengi,+ mwenye hazina nyingi,+ mwisho wako umekuja, kipimo+ chako cha kupata faida.+
14 Yehova wa majeshi ameapa kwa nafsi yake mwenyewe,+ ‘Nitakujaza watu, kama nzige,+ nao hakika watapiga kelele kwa kukuimbia.’+
15 Yeye ndiye Mtengenezaji wa dunia kwa nguvu zake,+ Yeye anayeifanya imara nchi yenye kuzaa+ kwa hekima yake,+ na Yeye ambaye kwa uelewaji+ wake alizitandaza mbingu.+
16 Kupitia sauti yake yeye huleta machafuko ya maji mbinguni, naye hufanya mivuke ipae kutoka katika mwisho wa dunia.+ Amefanya hata milango kwa ajili ya mvua,+ naye huleta upepo kutoka katika maghala yake.
17 Kila mtu amejiendesha kwa kukosa sana kutumia akili asiweze kujua.+ Kila fundi wa chuma ataona aibu kwa sababu ya sanamu ya kuchongwa;+ kwa maana sanamu yake ya kuyeyushwa ni uwongo,+ na hamna roho ndani ya hizo.+
18 Hizo ni ubatili,+ kazi ya mzaha.+ Wakati wa kuzikazia fikira, zitaangamia.+
19 “Yeye aliye Fungu la Yakobo si kama vitu hivyo,+ kwa maana yeye ndiye Mfanyizaji wa kila kitu,+ fimbo ya urithi wake.+ Yehova wa majeshi ndilo jina lake.”+
20 “Wewe ni rungu kwangu, kama silaha za vita,+ na kupitia wewe hakika nitayavunja mataifa vipande-vipande, na kupitia wewe nitaziangamiza falme.
21 Na kupitia wewe nitamvunja farasi na mpandaji wake vipande-vipande, na kupitia wewe nitalivunja gari la vita na mpandaji wake vipande-vipande.+
22 Na kupitia wewe nitamvunja mwanamume na mwanamke vipande-vipande, na kupitia wewe nitamvunja mzee na mvulana vipande-vipande, na kupitia wewe nitamvunja mwanamume kijana na bikira vipande-vipande.
23 Na kupitia wewe nitamvunja mchungaji na kundi lake vipande-vipande, na kupitia wewe nitamvunja mkulima na jozi yake ya wanyama vipande-vipande, na kupitia wewe nitawavunja magavana na watawala-wasaidizi vipande-vipande.
24 Nami nitamlipa Babiloni na wakaaji wote wa Ukaldayo ubaya wao wote ambao wametenda katika Sayuni mbele ya macho yenu,”+ asema Yehova.
25 “Tazama, mimi niko dhidi yako,+ Ee mlima wenye kuharibu,”+ asema Yehova, “wewe mwenye kuiharibu dunia yote;+ nami nitaunyoosha mkono wangu juu yako na kukuviringisha kutoka katika miamba na kukufanya kuwa mlima ulioteketezwa.”+
26 “Na watu hawatachukua kutoka kwako jiwe la pembeni wala jiwe kwa ajili ya misingi,+ kwa sababu wewe utakuwa mahame yenye ukiwa mpaka wakati usio na kipimo,”+ asema Yehova.
27 “Inueni ishara katika nchi.+ Pigeni baragumu kati ya mataifa. Takaseni+ mataifa juu yake. Iteni falme za Ararati,+ Mini na Ashkenazi+ zije juu yake. Wekeni juu yake ofisa mwandikishaji. Pandisheni+ farasi kama nzige waliojaa miiba.
28 Takaseni juu yake mataifa, wafalme wa Umedi,+ magavana wake na watawala-wasaidizi wake wote na nchi yote ya mamlaka ya kila mmoja.
29 Dunia itetemeke na kuwa katika maumivu makali,+ kwa maana fikira za Yehova zimeinuka juu ya Babiloni ili kuifanya nchi ya Babiloni kuwa kitu cha kushangaza, bila mkaaji.+
30 “Wanaume wenye nguvu wa Babiloni wameacha kupigana. Wameendelea kuketi katika mahali imara. Nguvu zao zimekauka.+ Wamekuwa wanawake.+ Makao yake yamewashwa moto. Mapingo yake yamevunjwa.+
31 “Mkimbiaji mmoja anakimbia ili kukutana na mkimbiaji mwingine, na mleta-habari mmoja ili kukutana na mleta-habari mwingine,+ kumletea habari mfalme wa Babiloni kwamba jiji lake limetekwa kwenye miisho yote,+
32 na kwamba vivuko vimeshikwa,+ na mashua zilizotengenezwa kwa mafunjo wameziteketeza kwa moto, na watu wa vita wameingiwa na hofu.”+
33 Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi: “Binti ya Babiloni ni kama uwanja wa kupuria.+ Ni wakati wa kumkanyagia chini awe mgumu. Bado kitambo kidogo na wakati wa mavuno utakuja kwa ajili yake.”+
34 “Nebukadreza mfalme wa Babiloni amenila;+ amenivuruga. Ameniweka kuwa kama chombo kitupu. Amenimeza kama nyoka mkubwa;+ amelijaza tumbo lake kwa vitu vyangu vyenye kupendeza. Amenioshea mbali.
35 ‘Jeuri niliyotendewa mimi na kutendewa mwili wangu na iwe juu ya Babiloni!’ mwanamke mkaaji wa Sayuni atasema.+ ‘Na damu yangu na iwe juu ya wakaaji wa Ukaldayo!’ Yerusalemu atasema.”+
36 Kwa hiyo Yehova amesema hivi: “Tazama, ninaendesha kesi yako,+ nami hakika nitalipiza kisasi kwa ajili yako.+ Nami nitaikausha bahari yake, nitavikausha visima vyake.+
37 Na Babiloni atakuwa marundo ya mawe,+ pango la mbwa-mwitu,+ kitu cha kushangaza na kitu cha kupigiwa mluzi, bila mkaaji.+
38 Wote pamoja watanguruma kama wana-simba wenye manyoya shingoni. Hakika watanguruma kama watoto wa simba.”
39 “Wakati watakapokuwa wamesisimuka nitaweka karamu zao na kuwalewesha, ili wafurahi;+ nao watalala usingizi unaodumu mpaka wakati usio na kipimo, ambamo hawataamka,”+ asema Yehova.
40 “Nitawashusha kama kondoo-dume kwenda machinjoni, kama kondoo-dume pamoja na mbuzi-dume.”+
41 “Jinsi Sheshaki alivyotekwa,+ na jinsi Sifa ya dunia yote ilivyokatwa!+ Jinsi Babiloni amekuwa kitu cha kushangaza katikati ya mataifa!+
42 Bahari imekuja juu ya Babiloni. Amefunikwa kwa wingi wa mawimbi yake.+
43 Majiji yake yamekuwa kitu cha kushangaza, nchi isiyo na maji na nchi tambarare ya jangwani.+ Kama nchi, ndani yao hakuna mtu atakayekaa, na katikati yao hakuna mwana wa binadamu atakayepita.+
44 Nami nitakaza fikira zangu juu ya Beli+ katika Babiloni, nami nitatoa katika kinywa chake kile ambacho amemeza.+ Na mataifa hayatamiminika kwake tena.+ Pia, lazima ukuta wenyewe wa Babiloni uanguke.+
45 “Tokeni katikati yake, enyi watu wangu,+ na kila mmoja aiponye nafsi yake+ kutoka kwenye hasira ya Yehova inayowaka.+
46 Au kama sivyo moyo wenu utakuwa na woga,+ nanyi mtaogopa kwa sababu ya habari ambayo itasikiwa katika nchi. Na habari hiyo itakuja katika muda wa mwaka mmoja, na baada yake katika muda wa mwaka mwingine kutakuwa na habari na jeuri katika dunia na mtawala juu ya mtawala.
47 Kwa hiyo, tazama! siku zinakuja, nami nitakaza fikira zangu juu ya sanamu za kuchongwa za Babiloni;+ na nchi yake yote itaona aibu, na watu wake wote waliouawa wataanguka katikati yake.+
48 “Na mbingu na dunia na vyote vilivyomo hakika vitapiga vigelegele vya shangwe juu ya Babiloni,+ kwa maana waporaji watakuja kwake kutoka kaskazini,”+ asema Yehova.
49 “Babiloni hakuwa tu kisababishi cha kuanguka kwa waliouawa wa Israeli+ lakini pia kule Babiloni waliouawa wa dunia yote wameanguka.+
50 “Ninyi mlioponyoka upanga, endeleeni kwenda. Msisimame tuli.+ Mkumbukeni Yehova kutoka mbali,+ Yerusalemu na aingie katika moyo wenu.”+
51 “Tumeona aibu,+ kwa maana tumesikia shutuma.+ Fedheha imefunika nyuso zetu,+ kwa maana wageni wamekuja juu ya mahali patakatifu pa nyumba ya Yehova.”+
52 “Kwa hiyo, tazama! siku zinakuja,” asema Yehova, “nami nitakaza fikira zangu juu ya sanamu zake za kuchongwa,+ na katika nchi yake yote aliyechomwa ataugua.”+
53 “Hata Babiloni akipaa juu mbinguni+ na hata akifanya kilele cha nguvu zake kisiweze kufikiwa,+ kutoka kwangu waporaji watakuja kwake,”+ asema Yehova.
54 “Sikilizeni! Kuna kilio kutoka Babiloni,+ na mshindo mkubwa kutoka nchi ya Wakaldayo,+
55 kwa maana Yehova anampora Babiloni, na hakika yeye ataangamiza kutoka ndani yake ile sauti kubwa,+ na mawimbi yao yatakuwa na machafuko kama maji mengi.+ Kelele za sauti yao hakika zitapigwa.
56 Kwa maana atakuja juu yake, juu ya Babiloni, mporaji,+ na wanaume wake wenye nguvu hakika watakamatwa.+ Pinde zao zitavunjwa-vunjwa,+ kwa maana Yehova ni Mungu wa malipo.+ Bila shaka atalipa.+
57 Nami nitawalewesha wakuu wake na watu wake wenye hekima, magavana wake na watawala-wasaidizi wake na wanaume wake wenye nguvu,+ nao watalala usingizi unaodumu mpaka wakati usio na kipimo, ambamo hawataweza kuamka,”+ asema Mfalme,+ ambaye jina lake ni Yehova wa majeshi.+
58 Yehova wa majeshi amesema hivi: “Ukuta wa Babiloni, ingawa ni mpana, bila shaka utabomolewa;+ na malango yake, ingawa ni marefu, yatawashwa moto.+ Na vikundi vya watu vitafanya kazi bure tu,+ na vikundi vya mataifa vitafanya kazi kwa ajili ya moto tu;+ nao watajichosha tu.”
59 Neno ambalo Yeremia nabii alimwamuru Seraya mwana wa Neria+ mwana wa Mahseya+ alipoenda pamoja na Sedekia mfalme wa Yuda kule Babiloni katika mwaka wa nne wa kuwa kwake mfalme; na Seraya ndiye aliyekuwa msimamizi wa makao.
60 Na Yeremia akaandika katika kitabu+ kimoja msiba wote ambao ungekuja juu ya Babiloni, haya maneno yote yaliyoandikwa juu ya Babiloni.
61 Na zaidi ya hayo, Yeremia akamwambia Seraya: “Mara tu utakapofika Babiloni na kumwona, lazima wewe pia uyasome kwa sauti maneno haya yote.+
62 Nawe useme, ‘Ee Yehova, wewe mwenyewe umesema juu ya mahali hapa, kupakatilia mbali ili kwamba mkaaji+ yeyote asiwe ndani yake, mwanadamu wala mnyama wa kufugwa, bali pawe mahame yenye ukiwa mpaka wakati usio na kipimo.’
63 Na itatukia kwamba utakapokuwa umemaliza kukisoma kitabu hiki, utakifunga kwenye jiwe, nawe lazima ukitupe katikati ya Efrati.+
64 Na useme, ‘Hivi ndivyo Babiloni atakavyozama asiinuke tena kamwe kwa sababu ya msiba ambao ninaleta juu yake;+ nao hakika watajichosha.’”+
Maneno ya Yeremia yamefikia hapa.