Yeremia 5:1-31

5  Nendeni huku na huku katika barabara za Yerusalemu na mwone, sasa, na mjue, nanyi mjitafutie katika viwanja vyake vya watu wote ikiwa mnaweza kumpata mwanadamu,+ ikiwa kuna yeyote anayetenda haki,+ yeyote anayetafuta uaminifu,+ nami nitamsamehe.  Hata wakisema: “Kama anavyoishi Yehova!” watakuwa wanaapa kwa uwongo mtupu.+  Ee Yehova, je, macho yako hayaangalii uaminifu?+ Umewapiga,+ lakini hawakuwa wagonjwa.+ Uliwaangamiza.+ Walikataa kukubali nidhamu.+ Walizifanya nyuso zao kuwa ngumu kuliko mwamba.+ Walikataa kurudi.+  Hata kama mimi mwenyewe nikisema: “Hakika wao ni wa tabaka ya chini. Walitenda kwa upumbavu, kwa maana wameipuuza njia ya Yehova, hukumu ya Mungu wao.+  Nitashika njia kwenda kwa wakuu na kusema nao;+ kwa maana wao lazima waliiangalia njia ya Yehova, hukumu ya Mungu wao.+ Hakika wao wote pamoja lazima waliivunja nira; lazima wawe walizikata pingu.”+  Ndiyo sababu simba kutoka msituni amewashambulia, mbwa-mwitu wa nchi tambarare za jangwani anaendelea kuwapora,+ chui anakaa macho kwenye majiji yao.+ Kila mtu anayetoka humo anararuliwa vipande-vipande. Kwa maana makosa yao yamekuwa mengi; matendo yao ya kukosa uaminifu yamekuwa mengi sana.+  Nawezaje kukusamehe kwa ajili ya jambo hili? Wana wako wameniacha, nao wanaendelea kuapa+ kwa kitu ambacho si Mungu.+ Nami niliendelea kuwashibisha,+ lakini wakaendelea kufanya uzinzi,+ nao wanaenda katika nyumba ya mwanamke kahaba wakiwa makundi-makundi.  Wamekuwa farasi walioshikwa na nyege, wenye mapumbu yenye nguvu. Kila mmoja wao analia kwa ajili ya mke wa mwenzake.+  “Je, nisitoze hesabu kwa sababu ya mambo haya?” asema Yehova.+ “Au, je, nafsi yangu isijilipizie kisasi juu ya taifa ambalo liko hivyo?”+ 10  “Njooni juu ya mistari yake ya mizabibu na kuharibu,+ lakini msiangamize kabisa.+ Chukueni machipukizi yake yenye kutoa majani mengi, kwa maana hayo si ya Yehova.+ 11  Kwa maana nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda hakika zimenitendea kwa hila,” asema Yehova.+ 12  “Wamemkana Yehova, nao wanaendelea kusema, ‘Yeye hayuko.+ Na hakuna msiba utakaokuja juu yetu, nasi hatutaona upanga wala njaa.’+ 13  Nao manabii wanakuwa upepo, na lile neno halimo ndani yao.+ Hivyo ndivyo watakavyotendewa.” 14  Kwa hiyo Yehova, Mungu wa majeshi, amesema hivi: “Kwa sababu ninyi mnasema jambo hilo, tazama, nayafanya maneno yangu kinywani mwenu kuwa moto,+ na watu hawa watakuwa kuni, nao hakika utawateketeza.”+ 15  “Tazama, ninaleta juu yenu taifa kutoka mbali,+ enyi nyumba ya Israeli,” asema Yehova. “Ni taifa linalodumu. Ni taifa la zamani za kale,+ taifa ambalo lugha yake hamwijui, nanyi hamwezi kusikia na kuelewa yale wanayosema. 16  Podo lao ni kama kaburi lililo wazi; wote ni wanaume wenye nguvu.+ 17  Hakika wao pia watakula mavuno yako na mkate wako.+ Watu hao watakula wana wako na binti zako. Watakula makundi yako na mifugo yako. Watakula mzabibu wako na mtini wako.+ Watavunja-vunja kwa upanga majiji yako yenye ngome unayoyategemea.” 18  “Na hata katika siku hizo,” asema Yehova, “Sitawaangamiza ninyi.+ 19  Na itakuwa kwamba mtasema, ‘Kwa sababu gani Yehova Mungu wetu ametutendea mambo haya yote?’+ Nawe utawaambia, ‘Kama mlivyoniacha mimi, kwenda kumtumikia mungu wa kigeni katika nchi yenu, ndivyo mtakavyowatumikia wageni katika nchi ambayo si yenu.’”+ 20  Tangazeni jambo hili katika nyumba ya Yakobo, na kulitangaza katika Yuda, mkisema: 21  “Sikieni jambo hili, sasa, enyi watu wasio na hekima ambao hawana moyo wa ufahamu:+ Wana macho, lakini hawawezi kuona;+ wana masikio, lakini hawawezi kusikia.+ 22  ‘Je, hata hamniogopi mimi,’+ asema Yehova, ‘au, je, hata hamna maumivu makali kwa sababu yangu,+ ambaye nimeweka mchanga kuwa mpaka wa bahari, sharti linalodumu mpaka wakati usio na kipimo kwamba haiwezi kuvuka? Ingawa mawimbi yake husukasuka, bado hayawezi kushinda; na ingawa huchafuka, bado hayawezi kuuvuka.+ 23  Lakini hawa watu wamekuwa na moyo mgumu na wenye kuasi; wamegeuka kando nao wanaendelea kutembea katika mwendo wao.+ 24  Lakini hawakusema moyoni mwao: “Sasa, na tumwogope Yehova Mungu wetu,+ Yeye anayenyesha mvua kubwa na mvua ya vuli na mvua ya masika katika majira yake,+ Yeye anayetulindia majuma yaliyoamriwa ya mavuno.”+ 25  Makosa yenu wenyewe yameyafukuzia mbali mambo hayo, na dhambi zenu wenyewe zimewazuilia ninyi mema.+ 26  “‘Kwa maana watu waovu wamepatikana kati ya watu wangu.+ Wanaendelea kukaza macho, kama wakati wawindaji wa ndege wanapochutama.+ Wameweka mtego wenye kuharibu. Wao wanawanasa watu. 27  Kama tundu lilivyojaa viumbe vinavyoruka, ndivyo nyumba zao zilivyojaa udanganyifu.+ Ndiyo sababu wamekuwa wakuu nao wanapata utajiri.+ 28  Wamenenepa;+ wameng’aa. Pia wamejaa kabisa mambo mabaya. Hawakutetea kesi yoyote,+ hata kesi ya mvulana asiye na baba,+ ili wapate mafanikio;+ nao hawakuifuatilia hukumu ya maskini.’” 29  “Je, nisitoze hesabu kwa sababu ya mambo hayo,” asema Yehova, “au, je, nafsi yangu isijilipizie kisasi juu ya taifa ambalo liko hivyo?+ 30  Hali yenye kushangaza, ndiyo, jambo lenye kuchukiza sana, limetokezwa katika nchi:+ 31  Manabii wenyewe kwa kweli wanatoa unabii kwa uwongo;+ nao makuhani wanakandamiza kulingana na nguvu zao.+ Na watu wangu wamependa mambo yawe hivyo;+ nanyi mtafanya nini mwisho wake?”+

Maelezo ya Chini