Yeremia 49:1-39

49  Kuhusu wana wa Amoni,+ Yehova amesema hivi: “Je, Israeli hana wana, au, je, yeye hana mrithi? Kwa nini Malkamu+ amemiliki Gadi,+ na watu wake mwenyewe wamekaa katika majiji ya Israeli?”+  “‘Kwa hiyo, tazama! siku zinakuja,’ asema Yehova, ‘nami nitafanya king’ora cha vita+ kisikiwe juu ya Raba+ la wana wa Amoni; na hakika yeye atakuwa kilima cha mahame yenye ukiwa,+ na miji yake ya kandokando+ itawashwa katika moto.’+ “‘Na Israeli atawamiliki wale wanaommiliki,’+ Yehova amesema.  “‘Piga mayowe,+ Ee Heshboni,+ kwa maana Ai ameporwa! Paazeni kilio, enyi miji ya kandokando ya Raba. Jifungeni nguo za magunia.+ Ombolezeni, na mwende huku na huku kati ya mazizi ya mawe, kwa maana Malkamu ataenda uhamishoni,+ makuhani wake na wakuu wake, wote pamoja.+  Kwa nini unajigamba kuhusu nchi tambarare ya chini,+ nchi yako tambarare ya chini inayotiririka, Ee binti usiye mwaminifu, wewe unayezitegemea hazina zako,+ ukisema: “Ni nani atakayenijia?”’”+  “‘Tazama, ninaleta juu yako jambo lenye kutia hofu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu,+ Yehova wa majeshi, ‘kutoka kwa wale wote wanaokuzunguka pande zote. Na hakika ninyi mtatawanywa, kila mmoja upande wake mwenyewe,+ na hapatakuwa na yeyote anayewakusanya pamoja wale wanaokimbia.’”  “‘Lakini baadaye nitawakusanya mateka wa wana wa Amoni,’+ asema Yehova.”  Kuhusu Edomu, Yehova wa majeshi amesema hivi: “Je, hakuna tena hekima+ yoyote katika Temani?+ Je, shauri limeangamia kutoka kwa wale walio na uelewaji? Je, hekima yao imeoza?+  Kimbieni!+ Geukeni mkimbie! Shukeni ndani sana ili mkae,+ enyi wakaaji wa Dedani!+ Kwa maana yale maafa ya Edomu nitayaleta juu yake, wakati ambao nitakaza fikira zangu juu yake.+  Ikiwa wakusanya-zabibu wangeingia kwako, je, hawangeacha masalio fulani? Ikiwa wezi wangekuja wakati wa usiku, hakika wangefanya uharibifu kiasi kile tu ambacho wangetosheka nacho.+ 10  Lakini mimi, nitamvua Esau awe uchi.+ Nitafunua mahali pake pa maficho,+ na mtu hataweza kujificha.+ Hakika uzao wake na ndugu zake na jirani zake wataporwa,+ naye hatakuwapo.+ 11  Waache wavulana wako wasio na baba.+ Mimi mwenyewe nitawahifadhi hai, na wajane wako watanitegemea mimi.”+ 12  Kwa maana Yehova amesema hivi: “Tazama! Ingawa si desturi yao kukinywa kikombe, bila shaka watakinywa.+ Na wewe mwenyewe, je, utaachwa kabisa bila kuadhibiwa? Hutaachwa bila kuadhibiwa, kwa maana utakunywa bila shaka.”+ 13  “Kwa maana nimeapa kwa nafsi yangu mwenyewe,”+ asema Yehova, “kwamba Bosra+ litakuwa kitu cha kushangaza,+ shutuma, uharibifu na laana tupu; na majiji yake yote yatakuwa mahali palipoharibiwa mpaka wakati usio na kipimo.”+ 14  Kuna habari ambayo nimesikia kutoka kwa Yehova, na kuna mjumbe ambaye ametumwa kati ya mataifa, kusema: “Jikusanyeni pamoja, mje juu yake, na msimame kupigana.”+ 15  “Kwa maana, tazama! Nimekufanya mdogo kwelikweli kati ya mataifa, umedharauliwa kati ya wanadamu.+ 16  Mtetemeko ambao ulisababisha umekudanganya, kimbelembele cha moyo wako,+ ewe unayekaa katika makimbilio ya mwamba, ukishika kilele cha kilima. Ingawa unajenga kiota chako juu kama tai,+ nitakushusha chini kutoka hapo,”+ asema Yehova. 17  “Na Edomu atakuwa kitu cha kushangaza.+ Kila mtu anayepita kando yake atatazama kwa mshangao na kupiga mluzi kwa sababu ya mapigo yake yote.+ 18  Kama ilivyotokea katika maangamizi ya Sodoma na Gomora na miji yake jirani,”+ Yehova amesema, “vivyo hivyo hakuna mtu atakayekaa hapo, na hakuna mwana wa binadamu atakayekaa ndani yake akiwa mgeni.+ 19  “Tazama! Mtu atapanda tu kama simba+ kutoka katika vichaka vyenye fahari kando ya Yordani kwenda kwenye makao yanayodumu,+ lakini katika muda mfupi nitamfanya akimbie kutoka kwake.+ Nami nitaweka juu yake yule ambaye amechaguliwa. Kwa maana ni nani aliye kama mimi,+ na ni nani atakayenipinga,+ na ni nani, sasa, aliye mchungaji anayeweza kusimama mbele zangu?+ 20  Kwa hiyo sikieni shauri la Yehova ambalo ametunga juu ya Edomu,+ na mawazo yake ambayo amefikiri juu ya wakaaji wa Temani:+ Hakika wadogo wa kundi watakokotwa huku na huku. Hakika kwa sababu yao atayafanya makao yao kuwa ukiwa.+ 21  Dunia imeanza kutetemeka kutokana na sauti ya kuanguka kwao.+ Kuna kilio!+ Sauti yake imesikiwa hata kwenye Bahari Nyekundu.+ 22  Tazama! Mtu atapaa na kurukia mawindo kama tai,+ naye atanyoosha mabawa yake juu ya Bosra;+ na moyo wa wanaume wenye nguvu wa Edomu siku hiyo utakuwa kama moyo wa mke aliye na taabu ya kuzaa mtoto.”+ 23  Kuhusu Damasko:+ “Hamathi+ na Arpadi+ wameona aibu, kwa maana wamesikia habari mbaya. Wamebomoka.+ Katika bahari kuna hangaiko; haiwezi kukaa bila machafuko.+ 24  Damasko amekufa moyo. Amegeuka ili kukimbia, na wasiwasi mtupu umemshika.+ Taabu na uchungu wa kuzaa zimemshika, kama mwanamke anayezaa.+ 25  Kwa nini jiji lenye sifa halikuachwa, mji wa furaha? + 26  “Kwa hiyo vijana wake wataanguka katika viwanja vyake vya watu wote, na wanaume wote wa vita watanyamazishwa katika siku hiyo,”+ asema Yehova wa majeshi. 27  “Nami nitawasha moto juu ya ukuta wa Damasko, nao utaiteketeza minara ya makao ya Ben-hadadi.”+ 28  Kuhusu Kedari+ na falme za Hasori,+ ambazo Nebukadreza mfalme wa Babiloni alipiga,+ Yehova amesema hivi: “Simameni, nendeni mpaka Kedari, na muwapore wana wa Mashariki.+ 29  Mahema+ yao na makundi+ yao yatachukuliwa, vitambaa vyao vya mahema+ na vyombo vyao vyote. Na ngamia+ zao watachukuliwa kutoka kwao. Na hakika wao watawalilia, ‘Kuna hofu pande zote!’”+ 30  “Kimbieni, kimbilieni mbali; shukeni ndani sana ili mkae, enyi wakaaji wa Hasori,”+ asema Yehova. “Kwa maana Nebukadreza mfalme wa Babiloni+ ametunga shauri juu yenu naye amefikiri wazo fulani juu yenu.” 31  “Simameni, pandeni juu ya taifa ambalo linastarehe,+ linalokaa katika usalama!”+ asema Yehova. “Halina milango wala mapingo. Wanakaa peke yao.+ 32  Na ngamia+ zao wataporwa, na makundi yao yaliyo mengi yatakuwa nyara. Nami nitawatawanya kwa kila upepo,+ wale ambao nywele zao zimekatwa kwenye vipaji vya nyuso;+ nami nitaleta maafa yao kutoka katika maeneo yote karibu nalo,” asema Yehova. 33  “Na Hasori+ atakuwa pango la mbwa-mwitu,+ mahame yenye ukiwa mpaka wakati usio na kipimo. Hakuna mtu atakayekaa humo, na hakuna mwana wa binadamu atakayekaa humo akiwa mgeni.”+ 34  Hili ndilo neno la Yehova lililomjia Yeremia nabii kuhusu Elamu+ mwanzoni mwa ufalme wa Sedekia+ mfalme wa Yuda, kusema: 35  “Yehova wa majeshi amesema hivi, ‘Tazama, ninauvunja upinde wa Elamu,+ mwanzo wa nguvu zao. 36  Nami nitaleta juu ya Elamu zile pepo nne kutoka katika miisho minne ya mbingu.+ Nami nitawatawanya kwenye pepo hizi zote,+ na hakutakuwa na taifa lolote ambako watu wa Elamu waliotawanywa+ hawatakuja ndani yake.’” 37  “Nami nitawavunja-vunja Waelamu mbele ya adui zao na mbele ya wale wanaoitafuta nafsi yao; nami nitaleta juu yao msiba, hasira yangu inayowaka,”+ asema Yehova. “Nami nitatuma upanga nyuma yao mpaka nitakapokuwa nimewaangamiza.”+ 38  “Nami nitaweka kiti changu cha ufalme katika Elamu,+ nitaangamiza kutoka humo mfalme na wakuu,” asema Yehova. 39  “Na hakika itakuwa kwamba katika siku za mwisho+ nitawakusanya mateka wa Elamu,”+ asema Yehova.

Maelezo ya Chini