Yeremia 48:1-47

48  Kuhusu Moabu,+ Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi:+ “Ole wake Nebo,+ kwa maana ameporwa! Kiriathaimu+ ameona aibu, ametekwa. Kilele kilicho salama kimeona aibu na kutiwa hofu.+  Moabu+ haina sifa yoyote tena. Katika Heshboni+ wamefikiria msiba juu yake: ‘Njooni, tumkatilie mbali asiwe taifa.’+ “Wewe pia, Ee Madmeni, unapaswa kunyamaza kimya. Upanga unatembea nyuma yako.  Kuna sauti ya kilio kutoka Horonaimu,+ uporaji na mvunjiko mkubwa.  Moabu amevunjwa.+ Watoto wake wamefanya kilio kisikiwe.  Kwa maana katika njia ya kwenda mpaka Luhithi+ mtu anapanda akilia—kuna kilio. Kwa maana katika njia ya kushuka kutoka Horonaimu kuna kilio chenye kutaabisha juu ya ule mvunjiko+ ambao watu wamesikia.  “Kimbieni; ponyeni nafsi zenu,+ nanyi mnapaswa kuwa kama mberoshi nyikani.+  Kwa sababu tegemeo lako liko katika kazi zako na katika hazina zako, wewe pia utatekwa.+ Na hakika Kemoshi+ ataenda uhamishoni,+ makuhani wake na wakuu wake wakati uleule.+  Na mporaji atakuja juu ya kila jiji,+ na hakutakuwa na jiji lolote linaloweza kuponyoka.+ Na nchi tambarare ya chini hakika itaangamia na nchi tambarare itaharibiwa, jambo ambalo Yehova amesema.  “Mpeni Moabu alama ya barabara, kwa maana ataenda wakati wa mabomoko;+ na majiji yake yatakuwa kitu tu cha kushangaza, bila kuwa na mtu anayekaa humo.+ 10  “Alaaniwe yule mtu anayetimiza utume wa Yehova kwa uzembe;+ na alaaniwe yule mtu anayeuzuilia upanga wake usimwage damu! 11  “Wamoabu wamekuwa wakistarehe tangu ujana wao,+ nao wanaendelea bila usumbufu juu ya machicha+ yao. Nao hawajamiminwa kutoka chombo kimoja ndani ya chombo kingine, nao hawajaenda uhamishoni. Ndiyo sababu ladha yao imesimama tuli ndani yao, na harufu yao haijabadilika. 12  “‘Kwa hiyo, tazama! siku zinakuja,’ asema Yehova, ‘nami nitatuma kwao watu wanaoinamisha chombo, nao hakika watawainamisha;+ nao watamwaga kilicho ndani ya vyombo vyao, na mitungi yao mikubwa wataivunja vipande-vipande. 13  Na Wamoabu wataona aibu kwa sababu ya Kemoshi,+ kama wale wa nyumba ya Israeli walivyoona aibu kwa sababu ya Betheli, uhakika wao.+ 14  Kwa nini mna ujasiri wa kusema: “Sisi ni wanaume wenye uwezo na wanaume wenye nguvu+ kwa ajili ya vita”?’ 15  “‘Moabu ameporwa, na mtu amepanda juu ya majiji yake.+ Na vijana wao walio bora zaidi wameshuka kwenda kuuawa,’+ asema Mfalme, ambaye jina lake ni Yehova wa majeshi.+ 16  “Maafa juu ya Wamoabu yako karibu kuja, na msiba wao unaharakisha sana.+ 17  Wale wote wanaowazunguka pande zote watawasikitikia, wale wote wanaolijua jina lao.+ Ninyi semeni, ‘Jinsi fimbo ya nguvu imevunjwa, fimbo ya urembo!’+ 18  “Shuka chini kutoka katika utukufu, na kuketi katika kiu, Ee mwanamke mkaaji, binti+ ya Diboni;+ kwa maana mporaji wa Moabu amekuja juu yako. Kwa kweli yeye atapaharibu mahali pako penye ngome.+ 19  “Simama tuli na kuiangalia njia, Ee mwanamke mkaaji wa Aroeri.+ Muulize yeye anayekimbia na yeye anayeponyoka. Sema, ‘Kumetokea nini?’+ 20  Moabu ameona aibu, kwa maana ameingiwa na hofu.+ Piga mayowe na kupaaza kilio. Tangazeni katika Arnoni+ kwamba Moabu ameporwa. 21  Na hukumu imekuja katika nchi iliyo tambarare,+ katika Holoni na katika Yahazi+ na juu ya Mefaathi,+ 22  na juu ya Diboni+ na juu ya Nebo+ na juu ya Beth-diblathaimu, 23  na juu ya Kiriathaimu+ na juu ya Beth-gamuli na juu ya Beth-meoni+ 24  na juu ya Keriothi+ na juu ya Bosra+ na juu ya majiji yote ya nchi ya Moabu, yale yaliyo mbali na yale yaliyo karibu. 25  “‘Pembe ya Moabu imekatwa,+ na mkono wake umevunjwa,’+ asema Yehova. 26  ‘Mlewesheni,+ kwa maana ameonyesha majivuno sana juu ya Yehova mwenyewe;+ na Moabu amegaagaa katika matapiko+ yake, naye amekuwa kitu cha kudhihakiwa, yeye mwenyewe. 27  “‘Na je, kwako Israeli hakuwa tu kitu cha kudhihakiwa?+ Au, je, alipatikana kati ya wezi wa waziwazi?+ Kwa maana ulikuwa ukijitikisa kichwa kila mara uliposema juu yake. 28  “‘Yaacheni majiji, mkae juu ya mwamba,+ ninyi wakaaji wa Moabu, na muwe kama njiwa ambaye hujenga kiota chake katika maeneo ya kinywa cha shimo.’”+ 29  “Tumesikia habari za kiburi cha Moabu+—ana majivuno sana—habari za ustahiki wake na za kiburi chake na za majivuno yake na za kuinuka kwa moyo wake.”+ 30  “‘Mimi mwenyewe nimeijua ghadhabu yake,’ asema Yehova, ‘na hivyo sivyo itakavyokuwa; maneno yake matupu+—kwa kweli hawatafanya kwa njia hiyo.+ 31  Ndiyo sababu nitapiga mayowe juu ya Moabu, nami nitapaaza kilio+ kwa ajili ya Moabu yote. Mtu atawaombolezea watu wa Kir-heresi.+ 32  “‘Nitakulilia kwa kilio kinachoshinda kile kilio kwa ajili ya Yazeri,+ Ee mzabibu wa Sibma.+ Machipukizi yako yenye matawi mengi yameivuka bahari. Mpaka baharini—mpaka Yazeri+—yamefika. Mporaji ameanguka+ juu ya matunda yako ya wakati wa kiangazi na juu ya ukusanyaji wako wa zabibu.+ 33  Na kushangilia na shangwe zimeondolewa katika shamba la matunda na katika nchi ya Moabu.+ Nami nimeikomesha divai kutoka katika mashinikizo ya divai.+ Hakuna yeyote atakayezikanyaga kwa kupaaza sauti. Huko kupaaza sauti hakutakuwa kupaaza sauti.’”+ 34  “‘Kutoka kwenye kilio katika Heshboni+ mpaka Eleale,+ mpaka Yahazi+ wamepaaza sauti yao,+ kutoka Soari+ mpaka Horonaimu,+ mpaka Eglath-shelishiya;+ kwa maana hata maji ya Nimrimu+ yatakuwa ukiwa mtupu. 35  Nami nitamkomesha katika Moabu,’ asema Yehova, ‘mtu anayeleta toleo mahali pa juu na mtu anayemfukizia mungu wake moshi wa dhabihu.+ 36  Ndiyo sababu moyo wangu mwenyewe utapiga-piga kwa ajili ya Moabu, kama tu filimbi;+ na kwa ajili ya watu wa Kir-heresi+ moyo wangu utapiga-piga, kama filimbi. Ndiyo sababu wingi ambao ametokeza hakika utaangamia.+ 37  Kwa maana kuna upara+ juu ya vichwa vyote, na ndevu zote zimekatwa.+ Kuna mikato+ juu ya mikono yote, na juu ya viuno kuna nguo za magunia!’”+ 38  “‘Juu ya paa zote za Moabu na katika viwanja vyake vya watu wote—vyote—kuna maombolezo;+ kwa maana nimemvunja Moabu kama tu chombo ambacho hakipendezi,’+ asema Yehova. 39  ‘Jinsi ameingiwa na hofu! Pigeni mayowe! Jinsi Moabu ameugeuza mgongo! Ameona aibu.+ Na Moabu amekuwa kitu cha kudhihakiwa na kitu chenye kuogopesha kwa wale wote wanaomzunguka pande zote.’” 40  “Kwa maana Yehova amesema hivi, ‘Tazama! Kama tai anayerukia mawindo,+ ndivyo mtu atakavyonyoosha mabawa yake juu ya Moabu.+ 41  Kwa kweli miji itatekwa, na mahali pake palipo imara hakika patakamatwa. Na moyo wa wanaume wenye nguvu wa Moabu lazima siku hiyo utakuwa kama moyo wa mke ambaye ana taabu ya kuzaa mtoto.’”+ 42  “‘Na hakika Moabu ataangamizwa asiwe kikundi cha watu,+ kwa maana ameonyesha majivuno+ sana juu ya Yehova. 43  Hofu na shimo na mtego ziko juu yako, Ee mkaaji wa Moabu,’+ asema Yehova. 44  ‘Yeyote anayekimbia kwa sababu ya hofu ataanguka ndani ya shimo; na yeyote anayetoka ndani ya shimo atakamatwa katika mtego.’+ “‘Kwa maana nitaleta juu yake, juu ya Moabu, mwaka wa kuwakazia fikira,’+ asema Yehova. 45  ‘Katika kivuli cha Heshboni wale wanaokimbia wamesimama tuli bila nguvu. Kwa maana hakika moto utatoka katika Heshboni,+ na mwali wa moto kutoka katikati ya Sihoni;+ nao utateketeza vipaji vya nyuso za Moabu na utosi wa kichwa cha wana wa ghasia.’+ 46  “‘Ole wako, Ee Moabu!+ Watu wa Kemoshi+ wameangamia. Kwa maana wana wako wamechukuliwa mateka na binti zako wakawa mateka. 47  Nami nitawakusanya mateka wa Moabu siku za mwisho,’+ asema Yehova. ‘Hukumu juu ya Moabu imefikia hapa.’”+

Maelezo ya Chini