Yeremia 46:1-28

46  Hili ndilo neno la Yehova lililomjia Yeremia nabii kuhusu mataifa:+  Kwa ajili ya Misri,+ kuhusu jeshi la Farao Neko mfalme wa Misri,+ aliyekuwa kando ya mto Efrati kule Karkemishi,+ ambaye Nebukadreza mfalme wa Babiloni alimshinda katika mwaka wa nne wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda:  “Pangeni ngao ndogo na ngao kubwa, na mkaribie ili kupigana.+  Fungeni farasi lijamu, na mpande, enyi wapanda-farasi, na msimame na kofia. Sugueni mikuki. Vaeni mavazi ya chuma.+  “‘Kwa nini nimewaona wakiwa wameingiwa na hofu? Wanarudi nyuma, na wanaume wao wenye nguvu wamevunjwa vipande-vipande; nao hakika wamekimbia, wala hawakugeuka.+ Kuna hofu pande zote,’+ asema Yehova.  ‘Mtu mwepesi asijaribu kukimbia, na mwanamume mwenye nguvu asijaribu kuponyoka.+ Juu kaskazini+ kando ya ukingo wa mto Efrati wamejikwaa na kuanguka.’+  “Ni nani huyu anayepanda juu kama Mto Nile, kama mito ambayo maji yake yanajirusha?+  Misri inakuja kama Mto Nile,+ na kama mito maji yanajirusha.+ Nayo inasema, ‘Nitapanda. Nitaifunika dunia. Nitaliangamiza kwa urahisi jiji na wale wanaokaa ndani yake.’+  Pandeni, enyi farasi; na kwenda kiwazimu, enyi magari! Wanaume wenye nguvu na waende, Kushi+ na Putu,+ wanaochukua ngao, na Ludimu,+ wanaoshika na kukanyaga upinde. 10  “Na siku ile ni ya Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi, siku yake ya kisasi ya kujilipizia kisasi juu ya adui zake.+ Na hakika upanga utakula na kushiba na kujijaza damu yao, kwa maana Bwana Mwenye Enzi Kuu,+ Yehova wa majeshi, ana dhabihu+ katika nchi ya kaskazini kando ya mto Efrati.+ 11  “Panda mpaka Gileadi uchukue zeri,+ Ee bikira, binti ya Misri.+ Umezidisha njia za kuponya bure tu. Hakuna matibabu kwa ajili yako.+ 12  Mataifa yamesikia aibu+ yako na kilio chako kimeijaza nchi.+ Kwa maana wamejikwaa, mwanamume mwenye nguvu juu ya mwanamume mwenye nguvu.+ Wameanguka chini pamoja, wote wawili.” 13  Neno ambalo Yehova alimwambia Yeremia nabii kuhusu kuja kwa Nebukadreza mfalme wa Babiloni ili kuipiga nchi ya Misri:+ 14  “Lihubiri jambo hilo katika Misri, na mlitangaze kule Migdoli,+ na mlitangaze kule Nofu+ na Tahpanhesi.+ Semeni, ‘Simama, pia ujifanyie matayarisho,+ kwa maana hakika upanga utakula kukuzunguka pande zote.+ 15  Kwa nini watu wako wenye nguvu wamefagiliwa mbali?+ Hawakusimama, kwa maana Yehova mwenyewe amewasukumia mbali.+ 16  Hesabu kubwa wanajikwaa. Kwa kweli pia wanaanguka. Nao wanaendelea kuambiana: “Simameni, na acheni sisi turudi kwa watu wetu na kwa nchi ya jamaa zetu kwa sababu ya upanga unaoonea.”’ 17  Huko wametangaza, ‘Farao mfalme wa Misri ni kelele tupu.+ Ameachilia wakati wa sherehe upite.’+ 18  “‘Kama ninavyoishi,’ asema Mfalme, ambaye jina lake ni Yehova wa majeshi,+ ‘kama Tabori+ kati ya milima na kama Karmeli+ kando ya bahari yeye ataingia. 19  Jifanyie mzigo kwa ajili ya uhamisho,+ Ee mwanamke mkaaji, binti+ ya Misri. Kwa maana Nofu+ litakuwa kitu cha kushangaza na kwa kweli litawashwa moto, hivi kwamba lisiwe na mkaaji.+ 20  Misri ni ndama-jike mrembo sana. Kutoka upande wa kaskazini hakika mbu atakuja juu yake.+ 21  Na zaidi, askari-jeshi wake waliokodiwa walio katikati yake ni kama ndama waliononeshwa.+ Lakini wao pia wamerudi nyuma;+ wamekimbia pamoja. Hawakusimama.+ Kwa maana ile siku ya msiba wao imekuja juu yao, wakati wa kuwakazia fikira.’+ 22  “‘Sauti yake ni kama ile ya nyoka ambaye anaenda;+ kwa maana watu wataenda wakiwa na nguvu, nao wataingia kwake wakiwa na mashoka, kama wale wanaokusanya kuni. 23  Hakika wataukata msitu wake,’+ asema Yehova, ‘kwa maana haukuweza kupenywa. Kwa maana wamekuwa wengi sana kuliko nzige,+ nao hawana hesabu. 24  Hakika binti+ ya Misri ataona aibu. Kwa kweli atatiwa mkononi mwa watu wa kaskazini.’+ 25  “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema, ‘Tazama, ninakaza fikira zangu juu ya Amoni+ kutoka No+ na juu ya Farao na juu ya Misri na juu ya miungu+ yake na juu ya wafalme+ wake, juu ya Farao na juu ya wale wote wanaomtegemea.’+ 26  “‘Nami nitawatia mkononi mwa wale wanaoitafuta nafsi yao na mkononi mwa Nebukadreza mfalme wa Babiloni+ na mkononi mwa watumishi wake; na baadaye watu watakaa ndani yake kama katika siku za zamani za kale,’+ asema Yehova. 27  “‘Nawe usiogope, Ee mtumishi wangu Yakobo, wala usiingiwe na hofu, Ee Israeli.+ Kwa maana, tazama, ninakuokoa kutoka mbali na uzao wako kutoka katika nchi yako ya utekwani.+ Na hakika Yakobo atarudi, hatakuwa na usumbufu naye atastarehe na kusiwe na yeyote wa kumtetemesha.+ 28  Nawe usiogope, Ee mtumishi wangu Yakobo,’ asema Yehova, ‘kwa maana mimi niko pamoja nawe.+ Kwa maana nitafanya maangamizi kati ya mataifa yote ambako nimekutawanya huko,+ lakini wewe sitakuangamiza.+ Hata hivyo, nitakutia adabu kwa kiwango kinachofaa,+ nami sitakuacha kamwe bila kukuadhibu.’”+

Maelezo ya Chini