Yeremia 45:1-5
45 Neno ambalo Yeremia nabii alimwambia Baruku+ mwana wa Neria alipoandika katika kitabu maneno haya kutoka kinywani mwa Yeremia+ katika mwaka wa nne wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, akisema:
2 “Yehova Mungu wa Israeli amesema hivi kukuhusu wewe, Ee Baruku,
3 ‘Umesema: “Ole wangu,+ sasa, kwa maana Yehova ameongeza huzuni juu ya maumivu yangu! Nimechoka kwa sababu ya kuugua kwangu, nami sikupata mahali pa kupumzika.”’+
4 “Wewe mwambie hivi, ‘Yehova amesema hivi: “Tazama! Kile ambacho nimekijenga ninakibomoa, na kile ambacho nimekipanda ninaking’oa, ndiyo, nchi yote.+
5 Na wewe unaendelea kujitafutia makuu.+ Usiendelee kuyatafuta.”’+
“‘Kwa maana, tazama, ninaleta msiba juu ya wote wenye mwili,’+ asema Yehova, ‘nami nitakupa wewe nafsi yako kuwa nyara katika mahali pote utakapoenda.’”+