Yeremia 44:1-30

44  Neno lililomjia Yeremia kwa ajili ya Wayahudi wote waliokuwa wakikaa katika nchi ya Misri,+ wale waliokuwa wakikaa kule Migdoli+ na Tahpanhesi+ na Nofu+ na katika nchi ya Pathrosi,+ likisema:  “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Ninyi wenyewe mmeona msiba wote ambao nimeleta juu ya Yerusalemu+ na juu ya majiji yote ya Yuda, na, tazama, hayo leo ni mahali palipoharibiwa, na ndani yake hamna mkaaji.+  Ni kwa sababu ya ubaya wao ambao walifanya ili kunitia uchungu kwa kwenda kufukiza moshi wa dhabihu+ na kutoa utumishi kwa miungu mingine ambayo wao hawakuijua, wala ninyi wala mababu zenu.+  Nami niliendelea kuwatuma kwenu watumishi wangu wote manabii, nikiamka mapema na kuwatuma,+ nikisema: “Tafadhali, msifanye chukizo la aina hii ambalo nimelichukia.”+  Lakini hawakusikiliza,+ wala hawakutega sikio lao ili kurudi kutoka katika ubaya wao kwa kutoifukizia miungu mingine moshi wa dhabihu.+  Kwa hiyo ghadhabu yangu, na hasira yangu, ilimwagwa nayo ikateketeza katika majiji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu;+ nazo zikawa mahali palipoharibiwa, mahame yenye ukiwa, kama ilivyo leo hii.’+  “Na sasa Yehova, Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Kwa nini mnaleta msiba mkubwa juu ya nafsi+ zenu, ili mumkatilie mbali kutoka kwenu mwanamume na mwanamke, mtoto mdogo na yule anayenyonya,+ kutoka katikati ya Yuda, hivi kwamba hamjiachii mabaki;  kwa kunitia uchungu mimi kwa kazi za mikono yenu kwa kuifukizia miungu mingine moshi wa dhabihu+ katika nchi ya Misri, ambako mnaingia ili kukaa mkiwa wageni; kwa kusudi la kusababisha kukatiliwa mbali kwenu na kwa kusudi la ninyi kuwa laana na shutuma kati ya mataifa yote ya dunia?+  Je, mmeyasahau matendo mabaya ya mababu+ zenu na matendo mabaya ya wafalme wa Yuda+ na matendo mabaya ya wake zao+ na matendo mabaya yenu wenyewe na matendo mabaya ya wake zenu,+ ambayo wametenda katika nchi ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu? 10  Na mpaka leo hii hawakuona kuwa wamepondwa,+ wala hawakuogopa,+ wala hawakutembea katika sheria+ yangu na katika kanuni zangu ambazo niliweka mbele yenu na mbele ya mababu zenu.’+ 11  “Kwa hiyo Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Tazama, ninakaza uso wangu juu yenu kwa ajili ya msiba na kwa ajili ya kukatilia mbali Yuda yote.+ 12  Nami nitachukua mabaki wa Yuda ambao walikaza nyuso zao ili kuingia katika nchi ya Misri wakae humo wakiwa wageni,+ na hakika wote watamalizika katika nchi ya Misri.+ Wataanguka kwa upanga; nao watamalizika kwa njaa,+ kuanzia aliye mdogo zaidi mpaka aliye mkubwa zaidi; watakufa kwa upanga na kwa njaa. Nao watakuwa laana, kitu cha kushangaza na tukano na shutuma.+ 13  Nami nitatoza hesabu juu ya wale wanaokaa katika nchi ya Misri, kama nilivyotoza hesabu juu ya Yerusalemu, kwa upanga, kwa njaa na kwa tauni.+ 14  Na hakutakuwa na yeyote mwenye kuponyoka wala mwenye kuokoka kwa mabaki wa Yuda wanaoingia ili kukaa humo wakiwa wageni, katika nchi ya Misri,+ wa kurudi katika nchi ya Yuda ambayo wanaitamani kwa nafsi yao ili warudi kukaa humo;+ kwa maana hawatarudi, ila tu watu fulani walioponyoka.’” 15  Na wanaume wote waliojua kwamba wake zao walikuwa wakiifukizia miungu mingine moshi wa dhabihu,+ na wake wote waliokuwa wanasimama wakiwa kutaniko kubwa, na watu wote waliokuwa wakikaa katika nchi ya Misri,+ katika Pathrosi,+ wakamjibu Yeremia, wakisema: 16  “Kuhusu lile neno ambalo umetuambia katika jina la Yehova, sisi hatutakusikiliza;+ 17  lakini hakika tutafanya kila neno ambalo limetoka katika kinywa chetu,+ ili kumfukizia ‘malkia wa mbingu’+ moshi wa dhabihu na kummiminia matoleo ya kinywaji,+ kama sisi wenyewe+ na mababu+ zetu, wafalme+ wetu na wakuu wetu tulivyofanya katika majiji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu, wakati tuliposhiba mkate na kuwa na hali njema, nasi hatukuona msiba wowote kamwe.+ 18  Na tangu tulipoacha kumfukizia ‘malkia wa mbingu’+ moshi wa dhabihu na kummiminia matoleo ya kinywaji tumekosa kila kitu, nasi tumemalizika kwa upanga na kwa njaa.+ 19  “Pia, wakati tulipokuwa tukimfukizia ‘malkia wa mbingu’+ moshi wa dhabihu nasi tukawa na mwelekeo wa kummiminia matoleo ya kinywaji,+ je, tulimtolea keki za dhabihu bila kuwauliza waume zetu, ili kutengeneza sanamu yake, na kummiminia matoleo ya kinywaji?”+ 20  Naye Yeremia akawaambia watu wote, wanaume na wake na watu wote, waliokuwa wakimjibu neno, akisema: 21  “Kuhusu ule moshi wa dhabihu ambao mlifukiza katika majiji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu,+ ninyi+ na mababu+ zenu, wafalme+ wenu na wakuu+ wenu na watu wa nchi, je, Yehova hakukumbuka mambo hayo nayo yakaingia moyoni mwake?+ 22  Mwishowe Yehova hakuweza kuvumilia kwa sababu ya ubaya wa matendo yenu, kwa sababu ya machukizo ambayo mlikuwa mmefanya,+ na hivyo nchi yenu ikawa mahali palipoharibiwa na kitu cha kushangaza na laana, bila mkaaji, kama ilivyo leo hii.+ 23  Kwa sababu mlifukiza moshi wa dhabihu,+ mkamtendea dhambi Yehova,+ hamkuitii sauti ya Yehova+ nanyi hamkutembea katika sheria yake+ na katika kanuni zake na katika vikumbusho vyake, ndiyo sababu msiba huu umewapata ninyi kama ilivyo leo hii.”+ 24  Na Yeremia akaendelea kuwaambia watu wote na wanawake wote: “Sikieni neno la Yehova, Yuda wote mlio katika nchi ya Misri.+ 25  Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Kuhusu ninyi wanaume na wake zenu,+ ninyi wanawake pia mnasema kwa vinywa vyenu, (na kwa mikono yenu mmetimiza,) mkisema: “Bila shaka tutatimiza nadhiri zetu ambazo tumeweka,+ ili kumfukizia ‘malkia wa mbingu’+ moshi wa dhabihu na kummiminia matoleo ya kinywaji.”+ Ninyi wanawake bila shaka mtazitimiza nadhiri zenu, nanyi bila shaka mtazifanya nadhiri zenu.’ 26  “Kwa hiyo sikieni neno la Yehova, Yuda wote mnaokaa katika nchi ya Misri,+ ‘ “Tazama, mimi mwenyewe nimeapa kwa jina langu kuu,”+ Yehova amesema, “kwamba jina langu halitakuwa tena kitu cha kuitwa kwa kinywa cha mtu yeyote wa Yuda,+ akisema, ‘Kama anavyoishi Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova!’+ katika nchi yote ya Misri. 27  Tazama, ninakaa macho kuwaelekea wao kwa ajili ya msiba wala si kwa ajili ya mema;+ na watu wote wa Yuda walio katika nchi ya Misri hakika watamalizika kwa upanga na kwa njaa, mpaka watakapokoma kuwapo.+ 28  Nao wale wanaookoka upanga, watarudi kutoka katika nchi ya Misri kwenda katika nchi ya Yuda, hesabu yao wakiwa ni wachache;+ na wale wote wa mabaki ya Yuda, wanaoingia katika nchi ya Misri kukaa humo wakiwa wageni, watajua hakika ni neno la nani linalotimia, lile linalotoka kwangu au lile linalotoka kwao.”’”+ 29  “‘Na hii ndiyo ishara kwenu,’+ asema Yehova, ‘kwamba ninakaza fikira zangu juu yenu katika mahali hapa, ili mpate kujua kwamba maneno yangu bila shaka yatatimia juu yenu kwa ajili ya msiba:+ 30  Yehova amesema hivi: “Tazama, ninamtia Farao Hofra mfalme wa Misri,+ mkononi mwa adui zake na mkononi mwa wale wanaoitafuta nafsi yake,+ kama nilivyomtia Sedekia mfalme wa Yuda mkononi mwa Nebukadreza mfalme wa Babiloni, adui yake na yeye anayeitafuta nafsi yake.”’”+

Maelezo ya Chini