Yeremia 43:1-13
43 Basi ikawa kwamba mara tu Yeremia alipomaliza kuwaambia watu wote maneno yote ya Yehova Mungu wao ambayo Yehova Mungu wao alikuwa amemtuma nayo kwao, maneno hayo yote,+
2 Azaria mwana wa Hoshaya+ na Yohanani+ mwana wa Karea na watu wote wenye kimbelembele+ wakamwambia Yeremia: “Ni uwongo ambao wewe unasema.+ Yehova Mungu wetu hakukutuma, kusema, ‘Msiingie Misri kukaa humo mkiwa wageni.’+
3 Bali Baruku+ mwana wa Neria anakuchochea juu yetu ili kututia mkononi mwa Wakaldayo, ili watuue au watupeleke uhamishoni Babiloni.”+
4 Na Yohanani mwana wa Karea na wakuu wote wa majeshi na watu wote hawakuitii sauti ya Yehova,+ ili waendelee kukaa katika nchi ya Yuda.+
5 Basi Yohanani mwana wa Karea na wakuu wote wa majeshi wakachukua mabaki wote wa Yuda waliokuwa wamerudi kutoka katika mataifa yote ambako walikuwa wametawanywa, ili kukaa kwa muda katika nchi ya Yuda,+
6 wanaume na wake na watoto wadogo na binti za mfalme+ na kila nafsi ambayo Nebuzaradani+ mkuu wa walinzi alikuwa ameacha wakae pamoja na Gedalia+ mwana wa Ahikamu+ mwana wa Shafani,+ na Yeremia nabii na Baruku+ mwana wa Neria.
7 Na mwishowe wakaingia katika nchi ya Misri,+ kwa maana hawakuitii sauti ya Yehova; nao mwishowe wakafika mpaka Tahpanhesi.+
8 Ndipo neno la Yehova likamjia Yeremia katika Tahpanhesi, na kusema:
9 “Chukua mkononi mwako mawe makubwa, uyafiche katika saruji kwenye ngazi ya matofali iliyo kwenye mlango wa nyumba ya Farao katika Tahpanhesi mbele ya macho ya wanaume Wayahudi.+
10 Nawe uwaambie, ‘Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi: “Tazama, ninatuma watu na kumchukua Nebukadreza mfalme wa Babiloni,+ mtumishi wangu,+ nami nitakiweka kiti chake cha ufalme juu ya mawe haya ambayo nimeyaficha, na hakika yeye atanyoosha hema lake la fahari juu yake.
11 Naye ataingia na kuipiga nchi ya Misri.+ Yeyote aliyekusudiwa mapigo yenye kufisha atapigwa kwa mapigo yenye kufisha, na yeyote aliyekusudiwa kwenda utekwani ataenda utekwani, na yeyote aliyekusudiwa upanga atapigwa kwa upanga.+
12 Nami nitawasha moto katika nyumba za miungu ya Misri;+ naye hakika ataiteketeza na kuipeleka mateka na kujifunga yeye mwenyewe katika nchi ya Misri, kama mchungaji anavyojifunga katika vazi lake,+ na kwa kweli ataondoka huko kwa amani.
13 Naye hakika atavunja vipande-vipande nguzo za Beth-shemeshi, lililo katika nchi ya Misri; na nyumba za miungu ya Misri ataziteketeza kwa moto.”’”