Yeremia 38:1-28
38 Na Shefatia mwana wa Matani na Gedalia mwana wa Pashuri na Yukali+ mwana wa Shelemia na Pashuri mwana wa Malkiya+ wakayasikia maneno ambayo Yeremia alikuwa akiwaambia watu wote,+ akisema:
2 “Yehova amesema hivi, ‘Yule anayeendelea kukaa ndani ya jiji hili ndiye atakayekufa kwa upanga,+ kwa njaa+ na kwa tauni.+ Lakini yule atakayetoka nje kuwaendea Wakaldayo ndiye atakayeendelea kuishi na ndiye ambaye hakika nafsi yake itakuwa kama nyara kwake na ikiwa hai.’+
3 Yehova amesema hivi, ‘Bila shaka jiji hili litatiwa mkononi mwa jeshi la mfalme wa Babiloni, naye hakika ataliteka.’”+
4 Na wakuu wakaanza kumwambia mfalme: “Tafadhali, acha mtu huyu auawe,+ kwa maana hivyo ndivyo anavyoidhoofisha mikono ya watu wa vita ambao wamebaki ndani ya jiji hili na mikono ya watu wote, kwa kuwaambia maneno haya.+ Kwa maana mtu huyu hatafuti amani ya watu hawa bali msiba.”
5 Kwa hiyo Mfalme Sedekia akasema: “Tazama! Yuko mikononi mwenu. Kwa maana hakuna jambo lolote ambalo mfalme anaweza kuwazuia ninyi.”+
6 Nao wakamchukua Yeremia na kumtupa ndani ya tangi la maji la Malkiya+ mwana wa mfalme, lililokuwa katika Ua wa Walinzi.+ Hivyo wakamshusha Yeremia ndani kwa kamba. Basi hapakuwa na maji ndani ya lile tangi, bali matope; na Yeremia akaanza kuzama katika yale matope.+
7 Na Ebed-meleki Mwethiopia,+ mtu aliyekuwa towashi na aliyekuwa katika nyumba ya mfalme, akasikia kwamba walikuwa wamemtia Yeremia ndani ya tangi; na mfalme alikuwa ameketi katika Lango la Benyamini.+
8 Basi Ebed-meleki akatoka katika nyumba ya mfalme na kumwambia mfalme, akisema:
9 “Ee bwana wangu mfalme, watu hawa wametenda mabaya kwa yote ambayo wamemtendea Yeremia nabii, ambaye wamemtupa ndani ya tangi la maji, hivi kwamba atakufa+ hapo alipo kwa sababu ya njaa.+ Kwa maana hakuna mkate tena jijini.”
10 Ndipo mfalme akamwamuru Ebed-meleki Mwethiopia, akisema: “Chukua watu 30 chini ya usimamizi wako kutoka mahali hapa, nawe umwondoe Yeremia nabii katika lile tangi kabla hajafa.”+
11 Kwa hiyo Ebed-meleki akawachukua wale watu chini ya usimamizi wake, akaingia katika nyumba ya mfalme mpaka chini ya hazina+ na kuchukua kutoka hapo vitambaa vizee-vizee na vipande vizee-vizee vya nguo na kuvishusha kwa Yeremia ndani ya lile tangi+ kwa kamba.
12 Ndipo Ebed-meleki Mwethiopia akamwambia Yeremia: “Tafadhali, tia hivi vitambaa vizee-vizee na vipande vizee-vizee vya nguo katika makwapa yako chini ya kamba.” Basi Yeremia akafanya hivyo.+
13 Mwishowe wakamvuta Yeremia nje kwa zile kamba na kumtoa ndani ya lile tangi. Na Yeremia akaendelea kukaa katika Ua wa Walinzi.+
14 Na Mfalme Sedekia akatuma watu na kumchukua Yeremia nabii+ kwenye mlango wa tatu,+ ulio katika nyumba ya Yehova,+ kisha mfalme akamwambia Yeremia: “Ninakuuliza jambo fulani. Usinifiche jambo lolote.”+
15 Ndipo Yeremia akamwambia Sedekia: “Ikiwa nitakuambia, je, hutaniua bila shaka? Na ikiwa nitakushauri, wewe hutanisikiliza.”+
16 Kwa hiyo Mfalme Sedekia akamwapia Yeremia mahali pa maficho, akisema: “Kama anavyoishi Yehova, ambaye ametufanyia sisi nafsi+ hii, mimi sitakuua, wala sitakutia mkononi mwa watu hawa wanaoitafuta nafsi yako.”+
17 Basi Yeremia akamwambia Sedekia: “Yehova, Mungu wa majeshi,+ Mungu wa Israeli,+ amesema hivi, ‘Bila shaka ukitoka nje kwenda kwa wakuu wa mfalme wa Babiloni,+ hakika nafsi yako itaendelea kuishi na jiji hili halitateketezwa kwa moto, na wewe mwenyewe na nyumba yako hakika mtaendelea kuishi.+
18 Lakini ikiwa hutaenda nje kwa wakuu wa mfalme wa Babiloni, jiji hili pia lazima litatiwa mkononi mwa Wakaldayo, nao kwa kweli wataliteketeza kwa moto,+ nawe hutaponyoka mkononi mwao.’”+
19 Kisha Mfalme Sedekia akamwambia Yeremia: “Ninawaogopa Wayahudi ambao wamekimbia kwenda kwa Wakaldayo,+ wasije wakanitia katika mikono yao nao wakanitendea vibaya.”+
20 Lakini Yeremia akasema: “Hawatakutia mkononi mwao. Tafadhali, itii sauti ya Yehova kwa habari ya mambo ninayokuambia, na itakuwa vema kwako,+ na nafsi yako itaendelea kuishi.
21 Lakini ikiwa unakataa kwenda nje,+ hili ndilo jambo ambalo Yehova amenionyesha:
22 Na, tazama! wanawake wote ambao wameachwa katika nyumba ya mfalme wa Yuda+ wanatolewa nje kwa wakuu wa mfalme wa Babiloni,+ nao wanasema,‘Watu wanaoishi kwa amani pamoja nawe wamekushawishi+ na kukushinda.+Wamefanya mguu wako uzame chini katika matope; wamerudi nyuma kwenda upande ule mwingine.’+
23 Nao wanawatoa nje wake zako wote na wana wako wote na kuwapeleka kwa Wakaldayo, nawe mwenyewe hutaponyoka mkononi mwao,+ lakini utakamatwa kwa mkono wa mfalme wa Babiloni, na kwa sababu yako jiji hili litateketezwa kwa moto.”+
24 Na Sedekia akamwambia Yeremia: “Mtu yeyote asijue mambo haya, ili usife.
25 Na ikiwa wakuu+ watasikia kwamba nimesema nawe nao kwa kweli waje kwako na kukuambia, ‘Tafadhali, tuambie, Ulimwambia nini mfalme? Usitufiche jambo lolote, nasi hatutakuua. Na mfalme alikuambia habari gani?’
26 wewe pia utawaambia, ‘Nilikuwa nikitoa mbele ya mfalme ombi langu la kutaka kibali, kwamba asinirudishe katika nyumba ya Yehonathani+ ili nisife humo.’”
27 Baadaye wakuu wote wakamjia Yeremia na kuanza kumuuliza maswali. Yeye naye akawaambia kulingana na maneno hayo yote ambayo mfalme alikuwa ameamuru.+ Kwa hiyo wakanyamaza mbele yake, kwa maana habari hiyo haikusikiwa.
28 Na Yeremia akaendelea kukaa katika Ua wa Walinzi+ mpaka siku ambayo Yerusalemu lilitekwa.+ Na hilo likatukia wakati tu ambapo Yerusalemu lilitekwa.+