Yeremia 36:1-32

36  Ikawa kwamba katika mwaka wa nne wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, neno hili likamjia Yeremia kutoka kwa Yehova, likisema:  “Chukua kitabu cha kukunjwa,+ uandike ndani yake maneno+ yote ambayo nimekuambia juu ya Israeli na juu ya Yuda+ na juu ya mataifa yote,+ tangu siku niliyosema nawe, tangu siku za Yosia, mpaka leo hii.+  Labda wale wa nyumba ya Yuda watausikiliza msiba wote ninaofikiria kuwatendea,+ kusudi warudi, kila mmoja kutoka katika njia yake mbaya,+ na ili mimi kwa kweli nisamehe kosa lao na dhambi yao.”+  Na Yeremia akamwita Baruku+ mwana wa Neria ili Baruku aandike kwa kinywa cha Yeremia maneno yote ya Yehova ambayo Yeye alikuwa amemwambia, katika kile kitabu cha kukunjwa.+  Kisha Yeremia akamwamuru Baruku, akisema: “Nimefungiwa. Siwezi kuingia katika nyumba ya Yehova.+  Na wewe mwenyewe utaingia na kusoma kwa sauti katika kitabu cha kukunjwa ambacho umeandika kupitia kinywa changu maneno ya Yehova+ masikioni mwa watu katika nyumba ya Yehova katika siku ya kufunga;+ na pia masikioni mwa Yuda wote wanaoingia kutoka katika majiji yao unapaswa kuyasoma kwa sauti.+  Labda ombi lao la kutaka kibali litaanguka mbele za Yehova+ nao watarudi, kila mtu kutoka katika njia yake mbaya,+ kwa maana hasira na ghadhabu ni kuu ambazo Yehova amesema juu ya watu hawa.”+  Na Baruku+ mwana wa Neria akafanya kulingana na yote ambayo Yeremia nabii alikuwa amemwamuru, kusoma kwa sauti katika kile kitabu+ maneno ya Yehova kwenye nyumba ya Yehova.+  Sasa ikawa kwamba katika mwaka wa tano wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, katika mwezi wa tisa,+ watu wote katika Yerusalemu na watu wote waliokuwa wakiingia Yerusalemu kutoka katika majiji ya Yuda walitangaza kufunga mbele za Yehova.+ 10  Na Baruku akaanza kusoma kwa sauti katika kile kitabu maneno ya Yeremia kwenye nyumba ya Yehova, ndani ya chumba cha kulia chakula+ cha Gemaria+ mwana wa Shafani+ mwandikaji,+ katika ua wa juu, kwenye mwingilio wa lango jipya la nyumba ya Yehova,+ masikioni mwa watu wote. 11  Na Mikaya mwana wa Gemaria mwana wa Shafani+ akayasikia maneno yote ya Yehova katika kile kitabu. 12  Ndipo akashuka kwenye nyumba ya mfalme, kwenda katika chumba cha kulia chakula cha mwandishi, na, tazama! hapo ndipo wakuu wote walikuwa wameketi, Elishama+ mwandishi na Delaya+ mwana wa Shemaya na Elnathani+ mwana wa Akbori+ na Gemaria+ mwana wa Shafani+ na Sedekia mwana wa Hanania na wakuu wengine wote. 13  Na Mikaya+ akawaambia maneno yote ambayo alikuwa amesikia wakati Baruku aliposoma kwa sauti katika kile kitabu masikioni mwa watu.+ 14  Ndipo wakuu wote wakamtuma Yehudi+ mwana wa Nethania mwana wa Shelemia mwana wa Kushi kwa Baruku,+ na kusema: “Kile kitabu cha kukunjwa ambacho ulisoma kwa sauti masikioni mwa watu—kichukue mkononi mwako uje.” Basi Baruku mwana wa Neria akakichukua kile kitabu mkononi mwake, akaingia kwao.+ 15  Kisha wakamwambia: “Tafadhali keti, ukisome kwa sauti masikioni mwetu.” Kwa hiyo Baruku+ akasoma kwa sauti masikioni mwao. 16  Sasa ikawa kwamba mara tu walipoyasikia yale maneno yote, wakaangaliana kwa hofu; nao wakamwambia Baruku: “Bila shaka tutamwambia mfalme maneno haya yote.”+ 17  Nao wakamuuliza Baruku, wakisema: “Tafadhali tuambie, Uliandikaje maneno haya yote kutoka kinywani mwake?”+ 18  Ndipo Baruku akawaambia: “Aliendelea kunitangazia maneno haya yote kutoka kinywani mwake, nami nilikuwa nikiandika kwa wino katika kitabu.”+ 19  Mwishowe wakuu wakamwambia Baruku: “Nenda, jifiche, wewe pamoja na Yeremia, ili kwamba mtu yeyote asijue mahali mlipo.”+ 20  Kisha wakaingia kwa mfalme, kwenye ua,+ nao wakakiweka kile kitabu cha kukunjwa katika chumba cha kulia chakula+ cha Elishama+ mwandishi; nao wakaanza kusema maneno yale yote masikioni mwa mfalme. 21  Kwa hiyo mfalme akamtuma Yehudi+ kukichukua kile kitabu cha kukunjwa. Basi akakichukua kutoka katika chumba cha kulia chakula cha Elishama+ mwandishi.+ Na Yehudi akaanza kukisoma kwa sauti masikioni mwa mfalme na masikioni mwa wakuu wote waliokuwa wamesimama kando ya mfalme. 22  Na mfalme alikuwa ameketi katika nyumba ya majira ya baridi kali,+ katika mwezi wa tisa,+ na jiko la makaa+ lilikuwa linawaka mbele yake. 23  Kisha ikawa kwamba mara tu Yehudi alipokuwa amesoma safu za kurasa tatu au nne, akakipasua kwa kisu cha mwandishi, na pia akakitupa katika moto uliokuwa katika lile jiko mpaka kitabu chote kilipoishia ndani ya ule moto uliokuwa katika jiko.+ 24  Nao hawakuingiwa na hofu yoyote;+ na mfalme wala watumishi wake wote, waliokuwa wakisikiliza maneno hayo yote, hawakurarua mavazi yao.+ 25  Na hata Elnathani+ na Delaya+ na Gemaria+ wakamsihi mfalme asiteketeze kile kitabu cha kukunjwa, lakini hakuwasikiliza.+ 26  Na zaidi ya hayo, mfalme akawaamuru Yerahmeeli mwana wa mfalme na Seraya mwana wa Azrieli na Shelemia mwana wa Abdeeli waende kumleta Baruku mwandishi na Yeremia nabii.+ Lakini Yehova akaendelea kuwaficha.+ 27  Na neno la Yehova likamjia Yeremia tena baada ya mfalme kukiteketeza kile kitabu cha kukunjwa pamoja na yale maneno ambayo Baruku+ alikuwa ameandika kutoka katika kinywa cha Yeremia,+ na kusema: 28  “Chukua tena kitabu cha kukunjwa, kingine, nawe uandike juu yake yale maneno yote ya kwanza yaliyokuwa juu ya kile kitabu cha kwanza, ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda aliteketeza.+ 29  Nawe unapaswa kusema hivi juu ya Yehoyakimu mfalme wa Yuda, ‘Yehova amesema hivi: “Wewe mwenyewe umekiteketeza hiki kitabu cha kukunjwa,+ ukisema, ‘Kwa nini umeandika juu yake,+ ukisema: “Mfalme wa Babiloni atakuja bila shaka na hakika ataiharibu nchi hii na kumkomesha mwanadamu na mnyama kutoka ndani yake”?’+ 30  Kwa hiyo Yehova amesema hivi juu ya Yehoyakimu mfalme wa Yuda, ‘Hatakuwa na mtu yeyote anayeketi juu ya kiti cha ufalme cha Daudi,+ na maiti yake itakuwa kitu kilichotupwa nje+ kwenye joto wakati wa mchana na kwenye baridi kali wakati wa usiku. 31  Nami nitamtoza hesabu yeye+ na uzao wake na watumishi wake kosa lao,+ nami nitaleta juu yao na juu ya wakaaji wa Yerusalemu na juu ya watu wa Yuda ule msiba wote ambao nimesema juu yao,+ nao hawakusikiliza.’”’”+ 32  Na Yeremia akachukua kitabu kingine cha kukunjwa, akampa Baruku mwana wa Neria, mwandishi,+ ambaye aliandika juu yake kutoka kinywani+ mwa Yeremia maneno yote ya kile kitabu ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda alikuwa ameteketeza motoni;+ na maneno mengine mengi kama hayo yakaongezwa kwenye hayo.

Maelezo ya Chini