Yeremia 3:1-25
3 Kuna msemo: “Mwanamume akimwacha mke wake na mke huyo aondoke kwake na kuwa wa mwanamume mwingine, je, mwanamume huyo anapaswa kurudi kwake tena?”+
Je, nchi hiyo haikutiwa unajisi hakika?+
“Nawe mwenyewe umefanya ukahaba pamoja na rafiki wengi;+ na je, unapaswa kurudi kwangu mimi?”+ asema Yehova.
2 “Inua macho yako kuelekea mapito yaliyokanyagwa, ukaone.+ Ni wapi ambapo hawakukulala kinguvu?+ Umekaa kando ya njia kwa ajili yao, kama Mwarabu nyikani;+ nawe unaendelea kuitia nchi unajisi kwa matendo yako ya ukahaba na kwa ubaya wako.+
3 Kwa hiyo manyunyu mengi yamezuiwa,+ na hata mvua ya masika haikunyesha.+ Nawe umekuwa na paji la uso la mke anayefanya ukahaba. Umekataa kufedheheka.+
4 Je, umeniita kutoka sasa na kuendelea ‘Baba yangu,+ wewe ni rafiki wa karibu wa ujana wangu!+
5 Je, mtu anapaswa kufungia kinyongo mpaka wakati usio na kipimo, au kuendelea kuangalia jambo milele?’+ Tazama! Umesema, nawe ukaendelea kufanya mambo mabaya na kupata ushindi.”+
6 Na Yehova akaniambia katika siku za mfalme Yosia:+ “‘Je, umeona lile ambalo Israeli asiye mwaminifu amefanya?+ Anaenda juu ya kila mlima mrefu+ na chini ya kila mti wenye majani mengi,+ ili afanye ukahaba huko.+
7 Na baada ya yeye kufanya mambo hayo yote niliendelea kusema kwamba arudi kwangu, lakini hakurudi;+ na Yuda akaendelea kumtazama dada yake mwenye hila.+
8 Nilipoona jambo hilo, kwa sababu Israeli asiye mwaminifu alikuwa amefanya uzinzi, nilimfukuza+ nami nikampa cheti chake cha talaka kamili,+ ingawa hivyo Yuda, dada yake anayetenda kwa hila, hakuogopa, bali yeye mwenyewe pia akaanza kwenda na kufanya ukahaba.+
9 Na ukahaba wake ulifanyika kwa sababu ya maoni yake ya kipuuzi, naye aliendelea kuitia nchi unajisi+ na kufanya uzinzi pamoja na mawe na pamoja na miti;+
10 na hata ijapokuwa hayo yote Yuda dada yake mwenye hila hakurudi kwangu kwa moyo+ wake wote, ila kwa uwongo,’+ asema Yehova.”
11 Na Yehova akaendelea kuniambia: “Israeli asiye mwaminifu ameonyesha nafsi yake kuwa yenye uadilifu kuliko Yuda anayetenda kwa hila.+
12 Nenda, nawe uitangazie kaskazini+ maneno haya na kusema:
“‘“Rudi, Ee Israeli mwenye kuasi,” asema Yehova.’+ ‘ “Sitawatazama ninyi kwa hasira,+ kwa maana mimi ni mshikamanifu,”+ asema Yehova.’ ‘ “Sitaendelea kufungia kinyongo mpaka wakati usio na kipimo.+
13 Ila uangalie tu kosa lako, kwa maana umemkosea Yehova Mungu wako.+ Nawe umeendelea kutawanya njia zako kwa wageni+ chini ya kila mti wenye majani mengi,+ lakini ninyi hamkuisikiliza sauti yangu,” asema Yehova.’”
14 “Rudini, enyi wana waasi,’+ asema Yehova. “Kwa maana mimi nimekuwa mume wenu;+ nami nitawachukua, mmoja kutoka katika jiji moja na wawili kutoka katika familia moja, nami nitawaleta ninyi Sayuni.+
15 Nami nitawapa wachungaji wenye kupatana na moyo wangu,+ na hakika wao watawalisha ninyi kwa ujuzi na ufahamu.+
16 Na itatukia kwamba mtakuwa wengi nanyi hakika mtazaa matunda katika nchi siku hizo,” asema Yehova.+ “Hawatasema tena, ‘Sanduku la agano la Yehova!’+ wala halitaingia moyoni, wala hawatalikumbuka+ au kulitamani, nalo halitafanywa tena.
17 Wakati huo wataita Yerusalemu kuwa kiti cha ufalme cha Yehova;+ na mataifa yote yataletwa pamoja+ kwake kwa jina la Yehova katika Yerusalemu,+ nao hawataufuata tena ukaidi wa moyo wao mbaya.”+
18 “Katika siku hizo watatembea, nyumba ya Yuda ikiwa kando ya nyumba ya Israeli,+ nao pamoja+ watatoka katika nchi ya kaskazini na kuingia katika nchi ambayo niliwapa mababu zenu kuwa fungu la urithi.+
19 Nami mwenyewe nimesema, ‘Lo! jinsi nilivyokuweka kati ya wana na kukupa nchi yenye kutamanika,+ fungu la urithi la pambo la majeshi ya mataifa!’ Nami nikasema tena, Ninyi mtaniita ‘ “Baba yangu!”+ nanyi hamtarudi mwache kunifuata.’
20 ‘Kwa kweli kama mke anavyomwacha mwenzake kwa hila,+ ndivyo ninyi, enyi nyumba ya Israeli, mlivyonitendea kwa hila,’+ asema Yehova.”
21 Sauti imesikika katika njia zilizokanyagwa, kulia, kusihi kwa wana wa Israeli. Kwa maana wameipotosha njia yao;+ wamemsahau Yehova Mungu wao.+
22 “Rudini, ninyi wana waasi.+ Nitaiponya hali yenu ya uasi.”+
“Sisi hapa! Tumekuja kwako, kwa maana wewe, Ee Yehova, ni Mungu wetu.+
23 Kwa kweli vilima na pia machafuko juu ya milima+ ni uwongo.+ Kwa kweli wokovu wa Israeli uko katika Yehova Mungu wetu.+
24 Lakini jambo la aibu+ limekula kazi ya mababu zetu tangu ujana wetu, makundi yao na mifugo yao, wana wao na binti zao.
25 Tunalala katika aibu+ yetu, na fedheha yetu inaendelea kutufunika;+ kwa maana tumemtendea dhambi+ Yehova Mungu wetu, sisi na baba zetu tangu ujana wetu na kuendelea mpaka leo hii,+ nasi hatukuitii sauti ya Yehova Mungu wetu.”+