Yeremia 3:1-25

3  Kuna msemo: “Mwanamume akimwacha mke wake na mke huyo aondoke kwake na kuwa wa mwanamume mwingine, je, mwanamume huyo anapaswa kurudi kwake tena?”+ Je, nchi hiyo haikutiwa unajisi hakika?+ “Nawe mwenyewe umefanya ukahaba pamoja na rafiki wengi;+ na je, unapaswa kurudi kwangu mimi?”+ asema Yehova.  “Inua macho yako kuelekea mapito yaliyokanyagwa, ukaone.+ Ni wapi ambapo hawakukulala kinguvu?+ Umekaa kando ya njia kwa ajili yao, kama Mwarabu nyikani;+ nawe unaendelea kuitia nchi unajisi kwa matendo yako ya ukahaba na kwa ubaya wako.+  Kwa hiyo manyunyu mengi yamezuiwa,+ na hata mvua ya masika haikunyesha.+ Nawe umekuwa na paji la uso la mke anayefanya ukahaba. Umekataa kufedheheka.+  Je, umeniita kutoka sasa na kuendelea ‘Baba yangu,+ wewe ni rafiki wa karibu wa ujana wangu!+  Je, mtu anapaswa kufungia kinyongo mpaka wakati usio na kipimo, au kuendelea kuangalia jambo milele?’+ Tazama! Umesema, nawe ukaendelea kufanya mambo mabaya na kupata ushindi.”+  Na Yehova akaniambia katika siku za mfalme Yosia:+ “‘Je, umeona lile ambalo Israeli asiye mwaminifu amefanya?+ Anaenda juu ya kila mlima mrefu+ na chini ya kila mti wenye majani mengi,+ ili afanye ukahaba huko.+  Na baada ya yeye kufanya mambo hayo yote niliendelea kusema kwamba arudi kwangu, lakini hakurudi;+ na Yuda akaendelea kumtazama dada yake mwenye hila.+  Nilipoona jambo hilo, kwa sababu Israeli asiye mwaminifu alikuwa amefanya uzinzi, nilimfukuza+ nami nikampa cheti chake cha talaka kamili,+ ingawa hivyo Yuda, dada yake anayetenda kwa hila, hakuogopa, bali yeye mwenyewe pia akaanza kwenda na kufanya ukahaba.+  Na ukahaba wake ulifanyika kwa sababu ya maoni yake ya kipuuzi, naye aliendelea kuitia nchi unajisi+ na kufanya uzinzi pamoja na mawe na pamoja na miti;+ 10  na hata ijapokuwa hayo yote Yuda dada yake mwenye hila hakurudi kwangu kwa moyo+ wake wote, ila kwa uwongo,’+ asema Yehova.” 11  Na Yehova akaendelea kuniambia: “Israeli asiye mwaminifu ameonyesha nafsi yake kuwa yenye uadilifu kuliko Yuda anayetenda kwa hila.+ 12  Nenda, nawe uitangazie kaskazini+ maneno haya na kusema: “‘“Rudi, Ee Israeli mwenye kuasi,” asema Yehova.’+ ‘ “Sitawatazama ninyi kwa hasira,+ kwa maana mimi ni mshikamanifu,”+ asema Yehova.’ ‘ “Sitaendelea kufungia kinyongo mpaka wakati usio na kipimo.+ 13  Ila uangalie tu kosa lako, kwa maana umemkosea Yehova Mungu wako.+ Nawe umeendelea kutawanya njia zako kwa wageni+ chini ya kila mti wenye majani mengi,+ lakini ninyi hamkuisikiliza sauti yangu,” asema Yehova.’” 14  “Rudini, enyi wana waasi,’+ asema Yehova. “Kwa maana mimi nimekuwa mume wenu;+ nami nitawachukua, mmoja kutoka katika jiji moja na wawili kutoka katika familia moja, nami nitawaleta ninyi Sayuni.+ 15  Nami nitawapa wachungaji wenye kupatana na moyo wangu,+ na hakika wao watawalisha ninyi kwa ujuzi na ufahamu.+ 16  Na itatukia kwamba mtakuwa wengi nanyi hakika mtazaa matunda katika nchi siku hizo,” asema Yehova.+ “Hawatasema tena, ‘Sanduku la agano la Yehova!’+ wala halitaingia moyoni, wala hawatalikumbuka+ au kulitamani, nalo halitafanywa tena. 17  Wakati huo wataita Yerusalemu kuwa kiti cha ufalme cha Yehova;+ na mataifa yote yataletwa pamoja+ kwake kwa jina la Yehova katika Yerusalemu,+ nao hawataufuata tena ukaidi wa moyo wao mbaya.”+ 18  “Katika siku hizo watatembea, nyumba ya Yuda ikiwa kando ya nyumba ya Israeli,+ nao pamoja+ watatoka katika nchi ya kaskazini na kuingia katika nchi ambayo niliwapa mababu zenu kuwa fungu la urithi.+ 19  Nami mwenyewe nimesema, ‘Lo! jinsi nilivyokuweka kati ya wana na kukupa nchi yenye kutamanika,+ fungu la urithi la pambo la majeshi ya mataifa!’ Nami nikasema tena, Ninyi mtaniita ‘ “Baba yangu!”+ nanyi hamtarudi mwache kunifuata.’ 20  ‘Kwa kweli kama mke anavyomwacha mwenzake kwa hila,+ ndivyo ninyi, enyi nyumba ya Israeli, mlivyonitendea kwa hila,’+ asema Yehova.” 21  Sauti imesikika katika njia zilizokanyagwa, kulia, kusihi kwa wana wa Israeli. Kwa maana wameipotosha njia yao;+ wamemsahau Yehova Mungu wao.+ 22  “Rudini, ninyi wana waasi.+ Nitaiponya hali yenu ya uasi.”+ “Sisi hapa! Tumekuja kwako, kwa maana wewe, Ee Yehova, ni Mungu wetu.+ 23  Kwa kweli vilima na pia machafuko juu ya milima+ ni uwongo.+ Kwa kweli wokovu wa Israeli uko katika Yehova Mungu wetu.+ 24  Lakini jambo la aibu+ limekula kazi ya mababu zetu tangu ujana wetu, makundi yao na mifugo yao, wana wao na binti zao. 25  Tunalala katika aibu+ yetu, na fedheha yetu inaendelea kutufunika;+ kwa maana tumemtendea dhambi+ Yehova Mungu wetu, sisi na baba zetu tangu ujana wetu na kuendelea mpaka leo hii,+ nasi hatukuitii sauti ya Yehova Mungu wetu.”+

Maelezo ya Chini