Yeremia 29:1-32
29 Na haya ndiyo maneno ya barua ambayo Yeremia nabii alituma kutoka Yerusalemu kwa mabaki ya wanaume wazee wa watu waliohamishwa na kwa makuhani na kwa manabii na kwa watu wote, ambao Nebukadneza alikuwa amewapeleka uhamishoni kutoka Yerusalemu kwenda Babiloni+
2 baada ya Yekonia+ mfalme na malkia+ na maofisa wa makao ya mfalme, wakuu wa Yuda na Yerusalemu,+ na mafundi na wajenzi wa maboma+ kwenda kutoka katika Yerusalemu.
3 Ilikuwa kwa mkono wa Elasa mwana wa Shafani+ na Gemaria mwana wa Hilkia, ambao Sedekia+ mfalme wa Yuda aliwatuma kwenda Babiloni kwa Nebukadneza mfalme wa Babiloni, na kusema:
4 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amewaambia hivi watu wote waliohamishwa, ambao nimewapeleka uhamishoni+ kutoka Yerusalemu kwenda Babiloni,
5 ‘Jengeni nyumba na kukaa ndani yake, mpande bustani na kula matunda yake.+
6 Chukueni wake na kuzaa wana na binti;+ na kuwachukulia wana wenu wake na kuwaoza binti zenu kwa waume, ili wazae wana na binti; na muwe wengi huko, wala msiwe wachache.
7 Pia, tafuteni amani kwa ajili ya jiji ambamo nimewapeleka ninyi uhamishoni, nanyi msali kwa ajili yake kwa Yehova, kwa maana katika amani ya jiji hilo kutakuwa na amani kwa ajili yenu wenyewe.+
8 Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi: “Msiache manabii wenu walio katikati yenu na waaguzi wenu wawadanganye,+ nanyi msisikilize ndoto zao ambazo wanaota.+
9 Kwa maana ‘wanawatolea ninyi unabii wa uwongo katika jina langu. Mimi sikuwatuma,’+ asema Yehova.”’”
10 “Kwa maana Yehova amesema hivi, ‘Kupatana na kutimia kwa miaka 70 katika Babiloni nitawakazia ninyi fikira,+ nami nitawatimizia neno langu jema kwa kuwarudisha tena mahali hapa.’+
11 “‘Kwa maana mimi najua vema mawazo ninayofikiria kuwaelekea ninyi,’+ asema Yehova, ‘mawazo ya amani, wala si ya msiba,+ ili kuwapa ninyi wakati ujao na tumaini.+
12 Na hakika mtaniita na kuja na kusali kwangu, nami nitawasikiliza.’+
13 “‘Nanyi kwa kweli mtanitafuta na kunipata,+ kwa maana mtanitafuta kwa moyo wenu wote.+
14 Nami nitajiacha mnipate,’+ asema Yehova. ‘Nami nitakusanya kundi lenu la mateka na kuwakusanya ninyi pamoja kutoka katika mataifa yote na kutoka katika mahali pote ambapo nimewatawanya ninyi,’+ asema Yehova. ‘Nami nitawarudisha katika mahali ambapo kutoka hapo niliwapeleka uhamishoni.’+
15 “Lakini mmesema, ‘Yehova ametuinulia manabii katika Babiloni.’
16 “Kwa maana Yehova amesema hivi kwa mfalme anayeketi juu ya kiti cha ufalme cha Daudi+ na kwa watu wote wanaokaa katika jiji hili, ndugu zenu ambao hawakwenda pamoja nanyi uhamishoni,+
17 ‘Yehova wa majeshi amesema hivi: “Tazama, ninatuma juu yao upanga,+ njaa+ na tauni,+ nami nitawafanya kuwa kama tini zilizopasuka ambazo haziwezi kuliwa kwa sababu ya ubaya.”’+
18 “‘Nami nitawafuatilia kwa upanga, kwa njaa na kwa tauni, nami nitawatoa wawe kitu cha kutetemesha falme zote za dunia,+ kuwa laana na kuwa kitu cha kushangaza na kuwa kitu cha kupigiwa mluzi na kuwa kitu cha kushutumiwa katikati ya mataifa yote ambako hakika nitawatawanya,+
19 kwa sababu hawakuyasikiliza maneno yangu,’ asema Yehova, ‘ambayo nimetuma kwao kupitia watumishi wangu manabii, nikiamka mapema na kuwatuma.’+
“‘Lakini hamkusikiliza,’+ asema Yehova.
20 “Nanyi sikieni neno la Yehova, ninyi nyote mliohamishwa,+ ambao nimewafukuza kutoka Yerusalemu kwenda Babiloni.+
21 Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi kumhusu Ahabu mwana wa Kolaya na kumhusu Sedekia mwana wa Maaseya, ambao wanawatolea ninyi unabii wa uwongo katika jina langu mwenyewe,+ ‘Tazama, nitawatia mkononi mwa Nebukadreza mfalme wa Babiloni, naye atawapiga na kuwaua mbele ya macho yenu.+
22 Na kutoka kwao hakika laana itachukuliwa na kundi zima la wahamishwa walio katika Babiloni, na kusema: “Yehova na akufanye kama Sedekia na kama Ahabu,+ ambao mfalme wa Babiloni aliwachoma motoni!”+
23 kwa sababu wametenda upumbavu katika Israeli,+ nao wanaendelea kufanya uzinzi pamoja na wake za wenzao+ na kuendelea kusema uwongo kwa jina langu mwenyewe neno ambalo mimi sikuwaamuru.+
“‘“Mimi ndiye ninayejua nami ni shahidi,”+ asema Yehova.’”
24 “Nawe utamwambia hivi Shemaya+ wa Nehelamu,
25 ‘Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi: “Kwa sababu wewe umetuma barua+ katika jina lako kwa watu wote walioko Yerusalemu, na kwa Sefania+ mwana wa Maaseya, kuhani, na kwa makuhani wote, ukisema,
26 ‘Yehova amekufanya wewe kuwa kuhani badala ya Yehoyada kuhani, ili uwe mwangalizi mkuu wa nyumba ya Yehova+ kuelekea mtu yeyote aliyetiwa wazimu+ na mwenye kujiendesha kama nabii, nawe utamtia katika mikatale na katika kongwa;+
27 sasa, basi, kwa nini hukumkemea Yeremia wa Anathothi,+ ambaye anajiendesha kama nabii kwenu?+
28 Kwa maana ndiyo sababu ametuma ujumbe kwetu Babiloni, akisema: “Ni wa muda mrefu! Jengeni nyumba na kukaa ndani yake, na kupanda bustani na kula matunda yake,+ — ”’”’”
29 Na Sefania+ kuhani akaisoma barua hii masikioni mwa Yeremia nabii.
30 Ndipo neno la Yehova likamjia Yeremia, na kusema:
31 “Tuma ujumbe kwa watu wote waliohamishwa,+ ukisema, ‘Yehova amesema hivi kumhusu Shemaya wa Nehelamu: “Kwa sababu Shemaya amewatolea ninyi unabii, lakini mimi mwenyewe sikumtuma, naye alijaribu kuwafanya mtegemee uwongo,+
32 basi Yehova amesema hivi, ‘Tazama, ninakaza fikira zangu juu ya Shemaya+ wa Nehelamu na juu ya uzao wake.’+
“‘“‘Hatakuwa na mtu anayekaa katikati ya kikundi hiki cha watu;+ wala hatautazama wema ambao nitawafanyia watu wangu,’+ asema Yehova, ‘kwa maana amesema maasi ya waziwazi juu ya Yehova.’”’”+