Yeremia 28:1-17
28 Kisha ikawa kwamba mwaka huo, katika mwanzo wa ufalme wa Sedekia+ mfalme wa Yuda, katika mwaka wa nne, mwezi wa tano, Hanania+ mwana wa Azuri, yule nabii kutoka Gibeoni,+ akaniambia hivi ndani ya nyumba ya Yehova mbele ya macho ya makuhani na ya watu wote:
2 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Nitaivunja nira ya mfalme wa Babiloni.+
3 Katika muda wa miaka miwili kamili nitavirudisha mahali hapa vyombo vyote vya nyumba ya Yehova ambavyo Nebukadneza mfalme wa Babiloni+ alivichukua kutoka mahali hapa ili kuvipeleka Babiloni.’”
4 “‘Na Yekonia+ mwana wa Yehoyakimu,+ mfalme wa Yuda, pamoja na wahamishwa wote wa Yuda ambao wameenda Babiloni+ nitawarudisha tena mahali hapa,’ asema Yehova, ‘kwa maana nitaivunja nira+ ya mfalme wa Babiloni.’”
5 Na Yeremia nabii akamwambia Hanania nabii mbele ya macho ya makuhani na mbele ya macho ya watu wote waliokuwa wamesimama ndani ya nyumba ya Yehova;+
6 ndiyo, Yeremia nabii akasema: “Amina!+ Yehova na afanye hivyo! Yehova na ayatimize maneno yako ambayo umetoa unabii kwa kuvirudisha tena mahali hapa kutoka Babiloni vyombo vya nyumba ya Yehova na watu wote waliohamishwa!+
7 Hata hivyo, tafadhali sikia neno hili ninalosema masikioni mwako na masikioni mwa watu wote.+
8 Kwa habari ya manabii walionitangulia mimi na waliokutangulia wewe kutoka zamani za kale,+ wao pia walikuwa wakitoa unabii kuhusu nchi nyingi na kuhusu falme kubwa, juu ya vita na juu ya msiba na juu ya tauni.+
9 Kwa habari ya nabii anayetoa unabii wa amani,+ wakati neno la nabii huyo litakapotimia yule nabii ambaye Yehova amemtuma kikweli atajulikana.”+
10 Ndipo Hanania nabii akaichukua ile nira kutoka shingoni mwa Yeremia nabii na kuivunja.+
11 Na Hanania+ akasema mbele ya macho ya watu wote: “Yehova amesema hivi,+ ‘Hivi ndivyo nitakavyoivunja nira ya Nebukadneza mfalme wa Babiloni katika muda wa miaka miwili kamili ili itoke shingoni mwa mataifa yote.’”+ Na Yeremia nabii akaenda zake.+
12 Ndipo neno la Yehova likamjia Yeremia,+ baada ya Hanania nabii kuivunja ile nira kutoka shingoni mwa Yeremia nabii, na kusema:
13 “Nenda, umwambie Hanania, ‘Yehova amesema hivi: “Umevunja nira+ za miti, na badala ya hizo utatengeneza nira za chuma.”+
14 Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi: “Nitatia nira ya chuma juu ya shingo ya mataifa haya yote, ili yamtumikie Nebukadneza mfalme wa Babiloni;+ nao lazima watamtumikia.+ Nami nitampa hata wanyama wa mwituni.”’”+
15 Na Yeremia nabii akaendelea kumwambia Hanania+ nabii: “Tafadhali, sikiliza, Ee Hanania! Yehova hakukutuma wewe, bali wewe mwenyewe umewafanya watu hawa wautegemee uwongo.+
16 Kwa hiyo Yehova amesema hivi, ‘Tazama! Ninakuondolea mbali kutoka katika uso wa nchi. Mwaka huu utakufa hakika,+ kwa maana umesema maasi ya waziwazi juu ya Yehova.’”+
17 Basi Hanania nabii akafa mwaka huo, katika mwezi wa saba.+