Yeremia 26:1-24
26 Katika mwanzo wa utawala wa kifalme wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, neno hili lilikuja kutoka kwa Yehova, na kusema:
2 “Yehova amesema hivi, ‘Simama katika ua wa nyumba ya Yehova,+ nawe useme kuhusu majiji yote ya Yuda yanayokuja kuinama katika nyumba ya Yehova, useme maneno yote nitakayokuamuru uwaambie.+ Usiondoe hata neno moja.+
3 Labda watasikiliza na kurudi, kila mmoja kutoka katika njia yake mbaya,+ nami nitajuta msiba ninaofikiria kuleta juu yao kwa sababu ya ubaya wa matendo yao.+
4 Nawe uwaambie: “Yehova amesema hivi, ‘Ikiwa hamtanisikiliza kwa kutembea katika sheria yangu+ ambayo nimeweka mbele yenu,+
5 kwa kuyasikiliza maneno ya watumishi wangu manabii, ambao ninawatuma kwenu, nikiamka mapema na kuwatuma, ambao hamkuwasikiliza,+
6 mimi, kwa upande wangu, nitaifanya nyumba hii kama ile iliyo katika Shilo,+ na jiji hili nitalifanya kuwa laana kwa mataifa yote ya dunia.’”’”+
7 Na makuhani na manabii na watu wote wakaanza kumsikia Yeremia akisema maneno hayo ndani ya nyumba ya Yehova.+
8 Basi ikawa kwamba Yeremia alipokuwa amemaliza kusema yote ambayo Yehova alimwamuru kuwaambia watu wote, ndipo makuhani na manabii na watu wote wakamkamata, wakisema: “Hakika utakufa.+
9 Kwa nini umetoa unabii katika jina la Yehova, ukisema, ‘Nyumba hii itakuwa kama ile iliyo katika Shilo,+ nalo jiji hili litafanywa ukiwa hivi kwamba halitakuwa na mkaaji’?” Na watu wote wakaendelea kujikutanisha kumzunguka Yeremia ndani ya nyumba ya Yehova.
10 Baada ya muda wakuu wa Yuda wakasikia maneno hayo, nao wakatoka katika nyumba ya mfalme wakapanda kwenda katika nyumba ya Yehova+ na kuketi katika mwingilio wa lango jipya la Yehova.+
11 Na makuhani na manabii wakaanza kuwaambia wakuu na watu wote: “Mtu huyu anastahili hukumu ya kifo,+ kwa sababu ametoa unabii kulihusu jiji hili kama mlivyosikia kwa masikio yenu wenyewe.”+
12 Ndipo Yeremia akawaambia wakuu wote na watu wote: “Yehova ndiye aliyenituma kutoa unabii kuihusu nyumba hii na kulihusu jiji hili maneno yote ambayo mmeyasikia.+
13 Na sasa fanyeni njia zenu na matendo yenu yawe mema,+ na mwitii sauti ya Yehova Mungu wenu, na Yehova ataujuta msiba ambao amesema juu yenu.+
14 Na kwa habari yangu, tazama, mimi nipo hapa mkononi mwenu.+ Nitendeeni kulingana na yaliyo mema na kulingana na yaliyo sawa machoni penu.+
15 Ila tu mnapaswa kujua kabisa kwamba, ikiwa mnaniua, ni damu isiyo na hatia ambayo mnajiletea juu yenu wenyewe na juu ya jiji hili na juu ya wakaaji wake,+ kwa maana kwa kweli Yehova alinituma kwenu niseme masikioni mwenu maneno haya yote.”+
16 Ndipo wakuu+ na watu wote wakawaambia makuhani na manabii: “Hakuna hukumu ya kifo anayostahili mtu huyu,+ kwa maana alisema nasi katika jina la Yehova Mungu wetu.”+
17 Na zaidi ya hayo, watu fulani kati ya wanaume wazee wa nchi wakasimama na kuanza kuliambia kutaniko lote la watu:+
18 “Mika+ wa Moreshethi+ alikuwa akitoa unabii katika siku za Hezekia mfalme wa Yuda+ naye akawaambia watu wote wa Yuda, ‘Yehova wa majeshi amesema hivi: “Sayuni utalimwa kama shamba,+ na Yerusalemu litakuwa marundo ya mabomoko,+ na mlima wa ile Nyumba utakuwa kama mahali pa juu pa msitu.”’+
19 Je, Hezekia mfalme wa Yuda na wale wote wa Yuda walimuua? Je, hakumwogopa Yehova na kuanza kuutuliza uso wa Yehova,+ hivi kwamba Yehova akajuta ule msiba ambao alikuwa ametangaza juu yao?+ Basi sisi tunajifanyia msiba mkubwa juu ya nafsi zetu.+
20 “Na pia palikuwa na mtu aliyekuwa akitoa unabii katika jina la Yehova, Uriya mwana wa Shemaya kutoka Kiriath-yearimu.+ Naye aliendelea kutoa unabii juu ya jiji hili na juu ya nchi hii sawasawa na maneno yote ya Yeremia.
21 Na Mfalme Yehoyakimu+ na wanaume wake wote wenye nguvu na wakuu wote wakayasikia maneno yake, na mfalme akaanza kutafuta kumuua.+ Uriya aliposikia habari hizo, akaogopa+ mara moja, akakimbia, akaingia Misri.
22 Lakini Mfalme Yehoyakimu akatuma watu Misri, Elnathani mwana wa Akbori+ na watu wengine pamoja naye mpaka Misri.
23 Nao wakamleta Uriya kutoka Misri na kumleta kwa Mfalme Yehoyakimu, kisha akampiga na kumuua kwa upanga+ na kuitupa maiti yake katika makaburi ya wana wa watu.”
24 Zaidi ya hayo, mkono wa Ahikamu+ mwana wa Shafani+ ndio uliokuwa pamoja na Yeremia, asitiwe mkononi mwa watu ili auawe.+