Yeremia 25:1-38
25 Neno lililomjia Yeremia kuhusu watu wote wa Yuda katika mwaka wa nne wa Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, yaani, mwaka wa kwanza wa Nebukadreza mfalme wa Babiloni;
2 ambalo Yeremia nabii alisema kuhusu watu wote wa Yuda na kuhusu wakaaji wote wa Yerusalemu, akisema:
3 “Tangu mwaka wa 13 wa Yosia+ mwana wa Amoni, mfalme wa Yuda, mpaka leo hii, miaka hii 23, neno la Yehova limenijia, nikaendelea kusema nanyi, nikiamka mapema na kusema, lakini hamkusikiliza.+
4 Na Yehova alituma kwenu watumishi wake wote manabii, akiamka mapema na kuwatuma, lakini hamkusikiliza,+ wala hamkutega sikio lenu ili kusikiliza,+
5 wao wakisema, ‘Tafadhali, geukeni kila mmoja kutoka katika njia yake mbaya na kutoka katika ubaya wa matendo yake,+ nanyi mwendelee kukaa juu ya nchi ambayo Yehova aliwapa ninyi na mababu zenu tangu zamani za kale na mpaka wakati mrefu ujao.+
6 Nanyi msifuate miungu mingine ili kuitumikia na kuiinamia, ili msinitie uchungu mimi kwa kazi ya mikono yenu, na ili nisiwaletee ninyi msiba.’+
7 “‘Lakini hamkunisikiliza mimi,’ asema Yehova, ‘kusudi mnitie uchungu kwa kazi ya mikono yenu, ili kujiletea wenyewe msiba.’+
8 “Kwa hiyo Yehova wa majeshi amesema hivi, ‘ “Kwa sababu hamkuyatii maneno yangu,
9 tazama, ninatuma, nami nitazichukua familia zote za kaskazini,”+ asema Yehova, “nitatuma ujumbe kwa Nebukadreza mfalme wa Babiloni, mtumishi wangu,+ nami nitawaleta wao juu ya nchi hii+ na juu ya wakaaji wake na juu ya haya mataifa yote kuzunguka pande zote;+ nami nitawaangamiza na kuwafanya kuwa kitu cha kushangaza na kitu cha kupigiwa mluzi+ na ukiwa mpaka wakati usio na kipimo.+
10 Nami nitaangamiza kutoka ndani yao sauti ya furaha na sauti ya shangwe,+ sauti ya bwana-arusi na sauti ya bibi-arusi,+ sauti ya jiwe la kusagia la mkononi+ na nuru ya taa.+
11 Na nchi hii yote itakuwa mahali palipoharibiwa, kitu cha kushangaza, na mataifa haya yatamtumikia mfalme wa Babiloni miaka 70.”’+
12 “‘Na itatukia kwamba miaka 70 itakapotimia+ nitatoza hesabu juu ya mfalme wa Babiloni na juu ya taifa lake,’+ asema Yehova, ‘kwa sababu ya kosa lao, juu ya nchi ya Wakaldayo,+ nami nitaifanya kuwa mahame yenye ukiwa mpaka wakati usio na kipimo.+
13 Nami nitaleta juu ya nchi ile maneno yangu yote ambayo nimesema juu yake, yote ambayo yameandikwa katika kitabu hiki ambacho Yeremia ametoa unabii juu ya mataifa yote.+
14 Kwa maana hata wao wenyewe, mataifa mengi na wafalme wakubwa,+ wamewatumia vibaya kama watumishi;+ nami nitawalipa kulingana na matendo yao na kulingana na kazi ya mikono yao.’”+
15 Kwa maana Yehova Mungu wa Israeli ameniambia hivi: “Chukua kikombe hiki cha divai ya ghadhabu kutoka mkononi mwangu, nawe ukinyweshe+ mataifa yote ambayo ninakutuma kwao.
16 Nao lazima wanywe na kuyumba-yumba na kutenda kama wenda-wazimu kwa sababu ya upanga ninaotuma katikati yao.”+
17 Ndipo nikakichukua kile kikombe kutoka mkononi mwa Yehova na kukinywesha mataifa yote ambayo Yehova alikuwa amenituma kwao:+
18 yaani, Yerusalemu na majiji ya Yuda na wafalme wake, wakuu wake, ili kuyafanya kuwa ukiwa, kitu cha kushangaza,+ kitu cha kupigiwa mluzi na laana, kama ilivyo leo hii;+
19 Farao mfalme wa Misri na watumishi wake na wakuu wake na watu wake wote;+
20 na jamii yote iliyochangamana, na wafalme wote wa nchi ya Usi,+ na wafalme wote wa nchi ya Wafilisti+ na Ashkeloni+ na Gaza+ na Ekroni+ na mabaki ya Ashdodi;+
21 Edomu+ na Moabu+ na wana wa Amoni;+
22 na wafalme wote wa Tiro+ na wafalme wote wa Sidoni+ na wafalme wa kisiwa kilicho katika eneo la bahari;
23 na Dedani+ na Tema+ na Buzi na wale wote wenye nywele zilizokatwa kwenye vipaji vya nyuso;+
24 na wafalme wote wa Waarabu+ na wafalme wote wa jamii iliyochangamana wanaokaa nyikani;
25 na wafalme wote wa Zimri na wafalme wote wa Elamu+ na wafalme wote wa Wamedi;+
26 na wafalme wote wa kaskazini walio karibu na walio mbali, mmoja baada ya mwingine, na falme nyingine zote za dunia zilizo juu ya uso wa nchi; naye mfalme wa Sheshaki+ atakunywa baada yao.
27 “Nawe utawaambia, ‘Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, amesema hivi: “Kunyweni, mlewe, mtapike na kuanguka hivi kwamba msiweze kusimama+ kwa sababu ya upanga ninaotuma katikati yenu.”’+
28 Na iwe kwamba wakikataa kukichukua kikombe kutoka mkononi mwako ili wanywe, wewe pia utawaambia, ‘Yehova wa majeshi amesema hivi: “Bila shaka mtakinywa.+
29 Kwa maana, tazama! ninaanza kuleta msiba+ juu ya jiji ambalo linaitwa kwa jina langu, nanyi, je, mnapaswa kwa vyovyote kuachwa bila kuadhibiwa?”’+
“‘Hamtaachwa bila kuadhibiwa, kwa maana kuna upanga ambao ninaita juu ya wakaaji wote wa dunia,’ asema Yehova wa majeshi.
30 “Nawe utawatolea unabii kwa maneno haya yote, nawe utawaambia, ‘Yehova atanguruma kutoka juu,+ naye atatoa sauti yake kutoka katika makao yake matakatifu.+ Bila shaka atanguruma juu ya makao yake. Atapaaza sauti kama ile ya wale wanaokanyaga shinikizo la divai juu ya wakaaji wote wa dunia.’+
31 “‘Hakika kelele zitafika mpaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia, kwa maana Yehova ana ubishi na mataifa.+ Yeye binafsi atajiweka hukumuni na watu wote wenye mwili.+ Nao waovu atawatoa wauawe kwa upanga,’+ asema Yehova.
32 “Yehova wa majeshi amesema hivi, ‘Tazama! Msiba utaenda toka taifa mpaka taifa,+ na tufani kuu itaamshwa kutoka katika sehemu za mbali zaidi za dunia.+
33 Na wale waliouawa na Yehova siku hiyo hakika watakuwa kutoka mwisho mmoja wa dunia mpaka mwisho wa pili wa dunia.+ Hawataombolezewa, wala kukusanywa wala kuzikwa.+ Watakuwa kama mbolea juu ya uso wa nchi.’+
34 “Pigeni mayowe, ninyi wachungaji, na mpaaze kilio!+ Na mgaegae,+ ninyi watu mashuhuri wa kundi,+ kwa sababu siku za kuchinjwa kwenu na za kutawanywa kwenu zimetimia,+ nanyi mtaanguka kama chombo kinachotamanika!+
35 Na makimbilio yameangamia kwa wachungaji, na njia ya kuponyoka kwa watu mashuhuri wa kundi.+
36 Sikilizeni! Kilio cha wachungaji, na kupiga mayowe kwa watu mashuhuri wa kundi, kwa maana Yehova anapora malisho yao.
37 Na makao yenye amani yamefanywa kukosa uhai kwa sababu ya hasira ya Yehova inayowaka.+
38 Ametoka katika maficho yake kama mwana-simba mwenye manyoya shingoni,+ kwa maana nchi yao imekuwa kitu cha kushangaza kwa sababu ya upanga unaoonea na kwa sababu ya hasira yake inayowaka.”+