Yeremia 24:1-10
24 Na Yehova akanionyesha, na, tazama! vikapu viwili vya tini vilivyowekwa mbele ya hekalu la Yehova, baada ya Nebukadreza mfalme wa Babiloni kumpeleka uhamishoni Yekonia+ mwana wa Yehoyakimu,+ mfalme wa Yuda, na wakuu wa Yuda na mafundi+ na wajenzi wa maboma, kutoka Yerusalemu ili awalete Babiloni.+
2 Nacho kikapu kimoja, tini zilikuwa nzuri sana, kama tini za mapema;+ nacho kile kikapu cha pili, tini zilikuwa mbaya sana, hivi kwamba hazingeweza kuliwa kwa sababu ya ubaya.
3 Kisha Yehova akaniambia: “Unaona nini, Yeremia?” Basi nikasema: “Tini, zile tini nzuri zikiwa nzuri sana, na zile mbaya zikiwa mbaya sana, hivi kwamba haziwezi kuliwa kwa sababu ya ubaya.”+
4 Ndipo neno la Yehova likanijia, na kusema:
5 “Yehova Mungu wa Israeli amesema hivi, ‘Kama hizi tini nzuri, ndivyo nitakavyowaona kwa njia nzuri+ wale wahamishwa wa Yuda, ambao nitawapeleka kutoka mahali hapa mpaka katika nchi ya Wakaldayo.+
6 Nami nitaweka jicho langu juu yao kwa njia nzuri,+ na hakika mimi nitawarudisha katika nchi hii.+ Nami nitawajenga, wala sitawabomoa; nami nitawapanda, wala sitawang’oa.+
7 Nami nitawapa moyo wa kunijua,+ kwamba mimi ni Yehova; nao watakuwa watu wangu,+ nami nitakuwa Mungu wao, kwa maana watarudi kwangu kwa moyo wao wote.+
8 “‘Na kama zile tini mbaya ambazo haziwezi kuliwa kwa sababu ya ubaya,+ kwa kweli Yehova amesema hivi: “Ndivyo nitakavyomtoa Sedekia+ mfalme wa Yuda na wakuu wake na mabaki wa Yerusalemu wanaobaki katika nchi hii+ na wale wanaokaa katika nchi ya Misri+—
9 mimi pia nitawatoa kwa ajili ya kutetemesha, kwa ajili ya msiba, katika falme zote za dunia,+ kwa ajili ya shutuma na kwa ajili ya neno la kimethali, kwa ajili ya suto+ na kwa ajili ya laana,+ katika mahali pote nitakapowatawanya.+
10 Nami nitatuma juu yao upanga,+ njaa+ na tauni,+ mpaka waufikie mwisho wao kutoka katika nchi niliyowapa wao na mababu zao.”’”+