Yeremia 23:1-40

23  “Ole wao wachungaji wanaowaangamiza na kuwatawanya kondoo wa malisho yangu!”+ asema Yehova.  Kwa hiyo Yehova Mungu wa Israeli amesema hivi juu ya wachungaji wanaowachunga watu wangu: “Ninyi mmewatawanya kondoo zangu; nanyi mliendelea kuwatawanya, nanyi hamkuwakazia fikira zenu.”+ “Tazama, ninakaza fikira zangu juu yenu kwa sababu ya ubaya wa matendo yenu,”+ asema Yehova.  “Nami nitakusanya mabaki ya kondoo zangu kutoka katika nchi zote ambako nilikuwa nimewatawanya,+ nami nitawarudisha kwenye uwanja wao wa malisho,+ na hakika wao watazaa na kuwa wengi.+  Nami nitasimamisha juu yao wachungaji ambao kweli watawachunga;+ nao hawataogopa tena, wala hawataingiwa na hofu yoyote,+ na hakuna hata mmoja atakayekosekana,” asema Yehova.  “Tazama! Siku zinakuja,” asema Yehova, “nami nitamsimamishia Daudi chipukizi adilifu.+ Na hakika mfalme atatawala+ na kutenda kwa busara na kutenda haki na uadilifu katika nchi.+  Katika siku zake Yuda ataokolewa,+ na Israeli atakaa katika usalama.+ Na hili ndilo jina lake atakaloitwa, Yehova Ni Uadilifu Wetu.”+  “Kwa hiyo, tazama! siku zinakuja,” asema Yehova, “nao hawatasema tena, ‘Yehova yuko hai aliyewaleta wana wa Israeli kutoka katika nchi ya Misri,’+  bali, ‘Yehova yuko hai aliyepandisha na aliyeingiza uzao wa nyumba ya Israeli kutoka katika nchi ya kaskazini na kutoka katika nchi zote ambako nimewatawanya,’ na hakika wao watakaa katika nchi yao wenyewe.”+  Nao manabii, moyo wangu umevunjika ndani yangu. Mifupa yangu yote imeanza kutetemeka. Nimekuwa kama mtu ambaye amelewa,+ na kama mwanamume ambaye divai imemlemea, kwa sababu ya Yehova na kwa sababu ya maneno yake matakatifu. 10  Kwa maana nchi imejaa+ wazinzi.+ Kwa maana nchi inaomboleza+ kwa sababu ya laana, viwanja vya malisho vya nyika vimekauka;+ na mwenendo wao ni mbaya, na nguvu zao si kwa njia ya haki. 11  “Kwa maana nabii pamoja na kuhani wametiwa unajisi.+ Pia katika nyumba yangu mwenyewe nimeupata ubaya wao,”+ asema Yehova. 12  “Kwa hiyo njia yao itakuwa kwao kama mahali penye utelezi+ gizani, ambapo watasukumwa ndani yake na hakika waanguke.”+ “Kwa maana nitaleta msiba juu yao, mwaka wa kuwakazia fikira,”+ asema Yehova. 13  “Na katika manabii wa Samaria+ mimi nimeona jambo lisilofaa. Wametenda kama manabii waliochochewa na Baali,+ nao wanaendelea kuwafanya watu wangu, Israeli, waende huku na huku.+ 14  Na katika manabii wa Yerusalemu nimeona mambo yenye kuchukiza sana,+ kufanya uzinzi+ na kutembea katika uwongo;+ nao wameitia nguvu mikono ya watenda-maovu ili wasirudi,+ kila mmoja kutoka katika ubaya wake. Kwangu wote wamekuwa kama Sodoma,+ na wakaaji wake kama Gomora.”+ 15  Kwa hiyo Yehova wa majeshi amesema hivi juu ya manabii: “Tazama, ninawalisha pakanga, nami nitawapa maji yaliyotiwa sumu wanywe.+ Kwa maana kutoka kwa manabii wa Yerusalemu uasi-imani+ umeenea katika nchi yote.” 16  Yehova wa majeshi amesema hivi: “Msiyasikilize maneno ya manabii wanaowatolea ninyi unabii.+ Wanawafanya muwe ubatili.+ Wanasema maono ya moyo wao wenyewe+—si kutoka katika kinywa cha Yehova.+ 17  Wanawaambia tena na tena wale ambao hawaniheshimu, ‘Yehova amesema: “Ninyi mtakuwa na amani.”’+ Nao wamemwambia kila mtu anayetembea katika ukaidi wa moyo wake,+ ‘Hamtapatwa na msiba wowote.’+ 18  Kwa maana ni nani amesimama katika kikundi cha rafiki+ za Yehova ili aone na kulisikia neno lake?+ Ni nani amelikazia fikira neno lake ili alisikie?+ 19  Tazama! Dhoruba ya Yehova, ghadhabu, hakika itatoka, tufani inayozunguka.+ Itajizungusha juu ya kichwa cha waovu.+ 20  Hasira ya Yehova haitarudi nyuma mpaka atakapokuwa ametenda+ na mpaka atakapokuwa ametimiza mawazo ya moyo wake.+ Katika siku za mwisho ninyi mtalifikiria jambo hilo kwa uelewaji.+ 21  “Sikuwatuma manabii, ingawa wao wenyewe walikimbia. Sikusema nao, ingawa wao wenyewe walitoa unabii.+ 22  Lakini ikiwa wangekuwa wamesimama katika kikundi changu cha rafiki,+ ndipo wangewafanya watu wangu wayasikie maneno yangu, nao wangewarudisha kutoka katika njia yao mbaya na kutoka katika ubaya wa matendo yao.”+ 23  “Je, mimi ni Mungu aliye karibu,” asema Yehova, “na si Mungu aliye mbali?”+ 24  “Au, je, mtu yeyote anaweza kujificha katika maficho nami nisimwone?”+ asema Yehova. “Je, mimi kwa kweli sizijazi mbingu na dunia?”+ asema Yehova. 25  “Nimesikia yale ambayo manabii wanaotoa unabii wa uwongo katika jina langu+ wamesema, ‘Nimeota ndoto! Nimeota ndoto!’+ 26  Itadumu mpaka wakati gani katika moyo wa manabii wanaotoa unabii wa uwongo na ambao ni manabii wa udanganyifu wa moyo wao wenyewe?+ 27  Wanafikiria kuwafanya watu wangu walisahau jina langu kwa njia ya ndoto zao ambazo wanaendelea kusimuliana,+ kama baba zao walivyolisahau jina langu kwa sababu ya Baali.+ 28  Nabii ambaye ana ndoto, na asimulie ndoto hiyo; lakini yule ambaye ana neno langu, na aliseme neno langu kwa ukweli.”+ “Nyasi ina uhusiano gani na nafaka?”+ asema Yehova. 29  “Je, neno langu halilingani na moto,”+ asema Yehova, “na kama nyundo ya chuma ambayo huvunja mwamba?”+ 30  “Kwa hiyo tazama, mimi niko dhidi ya manabii,”+ asema Yehova, “wale wanaoyaiba maneno yangu, kila mmoja kutoka kwa mwenzake.”+ 31  “Tazama, mimi niko dhidi ya manabii,” asema Yehova, “wale wanaotumia ulimi wao ili kusema, ‘Neno!’”+ 32  “Tazama, mimi niko dhidi ya manabii wa ndoto za uwongo,” asema Yehova, “wale wanaozisimulia na kuwafanya watu wangu kwenda huku na huku kwa sababu ya uwongo+ wao na kwa sababu ya kujisifu+ kwao.” “Lakini mimi mwenyewe sikuwatuma wala kuwaamuru. Kwa hiyo hawatawafaidi watu hawa kwa vyovyote,”+ asema Yehova. 33  “Na watu hawa au nabii au kuhani wanapokuuliza, wakisema, ‘Mzigo wa Yehova ni nini?’+ wewe pia utawaambia, ‘ “Ninyi—Lo! jinsi mlivyo mzigo!+ Nami nitawaacha ninyi,”+ asema Yehova.’ 34  Naye nabii au kuhani au watu wanaosema, ‘Mzigo wa Yehova!’ Mimi pia nitakaza fikira zangu juu ya mtu huyo na juu ya nyumba yake.+ 35  Hivi ndivyo mnavyoendelea kuambiana mtu na mwenzake na mtu na ndugu yake, ‘Yehova ametoa jibu gani? Na Yehova amesema nini?’+ 36  Lakini msiutaje tena+ mzigo+ wa Yehova, kwa maana kwa kila mmoja mzigo unakuwa ni neno lake mwenyewe,+ nanyi mmeyabadili maneno ya Mungu aliye hai,+ Yehova wa majeshi, Mungu wetu. 37  “Utamwambia huyo nabii hivi, ‘Yehova amekupa jibu gani? Na Yehova amesema nini?+ 38  Na ikiwa mnaendelea kusema, “Mzigo wa Yehova!” basi Yehova amesema hivi: “Kwa sababu mnasema, ‘Hili neno ndilo mzigo wa Yehova,’ nilipoendelea kumtuma mtu kwenu, na kusema, ‘Msiseme: “Mzigo wa Yehova!”’ 39  kwa hiyo mimi hapa! Nami nitawapuuza ninyi, kabisa,+ nami nitawatupa pamoja na lile jiji nililowapa ninyi na mababu zenu—kutoka mbele zangu.+ 40  Nami nitatia juu yenu shutuma mpaka wakati usio na kipimo na fedheha mpaka wakati usio na kipimo, ambayo haitasahauliwa.”’”+

Maelezo ya Chini