Yeremia 18:1-23
18 Neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Yehova, likisema:
2 “Simama, ushuke mpaka nyumba ya mfinyanzi,+ na hapo nitakufanya usikie maneno yangu.”
3 Nami nikashuka mpaka nyumba ya mfinyanzi, na, tazama, alikuwa akifanya kazi juu ya magurudumu ya mfinyanzi.
4 Na chombo alichokuwa akitengeneza kwa udongo wa mfinyanzi kikaharibika mkononi mwa mfinyanzi, naye akageuka na kukifanya kuwa chombo kingine, kama ilivyokuwa sawa machoni pa mfinyanzi.+
5 Na neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema:
6 “‘Je, mimi siwezi kuwatendea kama mfinyanzi huyu alivyotenda, enyi nyumba ya Israeli?’ asema Yehova. ‘Tazama! Kama udongo mkononi mwa mfinyanzi, ndivyo ninyi mlivyo mkononi mwangu, enyi nyumba ya Israeli.+
7 Wakati wowote nikisema juu ya taifa na juu ya ufalme ili kuung’oa na kuubomoa na kuuharibu,+
8 na kwa kweli taifa lile ligeuke kutoka katika ubaya wake ambao nilisema juu yake,+ mimi pia nitajuta juu ya ule msiba niliokuwa nimefikiria kuutimiza juu yake.+
9 Lakini wakati wowote ambao huenda nikasema kuhusu taifa na kuhusu ufalme, kuujenga na kuupanda,+
10 nao kwa kweli ufanye mabaya machoni pangu kwa kutoitii sauti yangu,+ mimi pia nitajuta kwa yale mema ambayo nilisema moyoni mwangu kuwa nitafanya kwa faida yake.’
11 “Na sasa, tafadhali, waambie watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu, ‘Yehova amesema hivi: “Tazama, ninafanya msiba juu yenu na kutafakari wazo fulani juu yenu.+ Geukeni, tafadhali, kila mmoja kutoka katika njia yake mbaya, na mfanye njia zenu na matendo yenu kuwa mema.”’”+
12 Nao wakasema: “Hakuna tumaini!+ Kwa maana sisi tutafuata mawazo yetu wenyewe, nasi tutafanya kila mmoja ukaidi wa moyo wake mbaya.”+
13 Kwa hiyo Yehova amesema hivi: “Ulizeni wenyewe, tafadhali, kati ya mataifa. Ni nani amesikia mambo kama haya? Kuna jambo lenye kuchukiza sana ambalo bikira wa Israeli amefanya kupita kiasi.+
14 Je, theluji ya Lebanoni itatoka katika mwamba wa porini? Au, je, maji mageni, baridi, yanayotiririka, yatakaushwa?
15 Kwa maana watu wangu wamenisahau+ kwa kuwa wanakifukizia moshi wa dhabihu kitu cha ubatili,+ na kwa kuwa wanawakwaza watu katika njia zao,+ mapito ya zamani za kale,+ kutembea katika barabara, njia ambayo haijatengenezwa ikiwa na mafungu,
16 ili kuifanya nchi yao kuwa kitu cha kushangaza,+ kuwa ya kupigiwa mluzi mpaka wakati usio na kipimo.+ Kila mtu anayepita kando yake atatazama kwa mshangao na kutikisa kichwa chake.+
17 Nitawatawanya wao mbele ya adui kama kwa upepo wa mashariki.+ Nitawaonyesha wao mgongo, wala si uso,+ katika siku ya msiba wao.”
18 Nao wakasema: “Njooni, tutafakari juu ya Yeremia wazo fulani,+ kwa maana sheria haitaangamia kutoka kwa kuhani+ au shauri kutoka kwa mwenye hekima au neno kutoka kwa nabii.+ Njooni tumpige kwa ulimi,+ nasi tusisikilize lolote la maneno yake.”
19 Unitegee sikio, Ee Yehova, na kuisikiliza sauti ya wapinzani wangu.+
20 Je, ubaya unapaswa kulipwa badala ya wema?+ Kwa maana wameichimbia nafsi yangu shimo.+ Ukumbuke kusimama kwangu mbele zako ili kusema mema kuwahusu wao, ili kuigeuza ghadhabu yako iondoke kwao.+
21 Kwa hiyo uwatoe wana wao waone njaa,+ na kuwatoa wapatwe na nguvu za upanga;+ wake zao na wawe wanawake waliofiwa na watoto, na wajane.+ Wanaume wao na wauawe kwa tauni yenye kufisha, vijana wao na wapigwe na kuuawa kwa upanga vitani.+
22 Kilio na kisikiwe kutoka katika nyumba zao, utakapoleta juu yao kwa ghafula kikundi cha waporaji.+ Kwa maana wamechimba shimo ili kunikamata, nao wameficha mitego kwa ajili ya miguu yangu.+
23 Lakini wewe, Ee Yehova, unajua vema shauri lao lote juu yangu ili kuniua.+ Usilifunike kosa lao, wala usiifute ile dhambi yao kutoka mbele zako; bali wawe watu waliokwazwa mbele zako.+ Katika wakati wa hasira yako uwachukulie hatua.+