Yeremia 18:1-23

18  Neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Yehova, likisema:  “Simama, ushuke mpaka nyumba ya mfinyanzi,+ na hapo nitakufanya usikie maneno yangu.”  Nami nikashuka mpaka nyumba ya mfinyanzi, na, tazama, alikuwa akifanya kazi juu ya magurudumu ya mfinyanzi.  Na chombo alichokuwa akitengeneza kwa udongo wa mfinyanzi kikaharibika mkononi mwa mfinyanzi, naye akageuka na kukifanya kuwa chombo kingine, kama ilivyokuwa sawa machoni pa mfinyanzi.+  Na neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema:  “‘Je, mimi siwezi kuwatendea kama mfinyanzi huyu alivyotenda, enyi nyumba ya Israeli?’ asema Yehova. ‘Tazama! Kama udongo mkononi mwa mfinyanzi, ndivyo ninyi mlivyo mkononi mwangu, enyi nyumba ya Israeli.+  Wakati wowote nikisema juu ya taifa na juu ya ufalme ili kuung’oa na kuubomoa na kuuharibu,+  na kwa kweli taifa lile ligeuke kutoka katika ubaya wake ambao nilisema juu yake,+ mimi pia nitajuta juu ya ule msiba niliokuwa nimefikiria kuutimiza juu yake.+  Lakini wakati wowote ambao huenda nikasema kuhusu taifa na kuhusu ufalme, kuujenga na kuupanda,+ 10  nao kwa kweli ufanye mabaya machoni pangu kwa kutoitii sauti yangu,+ mimi pia nitajuta kwa yale mema ambayo nilisema moyoni mwangu kuwa nitafanya kwa faida yake.’ 11  “Na sasa, tafadhali, waambie watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu, ‘Yehova amesema hivi: “Tazama, ninafanya msiba juu yenu na kutafakari wazo fulani juu yenu.+ Geukeni, tafadhali, kila mmoja kutoka katika njia yake mbaya, na mfanye njia zenu na matendo yenu kuwa mema.”’”+ 12  Nao wakasema: “Hakuna tumaini!+ Kwa maana sisi tutafuata mawazo yetu wenyewe, nasi tutafanya kila mmoja ukaidi wa moyo wake mbaya.”+ 13  Kwa hiyo Yehova amesema hivi: “Ulizeni wenyewe, tafadhali, kati ya mataifa. Ni nani amesikia mambo kama haya? Kuna jambo lenye kuchukiza sana ambalo bikira wa Israeli amefanya kupita kiasi.+ 14  Je, theluji ya Lebanoni itatoka katika mwamba wa porini? Au, je, maji mageni, baridi, yanayotiririka, yatakaushwa? 15  Kwa maana watu wangu wamenisahau+ kwa kuwa wanakifukizia moshi wa dhabihu kitu cha ubatili,+ na kwa kuwa wanawakwaza watu katika njia zao,+ mapito ya zamani za kale,+ kutembea katika barabara, njia ambayo haijatengenezwa ikiwa na mafungu, 16  ili kuifanya nchi yao kuwa kitu cha kushangaza,+ kuwa ya kupigiwa mluzi mpaka wakati usio na kipimo.+ Kila mtu anayepita kando yake atatazama kwa mshangao na kutikisa kichwa chake.+ 17  Nitawatawanya wao mbele ya adui kama kwa upepo wa mashariki.+ Nitawaonyesha wao mgongo, wala si uso,+ katika siku ya msiba wao.” 18  Nao wakasema: “Njooni, tutafakari juu ya Yeremia wazo fulani,+ kwa maana sheria haitaangamia kutoka kwa kuhani+ au shauri kutoka kwa mwenye hekima au neno kutoka kwa nabii.+ Njooni tumpige kwa ulimi,+ nasi tusisikilize lolote la maneno yake.” 19  Unitegee sikio, Ee Yehova, na kuisikiliza sauti ya wapinzani wangu.+ 20  Je, ubaya unapaswa kulipwa badala ya wema?+ Kwa maana wameichimbia nafsi yangu shimo.+ Ukumbuke kusimama kwangu mbele zako ili kusema mema kuwahusu wao, ili kuigeuza ghadhabu yako iondoke kwao.+ 21  Kwa hiyo uwatoe wana wao waone njaa,+ na kuwatoa wapatwe na nguvu za upanga;+ wake zao na wawe wanawake waliofiwa na watoto, na wajane.+ Wanaume wao na wauawe kwa tauni yenye kufisha, vijana wao na wapigwe na kuuawa kwa upanga vitani.+ 22  Kilio na kisikiwe kutoka katika nyumba zao, utakapoleta juu yao kwa ghafula kikundi cha waporaji.+ Kwa maana wamechimba shimo ili kunikamata, nao wameficha mitego kwa ajili ya miguu yangu.+ 23  Lakini wewe, Ee Yehova, unajua vema shauri lao lote juu yangu ili kuniua.+ Usilifunike kosa lao, wala usiifute ile dhambi yao kutoka mbele zako; bali wawe watu waliokwazwa mbele zako.+ Katika wakati wa hasira yako uwachukulie hatua.+

Maelezo ya Chini