Yeremia 13:1-27

13  Yehova ameniambia hivi: “Nenda, ujipatie mshipi wa kitani uutie kiunoni mwako, lakini usiutie ndani ya maji yoyote.”  Basi nikauchukua mshipi kulingana na neno la Yehova, nikautia kiunoni mwangu.  Na neno la Yehova likanijia mara ya pili, na kusema:  “Uchukue ule mshipi uliopata, ulio kiunoni mwako, nawe usimame, uende Efrati,+ na kuuficha hapo katika mpasuko wa mwamba.”  Basi nikaenda, nikauficha kando ya Efrati, kama Yehova alivyoniamuru.  Lakini ikawa baada ya siku nyingi kwamba Yehova akaniambia: “Simama, nenda Efrati na kuchukua kutoka huko ule mshipi niliokuamuru uufiche huko.”  Basi nikaenda Efrati, nikachimba na kuuchukua ule mshipi kutoka mahali ambapo niliuficha, na, tazama! mshipi ulikuwa umeharibika; haukufaa kwa jambo lolote.  Ndipo neno la Yehova likanijia, na kusema:  “Yehova amesema hivi, ‘Ndivyo nitakavyokiharibu kiburi cha Yuda+ na kiburi kingi cha Yerusalemu. 10  Watu hawa wabaya wanaokataa kuyatii maneno yangu,+ wanaotembea katika ukaidi wa moyo+ wao na wanaoendelea kufuata miungu mingine ili kuitumikia na kuiinamia,+ pia watakuwa kama mshipi huu ambao haufai kwa jambo lolote.’ 11  ‘Kwa maana kama vile mshipi unavyoshikamana na kiuno cha mtu, ndivyo nilivyoifanya nyumba yote ya Israeli na nyumba yote ya Yuda kushikamana nami,’+ asema Yehova, ‘ili wawe kwangu kikundi cha watu+ na jina+ na sifa na kitu kizuri; lakini hawakutii.’+ 12  “Nawe uwaambie neno hili, ‘Yehova Mungu wa Israeli amesema hivi: “Kila mtungi mkubwa hujazwa divai.”’+ Nao hakika watakuambia, ‘Je, hatujui hakika kwamba kila mtungi mkubwa hujazwa divai?’ 13  Nawe uwaambie, ‘Yehova amesema hivi: “Tazama, ninawajaza ulevi wakaaji wote wa nchi hii na wafalme wanaoketi kwa ajili ya Daudi+ juu ya kiti chake cha ufalme na makuhani na manabii na wakaaji wote wa Yerusalemu.+ 14  Nami nitawagonganisha mmoja na mwingine, akina baba na wana, wakati uleule,”+ asema Yehova. “Sitaonyesha huruma, wala kuwa na majonzi, nami sitakuwa na rehema ya kujizuia kuwaharibu.”’+ 15  “Sikieni na mtege sikio. Msiwe na majivuno,+ kwa maana Yehova amesema.+ 16  Mpeni Yehova Mungu wenu utukufu,+ kabla hajaleta giza+ na kabla miguu yenu haijagongana juu ya milima wakati wa jioni.+ Nanyi hakika mtaitumaini nuru,+ naye kwa kweli ataifanya iwe kivuli kizito;+ ataigeuza iwe giza zito.+ 17  Lakini msiposikia jambo hilo,+ nafsi yangu italia na kutoa machozi katika mahali pa maficho kwa sababu ya kiburi nayo hakika itatoa machozi; na jicho langu litatiririka machozi,+ kwa sababu kundi+ la Yehova litakuwa limekwisha kuchukuliwa mateka. 18  “Mwambie mfalme na malkia,+ ‘Ketini mahali pa chini,+ kwa maana hakika taji lenu la urembo litashuka kutoka juu ya vichwa vyenu.’+ 19  Majiji ya kusini yamefungwa, hivi kwamba hakuna anayeyafungua. Yuda yote imepelekwa uhamishoni. Imepelekwa uhamishoni kabisa.+ 20  “Inua macho yako uone wale wanaokuja kutoka kaskazini.+ Liko wapi kundi ambalo ulipewa, kundi lako zuri?+ 21  Utasema nini wakati mtu anapokukazia fikira zake,+ wakati wewe umewafundisha kama rafiki zako kando yako tangu pale mwanzoni?+ Je, uchungu wa kuzaa hautakushika wewe, kama wa mwanamke anayezaa?+ 22  Na utakaposema moyoni mwako,+ ‘Kwa nini mambo haya yamenipata?’+ kwa sababu ya wingi wa makosa yako marinda yako yameondolewa yasiwe kifuniko;+ visigino vyako vimetendewa kijeuri. 23  “Je, Mkushi+ anaweza kuibadili ngozi yake? au, chui madoa yake?+ Ninyi pia mngeweza kufanya mema, watu waliofundishwa kutenda mabaya.+ 24  Basi nitawatawanya+ kama majani makavu yanayopita katika upepo kutoka nyikani.+ 25  Hii ndiyo kura yako, fungu lako lililopimwa kutoka kwangu,”+ asema Yehova, “kwa sababu umenisahau+ nawe unaendelea kuutegemea uwongo.+ 26  Nami pia nitainua marinda yako juu ya uso wako, na hakika aibu yako itaonwa,+ 27  matendo yako ya uzinzi+ na milio yako,+ mwenendo wako mpotovu katika ukahaba. Juu ya vilima, katika mashamba, nimeyaona machukizo yako.+ Ole wako, Ee Yerusalemu! Huwezi kuwa safi+—baada ya muda gani zaidi?”+

Maelezo ya Chini