Yeremia 11:1-23

11  Neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Yehova, likisema:  “Sikieni maneno ya agano hili! “Nawe uyaseme+ kwa watu wa Yuda na kwa wakaaji wa Yerusalemu,  nawe uwaambie, ‘Yehova Mungu wa Israeli amesema hivi: “Amelaaniwa mtu yule ambaye hayasikilizi maneno ya agano hili,+  ambayo niliwaamuru mababu zenu siku ile niliyowatoa katika nchi ya Misri,+ kutoka katika tanuru ya chuma,+ nikisema, ‘Tiini sauti yangu, nanyi mfanye mambo kulingana na yote ninayowaamuru;+ nanyi hakika mtakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wenu,+  kwa kusudi la kutimiza kiapo nilichowaapia mababu zenu,+ kuwapa nchi inayotiririka maziwa na asali,+ kama ilivyo leo hii.’”’” Nami nikajibu na kusema: “Amina, Ee Yehova.”  Na Yehova akaendelea kuniambia: “Tangaza maneno haya yote katika majiji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu,+ ukisema, ‘Sikieni maneno ya agano hili, nanyi lazima myafanye.+  Kwa maana niliwaonya mababu zenu siku ile niliyowatoa katika nchi ya Misri+ na mpaka leo hii, nikiamka mapema na kuwaonya, nikisema: “Tiini sauti yangu.”+  Lakini hawakusikiliza wala kutega sikio lao,+ bali wakaendelea kutembea kila mmoja katika ukaidi wa moyo wake mbaya;+ na kwa hiyo nikaleta juu yao maneno yote ya agano hili nililowaamuru kufanya, lakini hawakufanya.’”  Na zaidi, Yehova akaniambia: “Hila imepatikana kati ya watu wa Yuda na kati ya wakaaji wa Yerusalemu.+ 10  Wamerudi kwenye makosa ya mababu zao,+ wale wa kwanza, waliokataa kuyatii maneno yangu, lakini ambao wenyewe wameifuata miungu mingine ili kuitumikia.+ Nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda zimevunja agano langu nililofanya pamoja na mababu zao.+ 11  Kwa hiyo Yehova amesema hivi, ‘Tazama, ninaleta juu yao msiba+ ambao hawataweza kuondoka ndani yake;+ nao hakika wataniomba msaada, lakini sitawasikiliza.+ 12  Na majiji ya Yuda na wakaaji wa Yerusalemu wataenda na kuiomba msaada miungu ambayo wanaifukizia moshi wa dhabihu,+ lakini ambayo hakika haitawaletea wokovu wowote katika wakati wa msiba wao.+ 13  Kwa maana miungu yako imekuwa mingi kama majiji yako, Ee Yuda;+ nanyi mmeweka madhabahu nyingi kama barabara za Yerusalemu kwa ajili ya kile kitu cha aibu,+ madhabahu za kumfukizia Baali moshi wa dhabihu.’+ 14  “Nawe usisali kwa ajili ya watu hawa, wala usipaaze kilio cha kusihi wala sala kwa ajili yao,+ kwa maana sitawasikiliza wakati watakaponiomba kuhusu msiba wao.+ 15  “Mpendwa wangu ana kazi gani ndani ya nyumba yangu,+ hivi kwamba wengi wao wafanye jambo hili,+ hii mbinu ya uovu?+ Na kwa nyama takatifu, je, wao watafanya jambo hilo lipite kutoka juu yako,+ msiba wako utakapokuja? Je, wewe utafurahi wakati huo?+ 16  ‘Mzeituni wenye majani mengi, wenye kupendeza kwa kuwa na matunda na kwa umbo,’ ndivyo ambavyo Yehova amekuita jina lako.+ Kwa sauti ya mngurumo mkubwa, amewasha moto juu yake, nao wamevunja matawi yake.+ 17  “Na Yehova wa majeshi, Mpandaji wako,+ ametangaza msiba juu yako kwa sababu ya ubaya wa nyumba ya Israeli+ na nyumba ya Yuda ambao wametenda kwa upande wao ili kunitia uchungu kwa kumfukizia Baali moshi wa dhabihu.”+ 18  Na Yehova amenijulisha ili nijue. Wakati huo ulinionyesha matendo yao.+ 19  Nami nilikuwa kama mwana-kondoo dume, mtulivu, ambaye huletwa machinjioni,+ nami sikujua kwamba walipanga hila juu yangu:+ “Na tuuharibu mti pamoja na matunda yake, na tumkatilie mbali kutoka katika nchi ya walio hai,+ ili jina lake lisikumbukwe tena.” 20  Lakini Yehova wa majeshi anahukumu kwa uadilifu;+ anachunguza figo na moyo.+ Lo! acha nione kisasi chako juu yao, kwa maana ni kwako wewe nimeifunua kesi yangu.+ 21  Kwa hiyo Yehova amesema hivi juu ya watu wa Anathothi+ wanaoitafuta nafsi yako, wakisema: “Usitoe unabii katika jina la Yehova,+ usije ukafa mkononi mwetu”; 22  kwa hiyo Yehova wa majeshi amesema hivi: “Tazama, mimi ninakaza fikira zangu juu yao. Vijana watakufa kwa upanga.+ Wana wao na binti zao watakufa kwa njaa.+ 23  Nao hawatakuwa hata na mabaki, kwa sababu nitaleta msiba juu ya watu wa Anathothi,+ mwaka wa kuwakazia fikira.”+

Maelezo ya Chini