Yeremia 1:1-19

1  Maneno ya Yeremia+ mwana wa Hilkia, mmoja wa makuhani waliokuwa katika Anathothi+ katika nchi ya Benyamini;+  ambaye neno la Yehova lilimjia katika siku za Yosia+ mwana wa Amoni,+ mfalme wa Yuda, katika mwaka wa kumi na tatu wa utawala wake.+  Nalo likaendelea kuja katika siku za Yehoyakimu+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, mpaka kumalizika kwa mwaka wa kumi na moja wa Sedekia+ mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, mpaka Yerusalemu lilipoenda uhamishoni katika mwezi wa tano.+  Na neno la Yehova likaanza kunijia, na kusema:  “Kabla sijaanza kukuumba ndani ya tumbo+ nilikujua,+ na kabla hujatoka ndani ya tumbo la uzazi nilikutakasa.+ Nilikufanya uwe nabii kwa mataifa.”  Lakini nikasema: “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova! Tazama, mimi hakika sijui jinsi ya kusema,+ kwa sababu mimi ni mvulana tu.”+  Na Yehova akaendelea kuniambia: “Usiseme, ‘Mimi ni mvulana tu.’ Lakini kwa wale wote nitakaokutuma kwao, unapaswa kwenda; na kila jambo nitakalokuamuru, unapaswa kusema.+  Usiogope kwa sababu ya nyuso zao,+ kwa maana ‘mimi niko pamoja nawe ili kukukomboa,’+ asema Yehova.”  Basi Yehova akanyoosha mkono wake na kunigusa kinywa+ changu. Ndipo Yehova akaniambia: “Tazama, nimeyatia maneno yangu katika kinywa chako.+ 10  Tazama, nimekupa utume leo ili uwe juu ya mataifa na juu ya falme,+ ili kung’oa na kubomoa na kuangamiza na kuangusha,+ ili kujenga na kupanda.”+ 11  Na neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: “Unaona nini, Yeremia?” Basi nikasema: “Ninaona chipukizi la mlozi.” 12  Na Yehova akaendelea kuniambia: “Umeona vema, kwa maana niko macho kuhusu neno langu ili kulitimiza.”+ 13  Na neno la Yehova likanijia mara ya pili, na kusema: “Unaona nini?” Basi nikasema: “Ninaona chungu cha kupikia chenye mdomo mpana ambacho kinapuliziwa, na mdomo wake umeinama kutoka kaskazini.” 14  Ndipo Yehova akaniambia: “Msiba utafunguliwa kutoka kaskazini juu ya wakaaji wote wa nchi.+ 15  Kwa maana ‘tazama, ninaziita familia zote za falme za kaskazini,’ asema Yehova;+ ‘nao hakika watakuja na kuweka kila mmoja kiti chake cha ufalme kwenye mwingilio wa malango ya Yerusalemu,+ na juu ya kuta zake zote kuzunguka pande zote na juu ya majiji yote ya Yuda.+ 16  Nami nitasema nao hukumu zangu juu ya ubaya wao wote,+ kwa kuwa wameniacha+ nao wanaendelea kufukizia miungu mingine+ moshi wa dhabihu na kuinamia kazi za mikono yao wenyewe.’+ 17  “Nawe unapaswa kufunga mshipi viunoni mwako,+ na kusimama na kuwaambia kila jambo ambalo mimi ninakuamuru. Usiwe na hofu yoyote kwa sababu yao,+ ili mimi nisikutie hofu mbele yao. 18  Lakini mimi, tazama, leo nimekufanya wewe kuwa jiji lenye ngome na nguzo ya chuma na kuta za shaba+ juu ya nchi yote,+ kuwaelekea wafalme wa Yuda, kuwaelekea wakuu wake, kuwaelekea makuhani wake na kuwaelekea watu wa nchi hii.+ 19  Nao hakika watapigana nawe, lakini hawatakushinda,+ kwa maana ‘Mimi niko pamoja nawe,’+ asema Yehova, ‘ili nikukomboe.’”+

Maelezo ya Chini