Wimbo wa Sulemani 7:1-13

7  “Jinsi hatua zako zimekuwa nzuri katika viatu vyako,+ ewe binti mwenye kujitoa kwa kupenda!+ Mikato ya mapaja yako ni kama mapambo,+ kazi ya mikono ya fundi.  Kitovu chako ni bakuli la mviringo. Divai iliyochanganywa+ isikosekane ndani yake. Tumbo lako ni rundo la ngano, lililozungushiwa ua wa mayungiyungi.+  Maziwa yako mawili ni kama watoto wawili, mapacha ya swala-jike.+  Shingo yako+ ni kama mnara wa pembe ya tembo. Macho yako+ ni kama vidimbwi katika Heshboni,+ kando ya lango la Bath-rabimu. Pua yako ni kama mnara wa Lebanoni, ambao unaelekea Damasko.  Kichwa chako juu yako ni kama Karmeli,+ na mashungi+ ya nywele za kichwa chako ni kama sufu iliyotiwa rangi ya zambarau.+ Mfalme amenaswa na mining’inio ya nywele zako.+  Jinsi ulivyo mrembo, na jinsi unavyopendeza, ewe msichana mpendwa, katikati ya furaha tele!+  Hiki kimo chako kinafanana na mtende,+ na maziwa yako+ kama vishada vya tende.  Nimesema, ‘Nitapanda juu ya mtende, nikamate vitawi vya matunda yake ya tende.’+ Tafadhali, maziwa yako na yawe kama vishada vya mzabibu, na harufu nzuri ya pua yako kama matofaa,  na kinywa chako kama divai bora+ zaidi ambayo inashuka kwa ulaini+ kwa ajili ya mpenzi wangu, ikitiririka taratibu juu ya midomo ya wenye kulala usingizi.” 10  “Mimi ni wa mpenzi wangu,+ na tamaa yake imenielekea mimi.+ 11  Njoo, ewe mpenzi wangu, twende shambani;+ tukae katikati ya mimea ya hina.+ 12  Na tuamke mapema, twende katika mashamba ya mizabibu, tuone kama mzabibu umechipuka,+ kama ua limechanuka,+ kama mikomamanga imechanua.+ Huko nitakupa wewe maonyesho yangu ya mapenzi.+ 13  Dudai+ zimetoa harufu yake nzuri, na kando ya maingilio yetu kuna namna zote za matunda bora kabisa.+ Mapya na ya zamani vilevile, ewe mpenzi wangu, nimekuwekea hazina.

Maelezo ya Chini