Wakolosai 1:1-29

1  Paulo, mtume wa Kristo Yesu kupitia mapenzi ya Mungu,+ na Timotheo+ ndugu yetu  kwa watakatifu na ndugu waaminifu katika muungano+ na Kristo walioko Kolosai: Na muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu.+  Sikuzote sisi humshukuru+ Mungu Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo tunaposali kwa ajili yenu,+  kwa kuwa tulisikia juu ya imani yenu kuhusiana na Kristo Yesu na upendo mlio nao kwa watakatifu wote+  kwa sababu ya tumaini+ ambalo linawekwa akiba kwa ajili yenu mbinguni.+ Tumaini hili mlilisikia hapo mbele kupitia kutangazwa kwa ile kweli ya habari njema+  ambayo imejitokeza kwenu, kama inavyozaa matunda+ na kuongezeka+ katika ulimwengu+ wote kama vile inavyofanya pia katikati yenu, tangu siku mliposikia na kujua kwa usahihi fadhili zisizostahiliwa+ za Mungu katika kweli.+  Hivyo ndivyo mmejifunza kutoka kwa Epafra+ mtumwa mwenzetu mpendwa, aliye mhudumu mwaminifu wa Kristo kwa ajili yetu,  ambaye pia alitufunulia upendo+ wenu katika njia ya kiroho.  Hiyo ndiyo sababu sisi pia, tangu siku tuliposikia juu ya jambo hilo, hatujaacha kusali kwa ajili yenu+ na kuomba kwamba mjazwe ujuzi sahihi+ wa mapenzi yake katika hekima+ yote na utambuzi wa kiroho,+ 10  ili mtembee kwa kumstahili+ Yehova+ kwa kusudi la kumpendeza yeye kikamili mnapoendelea kuzaa matunda katika kila kazi njema+ na kuongezeka katika ujuzi sahihi+ wa Mungu, 11  mkifanywa kuwa na nguvu kwa nguvu zote kwa kadiri ya uwezo wake wenye utukufu+ ili kuvumilia+ kikamili na kuwa wenye ustahimilivu pamoja na shangwe, 12  mkimshukuru Baba aliyewafanya ninyi mfae kushiriki urithi+ wa watakatifu+ katika nuru.+ 13  Yeye alitukomboa kutoka katika mamlaka+ ya giza, akatuhamisha+ na kutuingiza katika ufalme+ wa Mwana wa upendo wake,+ 14  ambaye kwa njia yake tunaachiliwa huru kupitia fidia, kusamehewa dhambi zetu.+ 15  Yeye ndiye mfano+ wa Mungu asiyeonekana,+ mzaliwa wa kwanza+ wa viumbe vyote; 16  kwa sababu kwa njia yake+ vitu vingine vyote viliumbwa mbinguni na duniani, vitu vinavyoonekana na vitu visivyoonekana, hata viwe ni viti vya ufalme au utawala au serikali au mamlaka.+ Vitu vingine vyote vimeumbwa kupitia yeye+ na kwa ajili yake. 17  Pia, yeye ni wa kabla ya vitu vingine vyote+ na kwa njia yake vitu vingine vyote vilifanywa kuwapo,+ 18  naye ndiye kichwa cha mwili, kutaniko.+ Yeye ndiye mwanzo, mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu,+ ili yeye awe ndiye wa kwanza+ katika vitu vyote; 19  kwa sababu Mungu aliona ni vema ujazo+ wote ukae katika yeye, 20  na kupitia yeye apatanishe+ tena kwake mwenyewe vitu vingine vyote+ kwa kufanya amani+ kupitia damu+ aliyomwaga juu ya mti wa mateso,+ hata kama ni vitu vilivyo duniani au vitu vilivyo mbinguni. 21  Kwa kweli, ninyi ambao hapo zamani mlikuwa mmetengwa,+ nanyi mlikuwa adui kwa sababu akili zenu zilikuwa zimekazwa juu ya matendo maovu,+ 22  yeye sasa amewapatanisha+ tena kwa njia ya mwili wenye nyama wa huyo kupitia kifo chake,+ ili awatoe ninyi mkiwa watakatifu na wasio na dosari+ na bila shtaka+ lolote mbele zake, 23  bora tu, bila shaka, mwendelee katika imani,+ mkiwekwa imara juu ya msingi+ na mkiwa thabiti+ na bila kuondoshwa kwenye tumaini la ile habari njema mliyoisikia,+ na ambayo ilihubiriwa+ katika uumbaji wote+ ulio chini ya mbingu. Mimi Paulo, nilikuja kuwa mhudumu wa hii habari njema.+ 24  Ninashangilia sasa katika mateso yangu kwa ajili yenu,+ nami, kwa upande wangu, ninajazia kinachopungua cha dhiki+ za Kristo katika mwili wangu kwa ajili ya mwili wake, ambao ni kutaniko.+ 25  Mimi nilikuja kuwa mhudumu+ wa kutaniko hili kwa kupatana na usimamizi-nyumba+ kutoka kwa Mungu niliopewa kwa faida yenu ili kulihubiri neno la Mungu kwa ukamili, 26  siri takatifu+ iliyokuwa imefichwa tangu mifumo ya mambo+ iliyopita na tangu vizazi vilivyopita. Lakini sasa imefunuliwa+ kwa watakatifu wake, 27  ambao Mungu amependezwa kuwajulisha ule utajiri wenye utukufu+ wa hii siri takatifu+ katikati ya mataifa. Ni Kristo+ katika muungano na ninyi, tumaini la utukufu wake.+ 28  Yeye ndiye tunayemtangaza,+ tukimwonya kila mtu na kumfundisha kila mtu katika hekima yote,+ ili tumtoe kila mtu akiwa kamili+ katika muungano na Kristo. 29  Kwa kusudi hili kwa kweli ninafanya kazi kwa bidii, nikijikaza+ kulingana na utendaji+ wake na ambao unafanya kazi ndani yangu kwa nguvu.+

Maelezo ya Chini