Wakolosai 1:1-29
1 Paulo, mtume wa Kristo Yesu kupitia mapenzi ya Mungu,+ na Timotheo+ ndugu yetu
2 kwa watakatifu na ndugu waaminifu katika muungano+ na Kristo walioko Kolosai:
Na muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu.+
3 Sikuzote sisi humshukuru+ Mungu Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo tunaposali kwa ajili yenu,+
4 kwa kuwa tulisikia juu ya imani yenu kuhusiana na Kristo Yesu na upendo mlio nao kwa watakatifu wote+
5 kwa sababu ya tumaini+ ambalo linawekwa akiba kwa ajili yenu mbinguni.+ Tumaini hili mlilisikia hapo mbele kupitia kutangazwa kwa ile kweli ya habari njema+
6 ambayo imejitokeza kwenu, kama inavyozaa matunda+ na kuongezeka+ katika ulimwengu+ wote kama vile inavyofanya pia katikati yenu, tangu siku mliposikia na kujua kwa usahihi fadhili zisizostahiliwa+ za Mungu katika kweli.+
7 Hivyo ndivyo mmejifunza kutoka kwa Epafra+ mtumwa mwenzetu mpendwa, aliye mhudumu mwaminifu wa Kristo kwa ajili yetu,
8 ambaye pia alitufunulia upendo+ wenu katika njia ya kiroho.
9 Hiyo ndiyo sababu sisi pia, tangu siku tuliposikia juu ya jambo hilo, hatujaacha kusali kwa ajili yenu+ na kuomba kwamba mjazwe ujuzi sahihi+ wa mapenzi yake katika hekima+ yote na utambuzi wa kiroho,+
10 ili mtembee kwa kumstahili+ Yehova+ kwa kusudi la kumpendeza yeye kikamili mnapoendelea kuzaa matunda katika kila kazi njema+ na kuongezeka katika ujuzi sahihi+ wa Mungu,
11 mkifanywa kuwa na nguvu kwa nguvu zote kwa kadiri ya uwezo wake wenye utukufu+ ili kuvumilia+ kikamili na kuwa wenye ustahimilivu pamoja na shangwe,
12 mkimshukuru Baba aliyewafanya ninyi mfae kushiriki urithi+ wa watakatifu+ katika nuru.+
13 Yeye alitukomboa kutoka katika mamlaka+ ya giza, akatuhamisha+ na kutuingiza katika ufalme+ wa Mwana wa upendo wake,+
14 ambaye kwa njia yake tunaachiliwa huru kupitia fidia, kusamehewa dhambi zetu.+
15 Yeye ndiye mfano+ wa Mungu asiyeonekana,+ mzaliwa wa kwanza+ wa viumbe vyote;
16 kwa sababu kwa njia yake+ vitu vingine vyote viliumbwa mbinguni na duniani, vitu vinavyoonekana na vitu visivyoonekana, hata viwe ni viti vya ufalme au utawala au serikali au mamlaka.+ Vitu vingine vyote vimeumbwa kupitia yeye+ na kwa ajili yake.
17 Pia, yeye ni wa kabla ya vitu vingine vyote+ na kwa njia yake vitu vingine vyote vilifanywa kuwapo,+
18 naye ndiye kichwa cha mwili, kutaniko.+ Yeye ndiye mwanzo, mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu,+ ili yeye awe ndiye wa kwanza+ katika vitu vyote;
19 kwa sababu Mungu aliona ni vema ujazo+ wote ukae katika yeye,
20 na kupitia yeye apatanishe+ tena kwake mwenyewe vitu vingine vyote+ kwa kufanya amani+ kupitia damu+ aliyomwaga juu ya mti wa mateso,+ hata kama ni vitu vilivyo duniani au vitu vilivyo mbinguni.
21 Kwa kweli, ninyi ambao hapo zamani mlikuwa mmetengwa,+ nanyi mlikuwa adui kwa sababu akili zenu zilikuwa zimekazwa juu ya matendo maovu,+
22 yeye sasa amewapatanisha+ tena kwa njia ya mwili wenye nyama wa huyo kupitia kifo chake,+ ili awatoe ninyi mkiwa watakatifu na wasio na dosari+ na bila shtaka+ lolote mbele zake,
23 bora tu, bila shaka, mwendelee katika imani,+ mkiwekwa imara juu ya msingi+ na mkiwa thabiti+ na bila kuondoshwa kwenye tumaini la ile habari njema mliyoisikia,+ na ambayo ilihubiriwa+ katika uumbaji wote+ ulio chini ya mbingu. Mimi Paulo, nilikuja kuwa mhudumu wa hii habari njema.+
24 Ninashangilia sasa katika mateso yangu kwa ajili yenu,+ nami, kwa upande wangu, ninajazia kinachopungua cha dhiki+ za Kristo katika mwili wangu kwa ajili ya mwili wake, ambao ni kutaniko.+
25 Mimi nilikuja kuwa mhudumu+ wa kutaniko hili kwa kupatana na usimamizi-nyumba+ kutoka kwa Mungu niliopewa kwa faida yenu ili kulihubiri neno la Mungu kwa ukamili,
26 siri takatifu+ iliyokuwa imefichwa tangu mifumo ya mambo+ iliyopita na tangu vizazi vilivyopita. Lakini sasa imefunuliwa+ kwa watakatifu wake,
27 ambao Mungu amependezwa kuwajulisha ule utajiri wenye utukufu+ wa hii siri takatifu+ katikati ya mataifa. Ni Kristo+ katika muungano na ninyi, tumaini la utukufu wake.+
28 Yeye ndiye tunayemtangaza,+ tukimwonya kila mtu na kumfundisha kila mtu katika hekima yote,+ ili tumtoe kila mtu akiwa kamili+ katika muungano na Kristo.
29 Kwa kusudi hili kwa kweli ninafanya kazi kwa bidii, nikijikaza+ kulingana na utendaji+ wake na ambao unafanya kazi ndani yangu kwa nguvu.+