Waefeso 3:1-21
3 Kwa hiyo mimi, Paulo, mfungwa+ wa Kristo Yesu kwa ajili yenu, watu wa mataifa+—
2 ikiwa, kwa kweli, mmesikia juu ya usimamizi-nyumba+ wa fadhili zisizostahiliwa za Mungu ambao nilipewa kwa ajili yenu,
3 kwamba nilijulishwa siri takatifu kwa njia ya ufunuo,+ kama vile nilivyoandika kwa ufupi hapo mwanzoni.
4 Kwa kufikiria haya, mnapoisoma hii, mnaweza kuona utambuzi+ nilio nao katika siri takatifu+ ya Kristo.
5 Katika vizazi vingine siri hii+ haikujulishwa kwa wana wa binadamu kama vile ambavyo imefunuliwa+ sasa kwa mitume wake watakatifu na manabii+ kupitia roho,
6 yaani, kwamba watu wa mataifa wawe warithi wa pamoja na viungo vyenzi vya mwili+ na washiriki pamoja nasi wa ahadi+ katika muungano na Kristo Yesu kupitia habari njema.
7 Mimi nilikuja kuwa mhudumu+ wa hilo kulingana na zawadi ya bure ya fadhili zisizostahiliwa za Mungu nilizopewa kulingana na njia ambayo nguvu zake hutenda.+
8 Mimi, niliye mtu mdogo kuliko aliye mdogo+ zaidi kati ya watakatifu wote, nilipewa fadhili hizi zisizostahiliwa,+ ili niwatangazie mataifa+ habari njema juu ya utajiri+ usiopimika wa Kristo
9 na kufanya watu waone jinsi siri takatifu+ inavyosimamiwa+ ambayo tangu wakati uliopita usio na kipimo imefichwa katika Mungu, aliyeviumba vitu vyote.+
10 Hiyo ilikuwa kwa kusudi kwamba sasa serikali na mamlaka+ zilizo katika mahali pa kimbingu zijulishwe kupitia kutaniko+ hekima ya Mungu ya namna nyingi sana,+
11 kulingana na kusudi la milele alilofanyiza kuhusiana na Kristo,+ Yesu Bwana wetu,
12 ambaye kwa njia yake tuna uhuru huu wa kusema na tuna uwezo wa kukaribia+ tukiwa na uhakika kupitia imani yetu katika yeye.
13 Kwa hiyo nawaomba ninyi msife moyo kwa sababu ya hizi dhiki+ zangu kwa ajili yenu, kwa maana hizi zinamaanisha utukufu kwenu.
14 Kwa sababu hiyo nampigia Baba magoti,+
15 ambaye kila familia+ mbinguni na duniani hupata jina kutokana naye,+
16 kwa kusudi la kwamba awawezeshe ninyi kulingana na utajiri+ wa utukufu wake mfanywe kuwa na uwezo katika mtu mliye kwa ndani+ mkiwa na nguvu kupitia roho yake,+
17 ili muwe na Kristo akikaa kupitia imani yenu katika mioyo yenu kwa upendo;+ ili mtie mizizi+ na kuimarishwa juu ya ule msingi,+
18 ili mweze kufahamu kabisa akilini+ pamoja na watakatifu wote, upana na urefu na kimo na kina,+
19 na kuujua upendo wa Kristo+ ambao unazidi ujuzi, ili mjawe na ujazo+ wote ambao Mungu hutoa.
20 Basi kwa yeye anayeweza, kulingana na nguvu zake zinazotenda+ ndani yetu, kufanya kwa wingi zaidi kupita mambo yote tunayoomba au tunayofikiri,+
21 kwake kuwe na utukufu kwa njia ya kutaniko na kwa njia ya Kristo Yesu kwa vizazi vyote milele na milele.+ Amina.

