Ufunuo 6:1-17
6 Naye Mwana-Kondoo+ alipofungua mmoja wa ile mihuri saba,+ nikaona, na kumsikia mmoja wa wale viumbe hai+ wanne akisema kwa sauti kama ya ngurumo: “Njoo!”+
2 Nami nikaona, na, tazama! farasi mweupe;+ na yule anayeketi+ juu yake alikuwa na upinde;+ naye akapewa taji,+ naye akaenda akishinda+ na kukamilisha ushindi wake.+
3 Naye alipofungua muhuri wa pili, nikamsikia kiumbe hai wa pili+ akisema: “Njoo!”
4 Na mwingine akatokea, farasi mwenye rangi ya moto; na yeye anayeketi juu yake akapewa ruhusa ya kuondoa amani duniani ili wauane; naye akapewa upanga mkubwa.+
5 Naye+ alipofungua muhuri wa tatu, nikamsikia kiumbe hai wa tatu+ akisema: “Njoo!” Nami nikaona, na, tazama! farasi mweusi; na yeye anayeketi juu yake alikuwa na mizani+ mkononi mwake.
6 Nami nikasikia sauti kana kwamba ni katikati+ ya wale viumbe hai wanne+ ikisema: “Kibaba cha ngano kwa dinari+ moja, na vibaba vitatu vya shayiri kwa dinari moja; wala usidhuru mafuta ya zeituni na divai.”+
7 Naye alipofungua muhuri wa nne, nikasikia sauti ya kiumbe hai wa nne+ akisema: “Njoo!”
8 Nami nikaona, na, tazama! farasi wa rangi ya kijivu; na yeye anayeketi juu yake alikuwa na jina Kifo. Na Kaburi*+ lilikuwa likimfuata kwa ukaribu. Nao wakapewa mamlaka juu ya sehemu ya nne ya dunia, ili kuua kwa upanga+ mrefu na kwa upungufu wa chakula+ na kwa pigo lenye kufisha na kwa wanyama-mwitu+ wa dunia.
9 Naye alipofungua muhuri wa tano, nikaona chini ya madhabahu+ nafsi+ za wale waliouawa+ kwa sababu ya neno la Mungu na kwa sababu ya kazi ya ushahidi+ waliyokuwa nayo.
10 Nao wakalia kwa sauti kubwa, wakisema: “Utajizuia mpaka wakati gani, Bwana Mwenye Enzi Kuu+ mtakatifu na wa kweli,+ kuhukumu+ na kulipiza kisasi cha damu+ yetu juu ya wale wanaokaa duniani?”
11 Na kila mmoja wao akapewa kanzu nyeupe;+ nao wakaambiwa wapumzike tena muda kidogo, mpaka ijazwe pia hesabu ya watumwa wenzao na ndugu zao waliokuwa karibu kuuawa+ kama vile wao pia walivyouawa.
12 Nami nikaona alipofungua muhuri wa sita, na tetemeko kubwa la nchi likatokea; na jua likawa jeusi kama gunia+ la manyoya, na mwezi mzima ukawa kama damu,+
13 na nyota za mbinguni zikaanguka duniani, kama vile mtini unaotikiswa na upepo mkali unavyozitupa tini zake mbichi.
14 Na mbingu ikaondoka kama kitabu cha kukunjwa kinachokunjwa,+ na kila mlima na kila kisiwa vikaondolewa mahali pake.+
15 Na wafalme wa dunia na wenye daraja la juu na viongozi wa kijeshi na matajiri na wenye nguvu na kila mtumwa na kila mtu huru wakajificha katika mapango na katika miamba+ ya milima.
16 Nao wanaendelea kuiambia milima na miamba: “Tuangukieni,+ mtufiche kutoka usoni pa Yule anayeketi juu ya kile kiti cha ufalme+ na kutoka kwenye ghadhabu ya Mwana-Kondoo,+
17 kwa sababu siku kuu+ ya ghadhabu+ yao imekuja, na ni nani anayeweza kusimama?”+
Maelezo ya Chini
^ Hadesi. Tazama Nyongeza 4.