Ufunuo 20:1-15
20 Nami nikamwona malaika akishuka kutoka mbinguni mwenye ufunguo wa abiso+ na mnyororo mkubwa mkononi mwake.
2 Naye akamkamata yule joka+ mkubwa, yule nyoka wa zamani,+ ambaye ni Ibilisi+ na Shetani,+ na kumfunga kwa miaka elfu.
3 Naye akamtupa ndani ya abiso+ na kuifunga na kuitia muhuri juu yake, ili asipotoshe mataifa tena mpaka ile miaka elfu itakapokwisha. Baada ya mambo hayo yeye atafunguliwa kwa muda kidogo.+
4 Nami nikaona viti vya ufalme,+ na kulikuwa na wale walioketi juu yake, nao wakapewa mamlaka ya kuhukumu.+ Ndiyo, niliona nafsi za wale waliouawa kwa shoka kwa ajili ya ushahidi waliotoa kumhusu Yesu na kwa ajili ya kusema juu ya Mungu, na wale ambao hawakumwabudu yule mnyama-mwitu+ wala sanamu+ yake na ambao hawakupokea ile alama juu ya paji la uso wao na juu ya mkono wao.+ Nao wakawa hai na kutawala wakiwa wafalme+ pamoja na Kristo kwa miaka elfu.
5 (Wale wafu+ wengine hawakuwa hai mpaka ile miaka elfu ilipokwisha.)+ Huo ndio ufufuo wa kwanza.+
6 Mwenye furaha+ na mtakatifu+ ni yeyote aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza; kifo cha pili+ hakina mamlaka juu ya hao,+ bali watakuwa makuhani+ wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala wakiwa wafalme pamoja naye ile miaka elfu.+
7 Sasa mara tu ile miaka elfu itakapokwisha, Shetani atafunguliwa kutoka katika gereza lake,
8 naye ataenda kuyapotosha yale mataifa yaliyo katika pembe nne za dunia, Gogu na Magogu, kuwakusanya pamoja kwa ajili ya vita. Hesabu yao ni kama mchanga wa bahari.+
9 Nao wakasonga juu ya upana wa dunia na kuizunguka kambi ya watakatifu+ na lile jiji+ linalopendwa. Lakini moto ukashuka kutoka mbinguni na kuwateketeza.+
10 Na Ibilisi+ aliyekuwa akiwapotosha alitupwa ndani ya lile ziwa la moto na kiberiti, ambamo wote wawili, yule mnyama-mwitu+ na yule nabii wa uwongo, tayari walikuwa;+ nao watateswa mchana na usiku milele na milele.
11 Nami nikaona kiti cha ufalme kikubwa cheupe na yeye aliyeketi juu yake.+ Dunia na mbingu zikakimbia kutoka mbele zake,+ na mahali popote hapakupatikana kwa ajili ya hizo.
12 Nami nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo,+ wamesimama mbele ya kile kiti cha ufalme, na vitabu vya kukunjwa vikafunguliwa. Lakini kitabu kingine cha kukunjwa kikafunguliwa; hicho ni kitabu cha uzima.+ Na wafu wakahukumiwa kutokana na mambo yale yaliyoandikwa katika vile vitabu kulingana na matendo yao.+
13 Na bahari ikawatoa wale wafu waliokuwa ndani yake, na kifo na Kaburi* vikawatoa wale wafu+ waliokuwa ndani yake, nao walihukumiwa kila mmoja kulingana na matendo yake.+
14 Na kifo+ na Kaburi* vikatupwa ndani ya lile ziwa la moto. Hili linamaanisha kifo cha pili,+ lile ziwa la moto.+
15 Zaidi ya hayo, yeyote ambaye hakupatikana ameandikwa katika kile kitabu cha uzima+ alitupwa ndani ya lile ziwa la moto.+