Ufunuo 12:1-17
12 Na ishara+ kubwa ilionekana mbinguni, mwanamke+ aliyepambwa jua, na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake, na juu ya kichwa chake palikuwa na taji la nyota kumi na mbili,
2 naye alikuwa na mimba. Naye analia akiwa katika maumivu+ na katika uchungu wake wa kuzaa.
3 Na ishara nyingine ilionekana mbinguni, na, tazama! joka+ mkubwa wa rangi ya moto, mwenye vichwa saba na pembe kumi na mataji saba juu ya vichwa vyake;
4 na mkia+ wake unakokota sehemu ya tatu ya nyota+ za mbinguni, naye akazitupa chini mpaka duniani.+ Na huyo joka mkubwa akaendelea kusimama mbele ya yule mwanamke+ aliyekuwa karibu kuzaa,+ ili, atakapozaa, ammeze+ mtoto wake.
5 Na mwanamke yule akamzaa mwana,+ mwanamume, atakayechunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma.+ Na mtoto wake akanyakuliwa mpaka kwa Mungu na kwenye kiti chake cha ufalme.+
6 Na mwanamke yule akakimbilia nyikani,+ ambapo ana mahali palipotayarishwa na Mungu, ili wamlishe+ hapo siku 1,260.+
7 Na vita vikatokea ghafula mbinguni: Mikaeli+ na malaika zake wakapigana na yule joka mkubwa, naye joka mkubwa na malaika zake wakapigana
8 lakini hakushinda, wala mahali hapakupatikana mbinguni kwa ajili yao tena.
9 Kwa hiyo yule joka+ mkubwa akatupwa chini, yule nyoka wa zamani,+ yeye anayeitwa Ibilisi+ na Shetani,+ anayeipotosha dunia nzima inayokaliwa;+ akatupwa chini duniani,+ na malaika zake wakatupwa chini pamoja naye.
10 Nami nikaisikia sauti kubwa mbinguni ikisema:
“Sasa kumekuwa na wokovu+ na nguvu+ na ufalme wa Mungu wetu+ na mamlaka ya Kristo wake,+ kwa sababu mshtaki wa ndugu zetu ametupwa chini, anayewashtaki mchana na usiku mbele za Mungu wetu!+
11 Nao wakamshinda+ kwa sababu ya damu ya Mwana-Kondoo+ na kwa sababu ya neno la kutoa kwao ushahidi,+ nao hawakupenda nafsi+ zao hata walipokabili kifo.
12 Kwa sababu hiyo furahini, enyi mbingu nanyi mnaokaa ndani yake!+ Ole+ wa dunia na wa bahari,+ kwa sababu Ibilisi ameshuka kwenu, akiwa na hasira kali, akijua kwamba ana kipindi kifupi cha wakati.”+
13 Sasa yule joka mkubwa alipoona kwamba ametupwa chini duniani,+ alimtesa yule mwanamke+ aliyezaa mtoto mwanamume.
14 Lakini yule mwanamke akapewa mabawa mawili ya tai mkubwa,+ ili aruke kwenda nyikani+ mahali pake; hapo ndipo anapolishwa+ kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati+ mbali na uso wa yule nyoka.+
15 Naye nyoka akatapika maji+ kama mto kutoka katika kinywa chake nyuma ya yule mwanamke, ili kumzamisha kwa mto huo.+
16 Lakini dunia ikaja kumsaidia mwanamke,+ nayo dunia ikafungua kinywa chake na kuumeza mto ambao yule joka mkubwa aliutapika kutoka katika kinywa chake.
17 Na yule joka mkubwa akawa na ghadhabu kumwelekea yule mwanamke,+ naye akaenda zake kupigana vita na wale waliobaki wa uzao wake, wanaoshika amri za Mungu na walio na kazi ya kutoa ushahidi+ kumhusu Yesu.