Ufunuo 11:1-19
11 Nami nikapewa utete unaofanana na fimbo+ aliposema: “Simama upime patakatifu pa hekalu+ la Mungu na madhabahu na wale wanaoabudu ndani yake.
2 Lakini kwa habari ya ua ulio nje+ ya patakatifu pa hekalu, utupe nje kabisa wala usiupime, kwa sababu mataifa+ wamepewa huo, nao watalikanyagia chini ya miguu lile jiji takatifu+ kwa miezi 42.+
3 Nami nitawafanya mashahidi wangu wawili+ watoe unabii+ kwa siku 1,260 wakiwa wamevikwa nguo za magunia.”+
4 Hao wanafananishwa na ile mizeituni miwili+ na vile vinara viwili vya taa+ nao wamesimama mbele za Bwana wa dunia.+
5 Na yeyote akitaka kuwadhuru, moto hutoka katika vinywa vyao na kuwateketeza adui zao;+ na yeyote akitaka kuwadhuru, lazima atauawa kwa njia hiyo.
6 Hawa wana mamlaka ya kufunga mbingu+ ili mvua isinyeshe+ katika siku zao za kutoa unabii, nao wana mamlaka juu ya maji ili kuyageuza kuwa damu+ na kuipiga dunia kwa kila namna ya mapigo mara nyingi kama vile wanavyopenda.
7 Na wakiisha kumaliza kutoa ushahidi wao, yule mnyama-mwitu anayepanda kutoka katika abiso+ atapigana vita nao na kuwashinda na kuwaua.+
8 Na maiti zao zitakuwa juu ya njia pana ya lile jiji kubwa ambalo katika maana ya kiroho linaitwa Sodoma+ na Misri, ambako pia Bwana wao alitundikwa mtini.+
9 Na wale kati ya vikundi vya watu na makabila na lugha na mataifa+ watazitazama maiti zao kwa siku tatu na nusu,+ wala hawaziachi maiti zao zilazwe kaburini.
10 Na wale wanaokaa duniani wanashangilia+ juu yao na kujifurahisha, na watapelekeana zawadi,+ kwa sababu hao manabii wawili waliwatesa wale wanaokaa duniani.
11 Na baada ya zile siku tatu na nusu+ roho ya uhai kutoka kwa Mungu ikaingia ndani yao,+ nao wakasimama kwa miguu yao, na woga mkubwa ukawaingia wale waliokuwa wakiwatazama.
12 Nao wakasikia sauti kubwa+ kutoka mbinguni ikiwaambia: “Pandeni mje huku.”+ Nao wakapanda kuingia mbinguni katika wingu, na adui zao wakawatazama.
13 Na katika saa hiyo tetemeko kubwa la nchi likatokea, na sehemu ya kumi+ ya jiji ikaanguka; na watu elfu saba wakauawa na tetemeko hilo la nchi, na wale wengine wakawa na hofu na kumpa utukufu Mungu wa mbinguni.+
14 Ole wa pili+ umepita. Tazama! Ole wa tatu unakuja upesi.
15 Na malaika wa saba akaipiga tarumbeta yake.+ Na sauti kubwa zikatokea mbinguni, zikisema: “Ufalme wa ulimwengu umekuwa ufalme wa Bwana+ wetu na wa Kristo+ wake, naye atatawala akiwa mfalme milele na milele.”+
16 Na wale wazee 24+ waliokuwa wameketi juu ya viti vyao vya ufalme mbele za Mungu wakaanguka kifudifudi+ na kumwabudu Mungu,+
17 wakisema: “Tunakushukuru wewe,+ Yehova Mungu, Mweza-Yote,+ Yeye aliyeko+ na aliyekuwako, kwa sababu umechukua nguvu zako kuu+ na kuanza kutawala ukiwa mfalme.+
18 Lakini mataifa wakawa na ghadhabu, nayo ghadhabu yako mwenyewe ikaja, na wakati uliowekwa kwa ajili ya kuhukumiwa kwa wafu, na kuwapa thawabu+ watumwa wako manabii+ na watakatifu na wale wanaoliogopa jina lako, wadogo kwa wakubwa,+ na kuwaharibu+ wale wanaoiharibu dunia.”+
19 Na patakatifu pa hekalu la Mungu palipo mbinguni+ pakafunguliwa, na sanduku+ la agano lake likaonekana katika patakatifu pa hekalu lake.+ Na kukatokea umeme na sauti na ngurumo na tetemeko la nchi na mvua kubwa ya mawe.