Ufunuo 10:1-11
10 Nami nikamwona malaika+ mwingine mwenye nguvu akishuka kutoka mbinguni, amepambwa wingu,+ na upinde wa mvua ulikuwa juu ya kichwa chake, na uso wake ulikuwa kama jua,+ na miguu+ yake ilikuwa kama nguzo za moto,
2 na mkononi mwake alikuwa na kitabu kidogo cha kukunjwa kilichofunguliwa. Naye akaweka mguu wake wa kuume juu ya bahari, lakini ule wa kushoto juu ya dunia,+
3 naye akapaaza kilio kwa sauti kubwa kama vile simba+ anaponguruma. Na alipopaaza kilio, zile ngurumo+ saba zikatoa sauti zao.
4 Basi zile ngurumo saba ziliposema, nilikuwa karibu kuandika; lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni+ ikisema: “Yatie muhuri mambo+ ambayo zile ngurumo saba zilisema, nawe usiyaandike hayo.”
5 Na yule malaika niliyemwona amesimama juu ya bahari na juu ya dunia akainua mkono wake wa kuume kuelekea mbinguni,+
6 naye akaapa kwa Yule anayeishi+ milele na milele,+ aliyeiumba mbingu na vitu vilivyo ndani yake na dunia+ na vitu vilivyo ndani yake na bahari na vitu vilivyo ndani yake:+ “Hakutakuwa tena na kukawia;+
7 bali katika siku za kupiga kwa yule malaika wa saba,+ akiwa karibu kuipiga tarumbeta yake,+ ile siri takatifu+ ya Mungu kulingana na habari njema aliyowatangazia watumwa wake mwenyewe manabii+ itamalizika.”
8 Na ile sauti+ niliyosikia kutoka mbinguni inasema nami tena na kuniambia: “Nenda, kichukue kile kitabu cha kukunjwa kilichofunguliwa ambacho kimo mkononi mwa malaika ambaye amesimama juu ya bahari na juu ya dunia.”+
9 Nami nikaenda zangu kwa yule malaika na kumwambia anipe kile kitabu kidogo cha kukunjwa. Naye akaniambia: “Kichukue, ukile,+ nacho kitalitia tumbo lako uchungu, lakini kinywani mwako kitakuwa kitamu kama asali.”
10 Nami nikakichukua kile kitabu kidogo cha kukunjwa kutoka mkononi mwa yule malaika kisha nikakila,+ nacho kinywani mwangu kilikuwa kitamu kama asali;+ lakini nilipokuwa nimekila, tumbo langu likatiwa uchungu.
11 Nao wakaniambia: “Lazima utoe unabii tena kuhusiana na vikundi vya watu na mataifa na lugha na wafalme wengi.”+