Habakuki 3:1-19
3 Sala ya Habakuki nabii katika nyimbo za huzuni:
2 Ee Yehova, nimeisikia habari juu yako.+ Nimeogopa utendaji wako,+ Ee Yehova.
Ufanye hai utendaji wako katikati ya ile miaka! Ufanye ujulikane katikati ya ile miaka. Wakati wa msukosuko, ukumbuke kuonyesha rehema.+
3 Mungu mwenyewe alikuja kutoka Temani, Mtakatifu kutoka Mlima Parani.+ Sela.+
Utukufu wake ulizifunika mbingu;+ na dunia ikajazwa sifa yake.+
4 Nao uangavu wake, ukawa kama vile nuru.+ Alikuwa na miale miwili ikitoka mkononi mwake, na hapo ndipo palipofichwa nguvu zake.+
5 Tauni ikaenda mbele zake,+ na homa kali ilikuwa ikitoka miguuni pake.+
6 Alisimama tuli, apate kuitikisa dunia.+ Aliona, kisha akayarusha mataifa.+
Na milima ya milele ikavunjwa;+ vilima vinavyodumu kwa wakati usio na kipimo vikainama.+ Miendo ya zamani za kale ni yake.
7 Chini ya kitu chenye kudhuru niliona mahema ya Kushani. Vitambaa vya mahema ya nchi ya Midiani+ vikaanza kufadhaika.+
8 Je, ni juu ya mito, Ee Yehova, je, hasira yako imewaka juu ya mito,+ au je, ghadhabu yako iko juu ya bahari?+ Kwa maana ulipanda farasi zako;+ magari yako yalikuwa wokovu.+
9 Katika uchi wake upinde wako hufunuliwa.+ Viapo rasmi vya makabila ndivyo jambo lililosemwa.+ Sela. Ukaipasua dunia kwa mito.+
10 Milima ilikuona; ikawa katika maumivu makali.+ Dhoruba ya maji yenye mngurumo ikapita kati. Kilindi cha maji kikatoa mvumo wake.+ Kikainua mikono yake juu.
11 Jua—mwezi—vilisimama tuli,+ kwenye makao yaliyo juu sana.+ Kama nuru mishale yako mwenyewe ikaenda mfululizo.+ Mng’ao wa mkuki wako ukaangaza.+
12 Kwa shutuma ulipiga mwendo kati ya dunia. Kwa hasira ukayapura mataifa.+
13 Ukajitokeza kwa ajili ya wokovu wa watu wako,+ upate kumwokoa mtiwa-mafuta wako. Ulimvunja vipande-vipande aliye kichwa kutoka kwa nyumba ya mwovu.+ Msingi uliwekwa wazi, mpaka shingoni.+ Sela.
14 Kwa fimbo zake mwenyewe ulikichoma+ kichwa cha mashujaa wake wa vita waliposonga kama tufani ili kunitawanya.+ Upeo wao wa raha ulikuwa kama wa wale wanaokusudia kummeza mwenye kuteseka katika maficho.+
15 Kupitia bahari ulikanyaga kwa farasi zako, kupitia mkusanyo wa maji mengi.+
16 Nilisikia, tumbo langu likaanza kutetemeka; midomo yangu ilitetemeka kwa sababu ya ule mvumo; kuoza kukaanza kuingia katika mifupa yangu;+ na katika hali yangu nikafadhaika, kwamba ningojee kimya siku ya taabu,+ kuja kwake kwa watu,+ apate kuwavamia.
17 Ijapokuwa huenda mtini usichanue,+ kusiwe na mazao kwenye mizabibu; kazi ya mzeituni ikashindwa, matuta yasizae chakula chochote.+ Huenda kundi liondolewe zizini, na kusiwe na mifugo katika mazizi;+
18 Lakini mimi, nitafurahi katika Yehova mwenyewe;+ nitakuwa na shangwe katika Mungu wa wokovu wangu.+
19 Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu ndiye nguvu zangu;+ naye ataifanya miguu yangu kama ile ya paa,+ na mahali pangu pa juu atanitembeza.+
Kwa kiongozi wa
vinanda vyangu.