Ezekieli 5:1-17
5 “Na wewe, Ee Mwana wa binadamu, jichukulie upanga mkali. Utajichukulia ulio kama wembe wa kinyozi, nawe utaupitisha juu ya kichwa chako na juu ya ndevu zako,+ nawe utajichukulia mizani ya kupimia na kuzigawanya nywele hizo katika mafungu.
2 Sehemu ya tatu utaiteketeza katika moto katikati ya jiji mara tu zitakapotimia siku za kuzingira.+ Nawe utachukua sehemu nyingine ya tatu. Utaipiga kwa upanga kulizunguka jiji pande zote,+ nayo sehemu ya tatu ya mwisho utaitawanya kwenye upepo, nami nitauchomoa upanga nyuma yao.+
3 “Nawe utachukua hesabu ndogo katika hizo na kuzifunga katika pindo za nguo yako.+
4 Na nyingine kati ya hizo utazichukua nawe utazitupa katikati ya moto na kuziteketeza katika moto. Kutoka kwa moto huo utatoka na kwenda katika nyumba yote ya Israeli.+
5 “Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema, ‘Huyu ni Yerusalemu. Katikati ya mataifa nimemweka, kukiwa na nchi zinazomzunguka pande zote.
6 Naye alijiendesha kwa kuyaasi maamuzi yangu ya hukumu katika uovu kuliko mataifa,+ na kuziasi sheria zangu kuliko nchi zinazomzunguka pande zote, kwa maana waliyakataa maamuzi yangu ya hukumu, nao hawakutembea katika sheria zangu.’+
7 “Kwa hiyo hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema, ‘Kwa sababu mlikuwa na fujo+ kuliko mataifa yanayowazunguka ninyi pande zote, hamkutembea katika sheria zangu na hamkufanya maamuzi yangu ya hukumu;+ bali mlifanya kulingana na maamuzi ya hukumu ya mataifa yanayowazunguka pande zote, sivyo?+
8 kwa hiyo hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Tazama niko dhidi yako, Ee jiji, naam mimi,+ nami nitayatenda katikati yako maamuzi ya hukumu machoni pa mataifa.+
9 Nami nitafanya ndani yako jambo ambalo sijafanya na ambalo mfano wake sitafanya tena kwa sababu ya machukizo yenu yote.+
10 “ ‘ “Kwa hiyo akina baba wenyewe watakula wana katikati yako,+ na wana wenyewe watakula baba zao, nami nitatenda ndani yako matendo ya hukumu na kutawanya mabaki yako yote kuelekea kila upepo.” ’+
11 “ ‘Kwa hiyo kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘kwa hakika kwa sababu ni patakatifu pangu ulipopatia unajisi kwa machukizo+ yako yote na kwa vinyaa+ vyako vyote, mimi mwenyewe pia Ndiye nitakayekupunguza+ wewe nalo jicho langu halitakusikitikia+ na mimi mwenyewe sitakuhurumia.+
12 Sehemu ya tatu yako—kwa tauni watakufa,+ na kwa njaa watafikia mwisho wao katikati yako.+ Na sehemu nyingine ya tatu—kwa upanga wataanguka kukuzunguka pande zote. Na sehemu ya tatu ya mwisho nitawatawanya hata kuelekea kila upepo,+ nami nitauchomoa upanga nyuma yao.+
13 Na hasira yangu hakika itafikia mwisho+ wake nami nitaituliza ghadhabu yangu juu yao+ na kujifariji mwenyewe;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimesema katika kusisitiza kwangu kwamba watu wajitoe kikamili,+ nitakapomaliza ghadhabu yangu juu yao.
14 “ ‘Nami nitakufanya kuwa ukiwa na shutuma kati ya mataifa yanayokuzunguka pande zote mbele ya macho ya kila mpita-njia.+
15 Nawe utakuwa shutuma+ na kitu cha kutukanwa,+ mfano wa kuonya+ na tisho kwa mataifa yanayokuzunguka pande zote, nitakapotenda ndani yako matendo ya hukumu katika hasira na katika ghadhabu na katika makaripio ya ghadhabu.+ Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema.
16 “ ‘Nitakapotuma ile mishale yenye madhara ya njaa juu yao,+ itakayokuwa ya uharibifu, mishale ambayo nitatuma ili kuwaharibu ninyi,+ hata njaa nitaiongeza juu yenu nami nitazivunja fimbo zenu ambazo mikate ya mviringo huning’inizwa kuzizunguka.+
17 Nami nitatuma juu yenu njaa na wanyama-mwitu wenye kudhuru,+ nao watawaua watoto wenu, na tauni+ na damu+ zitapitia katikati yenu, nami nitauleta upanga juu yenu.+ Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema.’”