Ezekieli 36:1-38
36 “Na wewe, Ee mwana wa binadamu, toa unabii juu ya milima ya Israeli, nawe utasema, ‘Ee milima ya Israeli,+ lisikieni neno la Yehova.
2 Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Kwa sababu adui amesema juu yenu,+ ‘Aha! Hata mahali pa juu pa wakati wa kale+—pamekuwa mali yetu!’ ” ’+
3 “Kwa hiyo toa unabii, nawe utasema, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Kwa sababu, naam, kwa sababu kumekuwa na kufanywa ukiwa+ na kuumwa kutoka pande zote,+ ili muwe mali ya mabaki ya mataifa+ nanyi mnaendelea kusemwa kwa midomo+ na kati ya watu kuna habari mbaya,+
4 kwa hiyo, enyi milima ya Israeli,+ lisikieni neno la Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova! Ni hivi Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova ameambia milima na vilima, vijito na mabonde na mahali palipoharibiwa+ na kufanywa ukiwa na majiji yaliyoachwa ambayo yameporwa na kudhihakiwa na mabaki ya mataifa yanayozunguka pande zote;+
5 kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Hakika katika moto wa bidii yangu nitasema+ juu ya mabaki ya mataifa na juu ya Edomu yote,+ wale ambao wamejipatia wenyewe nchi yangu iwe mali yao kwa kushangilia kwa moyo wote,+ kwa dharau katika nafsi yao,+ kwa ajili ya kiwanja chake cha malisho na ili kuipora.’ ” ’+
6 “Kwa hiyo toa unabii kuhusu udongo wa Israeli, nawe utaambia milima na vilima, vijito na mabonde, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Tazama! mimi mwenyewe katika bidii yangu na katika ghadhabu yangu lazima nitasema, kwa sababu mmechukua fedheha ya mataifa.” ’+
7 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Mimi mwenyewe nimeuinua mkono wangu katika kiapo+ ili mataifa yanayowazunguka pande zote—hayo yatachukua fedheha yao yenyewe.+
8 Na ninyi wenyewe, enyi milima ya Israeli, mtatoa matawi yenu wenyewe na kuzaa matunda yenu wenyewe kwa ajili ya watu wangu Israeli,+ kwa maana wamekaribia hatua ya kuingia ndani.+
9 Kwa maana tazama, nimewapa ninyi kibali changu, nami hakika nitageuka kuwaelekea ninyi,+ na kwa kweli ninyi mtalimwa na kupandwa mbegu.+
10 Nami nitazidisha binadamu juu yenu, nyumba yote ya Israeli, naam, nyumba yote,+ na majiji yatakaliwa,+ na mahali palipoharibiwa penyewe patajengwa upya.+
11 Naam, nitawazidisha binadamu na wanyama juu yenu,+ nao hakika wataongezeka na kuzaa, nami kwa kweli nitawafanya ninyi mkaliwe kama ilivyokuwa hali yenu ya zamani+ nami nitafanya mema zaidi kuliko ilivyokuwa hali yenu ya zamani;+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.+
12 Na juu yenu nitawafanya binadamu watembee, naam, watu wangu Israeli, nao watawamiliki ninyi,+ nanyi mtakuwa fungu lao la urithi,+ nanyi hamtawaua+ watoto wao tena.’ ”
13 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Kwa sababu kuna wale wanaowaambia ninyi: “Wewe ni mmezaji wa binadamu, nawe umekuwa nchi inayowaua watoto wa mataifa yako,” ’+
14 ‘kwa hiyo hutawameza binadamu tena,+ nawe hutawaua watoto wa mataifa yako tena,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.
15 ‘Nami sitasababisha tena mazungumzo zaidi yenye kufedhehesha ya mataifa yasikiwe juu yako,+ nawe hutachukua tena shutuma ya watu,+ nayo mataifa yako hutayafanya yajikwae tena,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”
16 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema:
17 “Mwana wa binadamu, nyumba ya Israeli walikuwa wakikaa katika nchi yao, nao wakaendelea kuichafua kwa njia yao na kwa matendo yao.+ Njia yao imekuwa mbele zangu kama uchafu wa hedhi.+
18 Nami nikamwaga ghadhabu yangu juu yao kwa sababu ya damu waliyokuwa wameimwaga juu ya nchi,+ nchi ambayo walikuwa wameichafua kwa sanamu zao za mavi.+
19 Nami nikawatawanya katikati ya mataifa, hivi kwamba wakasambaa katika nchi mbalimbali.+ Niliwahukumu kulingana na njia yao na kulingana na matendo yao.+
20 Kwa hiyo wakaingia kwa mataifa ambamo waliingia, na watu wakatia unajisi jina langu takatifu+ kwa kusema hivi juu yao, ‘Hawa ndio watu wa Yehova, nao wametoka katika nchi yake.’+
21 Nami nitalihurumia jina langu takatifu, ambalo nyumba ya Israeli imelitia unajisi katikati ya mataifa ambamo wameingia.”+
22 “Kwa hiyo iambie nyumba ya Israeli, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Sifanyi jambo hili kwa ajili yenu, Ee nyumba ya Israeli, bali kwa ajili ya jina langu takatifu, ambalo ninyi mmelitia unajisi katikati ya mataifa ambamo mmeingia.” ’+
23 ‘Nami hakika nitalitakasa jina langu kuu,+ ambalo lilikuwa likitiwa unajisi katikati ya mataifa, ambalo ninyi mlilitia unajisi katikati yao; nayo mataifa yatalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘wakati nitakapotakaswa katikati yenu mbele ya macho yao.+
24 Nami nitawatoa ninyi kutoka kwa mataifa na kuwakusanya pamoja kutoka katika nchi zote na kuwaingiza katika nchi yenu.+
25 Nami nitawanyunyizia maji safi, nanyi mtakuwa safi;+ nami nitawasafisha ninyi kutokana na uchafu+ wenu wote na kutokana na sanamu zenu zote za mavi.+
26 Nami nitawapa ninyi moyo mpya,+ na nitatia ndani yenu roho mpya,+ nami nitauondoa moyo wa jiwe kutoka mwilini mwenu na kuwapa ninyi moyo wa nyama.+
27 Nami nitaitia roho yangu ndani yenu,+ nami nitachukua hatua ili mtembee katika masharti yangu,+ nayo maamuzi yangu ya hukumu mtayashika na kuyafanya kikweli.+
28 Nanyi hakika mtakaa katika nchi niliyowapa mababu zenu,+ nanyi mtakuwa watu wangu na mimi mwenyewe nitakuwa Mungu wenu.’+
29 “ ‘Nami nitawaokoa ninyi kutoka kwenye uchafu+ wenu wote na kuiita nafaka na kuifanya iwe tele, nami sitaweka juu yenu njaa yoyote.+
30 Nami hakika nitafanya matunda ya mti yawe tele, na mazao ya shamba, ili msishutumiwe tena na mataifa kwa sababu ya njaa.+
31 Nanyi mtakumbuka njia zenu mbaya na matendo yenu ambayo hayakuwa mazuri,+ nanyi mtachukizwa na nafsi zenu wenyewe kwa sababu ya makosa yenu na kwa sababu ya machukizo yenu.+
32 Sifanyi jambo hili kwa ajili yenu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘na ijulikane kwenu. Mwone aibu na kufedheheka kwa sababu ya njia zenu, Ee nyumba ya Israeli.’+
33 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Siku nitakayowasafisha ninyi kutokana na makosa yenu yote nitayafanya pia majiji yakaliwe,+ na mahali palipoharibiwa patajengwa upya.+
34 Nayo nchi iliyofanywa ukiwa italimwa, ingawa ilikuwa imekuwa mahame yenye ukiwa machoni pa kila mpita-njia.+
35 Na hakika watu watasema: “Ile nchi kule ambayo ilifanywa ukiwa imekuwa kama bustani ya Edeni,+ nayo majiji yaliyokuwa ukiwa na ambayo yalikuwa yamebomolewa yametiwa ngome; yamekaliwa.”+
36 Nayo mataifa yatakayokuwa yamebaki kuwazunguka ninyi pande zote yatalazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimejenga vitu vilivyobomolewa,+ nimepanda kilichofanywa ukiwa. Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema nami nimelitenda.’+
37 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Hili ndilo bado nitajiacha niulizwe na nyumba ya Israeli ili niwafanyie:+ Mimi nitawazidisha kwa watu kama kundi.+
38 Kama kundi la watu watakatifu, kama kundi la Yerusalemu katika majira yake ya sherehe,+ hivyo ndivyo majiji yaliyokuwa yamefanywa ukiwa yatakavyojaa kundi la watu;+ nao watu watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’ ”