Ezekieli 22:1-31
22 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema:
2 “Na wewe, Ee mwana wa binadamu, je, utahukumu,+ je, utahukumu lile jiji lenye hatia ya damu+ na kulifanya lijue machukizo yake yote?+
3 Nawe utasema, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Ee jiji, linalomwaga damu+ katikati yake mpaka wakati wake ufike,+ na ambalo limefanya sanamu za mavi ndani yake ili kuwa lisilo safi,+
4 umekuwa na hatia kwa damu yako ambayo umemwaga,+ na umekuwa usiye safi kwa sanamu zako za mavi ambazo umefanya.+ Nawe unazileta siku zako karibu, nawe utaifikia miaka yako. Ndiyo sababu lazima nikufanye kuwa kitu cha kushutumiwa kwa mataifa na cha kudhihakiwa katika nchi zote.+
5 Nchi zilizo karibu nawe na zile zilizo mbali nawe zitakudhihaki, wewe uliye na jina lisilo safi, uliyejaa mvurugo.+
6 Tazama! Wakuu+ wa Israeli wamekuwa ndani yako, kila mmoja akiwa amejitoa kwa mkono wake ili kumwaga damu.+
7 Wamemtendea dharau baba na mama ndani yako.+ Wamemtendea mkaaji mgeni ndani yako kwa upunjaji.+ Wamewatendea vibaya mvulana asiye na baba na mjane ndani yako.” ’ ”+
8 “ ‘Umepadharau mahali pangu patakatifu, nazo sabato zangu umezitia unajisi.+
9 Wachongezi wanaofanya hivyo waziwazi wamo ndani yako, kwa kusudi la kumwaga damu;+ nao wamekula juu ya milima ndani yako.+ Wameendeleza mwenendo mpotovu ndani yako.+
10 Wameufunua uchi wa baba ndani yako;+ wamemfedhehesha mwanamke asiye safi katika hedhi yake ndani yako.+
11 Na mwanamume amefanya chukizo pamoja na mke wa mwenzake, na mwanamume amemnajisi+ binti-mkwe wake mwenyewe kwa mwenendo mpotovu;+ na ndani yako mwanamume amemfedhehesha dada yake, binti ya baba yake mwenyewe.+
12 Wamechukua rushwa ndani yako kwa kusudi la kumwaga damu.+ Umechukua faida na riba,+ nawe kwa ujeuri unaendelea kupata mapato+ ya wenzako kwa upunjaji,+ nawe umenisahau mimi,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.
13 “ ‘Na, tazama! Nimeupiga mkono wangu+ kwa sababu ya pato lisilo la haki ambalo umepata,+ na kwa sababu ya matendo yako ya kumwaga damu yaliyo katikati yako.+
14 Je, moyo wako utaendelea kuvumilia+ au mikono yako kukupa nguvu katika siku ambayo nitatenda kukuelekea wewe?+ Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema nami nitatenda.+
15 Nami nitakutawanya wewe kati ya mataifa na kukutawanya kati ya nchi+ hizo, nami nitauharibu uchafu wako kutoka ndani yako.+
16 Nawe hakika utatiwa unajisi ndani yako mwenyewe mbele ya macho ya mataifa, nawe utalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’ ”+
17 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema:
18 “Mwana wa binadamu, kwangu mimi wale wa nyumba ya Israeli wamekuwa kama takataka.+ Wote ni shaba na bati na chuma na risasi katikati ya tanuru. Wamekuwa takataka nyingi, ile ya fedha.+
19 “Kwa hiyo, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi, ‘Kwa sababu ninyi nyote mmekuwa kama takataka+ nyingi, kwa hiyo, tazama, ninawakusanya ninyi pamoja katikati ya Yerusalemu.+
20 Kama kukusanya fedha na shaba na chuma+ na risasi na bati katikati ya tanuru, ili kupuliza+ juu yake kwa moto kusudi ziyeyuke,+ ndivyo nitakavyowakusanya wao pamoja katika hasira yangu na katika ghadhabu yangu, nami nitawapuliza na kuwayeyusha ninyi.
21 Nami nitawakusanya pamoja na kupuliza juu yenu kwa moto wa ghadhabu yangu,+ nanyi mtayeyushwa katikati yake.+
22 Kama kuyeyushwa kwa fedha katikati ya tanuru, ndivyo ninyi mtakavyoyeyushwa katikati yake; nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimemwaga ghadhabu yangu juu yenu.’ ”+
23 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema:
24 “Mwana wa binadamu, iambie hivi, ‘Wewe ni nchi isiyosafishwa, ambayo hainyeshewi wakati wa siku ya shutuma.+
25 Katikati yake kuna hila ya manabii wake,+ kama simba anayenguruma, anayerarua mawindo.+ Kwa kweli wanairarua nafsi.+ Wanaendelea kuchukua hazina na vitu vyenye thamani.+ Wamewazidisha wajane wake katikati yake.+
26 Makuhani wake wenyewe wameitendea jeuri sheria yangu,+ nao wanaendelea kutia unajisi mahali pangu patakatifu.+ Hawatofautishi kati ya kitu kitakatifu na cha kawaida,+ nao hawajafanya chochote kijulikane kati ya kitu kisicho safi na kilicho safi,+ nao wameyaficha macho+ yao yasione sabato zangu, nami ninatiwa unajisi katikati yao.+
27 Wakuu wake walio katikati yake ni kama mbwa-mwitu wanaorarua mawindo katika kumwaga damu,+ katika kuangamiza nafsi kusudi wapate pato lisilo la haki.+
28 Nao manabii wake wamewapigia lipu kwa kutumia chokaa,+ wakiona maono yasiyo halisi+ na kuagua uwongo+ kwa ajili yao, na kusema: “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi,” wakati ambapo Yehova mwenyewe hajasema.
29 Watu wa nchi wenyewe wameendesha mbinu ya kupunja+ nao wamenyakua katika unyang’anyi,+ nao wamemtendea vibaya+ anayeteseka na aliye maskini, na kumpunja bila haki mkaaji mgeni.’+
30 “ ‘Nami nikaendelea kumtafuta mtu kati yao ambaye angekuwa akiurekebisha ukuta wa mawe+ na kusimama katika pengo+ mbele yangu kwa ajili ya nchi hiyo, ili mimi nisiiangamize;+ nami sikumpata yeyote.
31 Kwa hiyo nitamwaga shutuma+ zangu juu yao. Nitawaangamiza wao kwa moto wa ghadhabu yangu.+ Nitaileta njia yao juu ya kichwa chao wenyewe,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”