Ezekieli 19:1-14
19 “Nawe, imba wimbo wa huzuni+ kuhusu wakuu wa Israeli,+
2 nawe useme, ‘Mama yako alikuwa nini? Simba-jike kati ya simba.+ Alilala kati ya wana-simba wenye manyoya shingoni. Aliwalea watoto wake.
3 “ ‘Na hatua kwa hatua akamlea mmoja wa watoto wake.+ Akawa mwana-simba mwenye manyoya shingoni, naye akaanza kujifunza jinsi ya kurarua mawindo.+ Alimrarua hata mtu wa udongo.
4 Na mataifa yakaendelea kusikia juu yake. Akakamatwa katika shimo lao, nao wakamchukua kwa kulabu mpaka katika nchi ya Misri.+
5 “ ‘Mama huyo alipoona kwamba amengoja nalo tumaini lake lilikuwa limepotea, ndipo akachukua mwingine kati ya watoto wake.+ Akamweka kuwa mwana-simba mwenye manyoya shingoni.
6 Na huyo akaanza kutembea huku na huku katikati ya simba. Akawa mwana-simba mwenye manyoya shingoni. Naye hatua kwa hatua akajifunza jinsi ya kurarua mawindo.+ Akamrarua hata mtu wa udongo.+
7 Naye akaijua minara ya makao yake, akayaharibu majiji yao,+ hivi kwamba nchi ikafanywa ukiwa naye akaijaza kwa sauti ya mngurumo wake.+
8 Na mataifa kuzunguka pande zote kutoka katika wilaya za utawala wakaanza kujipanga dhidi yake+ na kuutandaza wavu wao juu yake.+ Akakamatwa katika shimo lao.+
9 Mwishowe wakamweka katika tundu kwa kulabu na kumleta kwa mfalme wa Babiloni.+ Wakamleta kwa kutumia nyavu za kuwindia, ili sauti yake isisikiwe tena katika milima ya Israeli.+
10 “ ‘Mama yako+ alikuwa kama mzabibu katika damu yako,+ uliopandwa kando ya maji. Akawa mwenye kuzaa matunda na mwenye kujaa matawi kwa sababu ya maji mengi.+
11 Nayo yakawa kwake fimbo zenye nguvu, zilizokusudiwa kuwa fimbo za enzi za watawala.+ Nacho kimo chake kikarefuka hatua kwa hatua katikati ya matawi, nao ukaonekana kwa sababu ya urefu wake, kwa sababu ya wingi wa majani yake.+
12 Lakini mwishowe aling’olewa kwa ghadhabu.+ Akatupwa chini, na kulikuwa na upepo wa mashariki ulioyakausha matunda yake.+ Fimbo yake yenye nguvu ilikatwa nayo ikakauka.+ Moto wenyewe ukaiteketeza.+
13 Na sasa amepandwa nyikani,+ katika nchi isiyo na maji na yenye kiu.+
14 Na moto ukatoka katika fimbo yake.+ Ukateketeza machipukizi yake, matunda yake, na ndani yake akawa hana fimbo yoyote yenye nguvu, fimbo yoyote ya enzi ya kutawalia.+
“ ‘Huo ni wimbo wa huzuni, nao utakuwa wimbo wa huzuni.’ ”+