Ezekieli 15:1-8
15 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema:
2 “Mwana wa binadamu, mzabibu+ hutofautianaje na kila mti mwingine, hilo chipukizi, ambalo limekuja kuwa kati ya miti ya msituni?
3 Je, ufito huchukuliwa kutoka kwa huo ili kuutumia kufanyia kazi? Au watu huchukua kutoka kwa huo kijiti ili kuning’iniza aina yoyote ya chombo juu yake?
4 Tazama! Lazima utiwe motoni uwe kuni.+ Hakika moto huteketeza miisho yake yote miwili, na sehemu yake ya katikati huungua.+ Je, unafaa kwa kazi yoyote?
5 Tazama! Unapokuwa mzima, hautumiwi kwa kazi yoyote. Itakuwaje basi wakati ambapo moto umeuteketeza nao umeungua, je, kwa kweli unaweza kutumiwa tena kwa kazi zaidi!”+
6 “Kwa hiyo hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema, ‘Kama vile mzabibu kati ya miti ya msituni, ambao nimeupa moto uwe kuni, ndivyo nimewatoa wakaaji wa Yerusalemu.+
7 Nami nimeukaza uso wangu juu yao.+ Wametoka motoni, lakini moto wenyewe utawateketeza.+ Nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova, nitakapouelekeza uso wangu juu yao.’ ”+
8 “ ‘Nami nitaifanya nchi iwe mahame yenye ukiwa,+ kwa sababu wametenda kwa kukosa uaminifu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”