Esta 10:1-3

10  Naye Mfalme Ahasuero akaweka kazi ya kulazimishwa+ juu ya nchi na visiwa+ vya bahari.  Basi kuhusu kazi zake zote zenye nguvu na uwezo wake na taarifa kamili ya ukuu wa Mordekai+ ambao mfalme alimtukuza+ nao, je, mambo hayo hayakuandikwa katika Kitabu cha mambo+ ya nyakati ya wafalme wa Umedi na Uajemi?+  Kwa maana Mordekai Myahudi alikuwa wa pili+ kwa Mfalme Ahasuero naye alikuwa mkuu kati ya Wayahudi na alikubaliwa na wengi wa ndugu zake, akifanya kazi kwa ajili ya mema ya watu wake na kusema amani+ kwa uzao wao wote.

Maelezo ya Chini