Ayubu 19:1-29
19 Naye Ayubu akajibu, akasema:
2 “Ninyi mtaendelea kunikasirisha nafsi yangu mpaka wakati gani+Na kuendelea kuniponda kwa maneno?+
3 Hizi mara kumi mmenikemea;Hamna aibu kwamba mnanitendea kwa ugumu hivyo.+
4 Na, kama nimefanya kosa,+Hilo kosa litakaa pamoja nami.
5 Ikiwa kwa kweli mnajivuna sana juu yangu,+Na kuonyesha kwamba shutuma yangu inanifaa,+
6 Jueni, basi, kwamba Mungu mwenyewe amenipotosha,Naye ameuzungusha wavu wake wa kuwindia juu yangu.+
7 Tazama! Ninaendelea kupaaza sauti, ‘Jeuri!’ lakini sipati jibu lolote;+Naendelea kulia nipewe msaada, lakini hakuna haki.+
8 Amezuia pito langu kwa ukuta wa mawe,+ nami siwezi kupita;Naye anaweka giza katika barabara zangu.+
9 Amenivua utukufu wangu,+Naye anaondoa taji la kichwa changu.
10 Ananibomoa pande zote, nami naenda zangu;Naye anang’oa tumaini langu kama mti.
11 Pia hasira yake inawaka juu yangu,+Naye anaendelea kunihesabu kuwa adui yake.
12 Vikosi vyake vinakuja kwa muungano na kujenga njia yao juu yangu,+Nao wanapiga kambi kuzunguka hema langu.
13 Ndugu zangu amewaweka mbali sana nami,+Na wale wanaonijua hata wamejitenga nami.
14 Watu ninaofahamiana nao wamekoma kuwapo,+Na wale ninaowajua wamenisahau,
15 Wale wanaokaa wakiwa wageni nyumbani mwangu;+ na vijakazi wangu wananiona kuwa mgeni;Nimekuwa mgeni kwelikweli machoni pao.
16 Nimemwita mtumishi wangu, lakini hajibu.Ninaendelea kumwomba huruma kwa kinywa changu mwenyewe.
17 Pumzi yangu imemchukiza mke wangu,+Nami nimenuka kwa wana wa tumbo la mama yangu.
18 Pia wavulana wadogo wenyewe wamenikataa;+Ninaposimama tu, wanaanza kunisema.
19 Watu wote wa kikundi cha rafiki zangu wananichukia,+Na wale ambao nimewapenda wamenigeuka.+
20 Mifupa yangu inashikamana na ngozi na nyama yangu,+Nami ninaponyoka na ngozi ya meno yangu.
21 Mnionyeshe kibali kidogo, mnionyeshe kibali kidogo, enyi rafiki zangu,+Kwa kuwa mkono wenyewe wa Mungu umenigusa.+
22 Kwa nini mnaendelea kunitesa kama anavyofanya Mungu,+Na hamshibi nyama yangu?
23 Laiti sasa maneno yangu yangekuwa yameandikwa!Laiti yangekuwa yameandikwa katika kitabu!
24 Kwa kalamu ya chuma+ na kwa risasi,Laiti yangekuwa yamechongwa milele katika mwamba!
25 Nami mwenyewe najua vema kwamba mkombozi wangu+ yuko hai,Na kwamba, akija baada yangu, yeye atasimama+ juu ya mavumbi.
26 Na baada ya ngozi yangu, ambayo wameichuna,—hii!Lakini ijapokuwa kupungua kwa mwili wangu nitamwona Mungu,
27 Ambaye mimi mwenyewe nitamwona,+Na ambaye macho yangu hakika yatamwona, bali si mgeni.Figo zangu zimeisha nguvu ndani yangu kabisa.
28 Kwa maana ninyi mnasema, ‘Kwa nini tunaendelea kumtesa?’+Wakati mzizi wenyewe wa jambo hili unapatikana ndani yangu.
29 Ogopeni kwa ajili yenu kwa sababu ya upanga,+Kwa kuwa upanga unamaanisha ghadhabu juu ya makosa,Ili ninyi mjue kwamba kuna mwamuzi.”+

