2 Wafalme 21:1-26
21 Manase+ alikuwa na umri wa miaka 12 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka 55 katika Yerusalemu. Na jina la mama yake lilikuwa Hefziba.
2 Naye akafanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova,+ kulingana na machukizo ya mataifa+ ambayo Yehova alikuwa amefukuza kutoka mbele ya wana wa Israeli.
3 Kwa hiyo akajenga tena mahali pa juu ambapo Hezekia baba yake alikuwa amepaharibu,+ akasimamisha madhabahu kwa ajili ya Baali na kutengeneza mti mtakatifu, kama alivyofanya Ahabu+ mfalme wa Israeli; naye akaanza kuliinamia+ jeshi lote la mbinguni+ na kulitumikia.+
4 Naye akajenga madhabahu katika nyumba ya Yehova,+ ambayo Yehova alikuwa amesema hivi kuihusu: “Nitaweka jina langu katika Yerusalemu.”+
5 Naye akajenga madhabahu kwa ajili ya jeshi lote la mbinguni+ katika nyua mbili za nyumba ya Yehova.+
6 Naye akampitisha motoni mwana wake mwenyewe,+ naye akafanya uchawi,+ akatafuta ishara za bahati na kufanyiza wenye kuwasiliana na pepo+ na wajuzi wa kubashiri+ matukio. Alifanya kwa kiasi kikubwa yale yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova, na kumtia uchungu.
7 Na zaidi, akaweka sanamu ya kuchongwa+ ya mti mtakatifu aliyokuwa ametengeneza katika nyumba+ ambayo Yehova alikuwa amemwambia Daudi na Sulemani mwana wake hivi: “Katika nyumba hii na katika Yerusalemu, ambalo nimelichagua kutoka katika makabila yote ya Israeli, nitaliweka jina langu mpaka wakati usio na kipimo.+
8 Nami sitafanya tena mguu wa Israeli utoke katika nchi niliyowapa mababu zao,+ mradi tu wawe waangalifu kufanya kulingana na yote ambayo nimewaamuru,+ naam, kuhusiana na sheria yote ambayo mtumishi wangu Musa aliwaamuru.”
9 Nao hawakusikiliza,+ lakini Manase akaendelea kuwashawishi wafanye yaliyokuwa mabaya+ kuliko yale mataifa+ ambayo Yehova alikuwa ameyaangamiza kutoka mbele ya wana wa Israeli.
10 Na Yehova akaendelea kusema kupitia watumishi wake manabii,+ akisema:
11 “Kwa sababu Manase+ mfalme wa Yuda amefanya machukizo+ haya, ametenda kwa uovu zaidi kuliko yote waliyotenda Waamori+ waliomtangulia, naye akasababisha Yuda watende dhambi+ kwa sanamu zake za mavi.
12 Ndiyo sababu Yehova, Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Tazama, ninaleta msiba juu ya Yerusalemu+ na Yuda, ambao yeyote akiusikia masikio yake mawili yatawasha.+
13 Nami nitanyoosha juu ya Yerusalemu kamba ya kupimia+ iliyotumika juu ya Samaria+ na pia timazi iliyotumiwa juu ya nyumba ya Ahabu;+ nami nitafuta+ kabisa Yerusalemu kama vile mtu anavyofuta kabisa bakuli lisilo na mkono, akilifuta kabisa na kulipindua.+
14 Nami nitaacha mabaki+ ya urithi+ wangu na kuwatia mkononi mwa adui zao, nao watakuwa vitu vya kuporwa na kunyakuliwa na adui zao wote,+
15 kwa sababu walifanya yaliyokuwa mabaya machoni pangu nao waliendelea kunitia uchungu tangu siku ile mababu zao walipotoka Misri mpaka leo hii.’”+
16 Manase pia alimwaga kwa wingi sana damu isiyo na hatia,+ mpaka alipolijaza Yerusalemu kutoka mwisho huu mpaka mwisho ule, mbali na dhambi yake aliyosababisha Yuda kutenda dhambi kwa kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova.+
17 Na mambo mengine ya Manase na yote aliyoyafanya na dhambi yake aliyotenda, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Yuda?
18 Mwishowe Manase akalala pamoja na mababu zake,+ akazikwa katika bustani ya nyumba yake, katika bustani ya Uza;+ na Amoni mwana wake akaanza kutawala mahali pake.
19 Amoni+ alikuwa na umri wa miaka 22 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka miwili+ katika Yerusalemu. Na jina la mama yake lilikuwa Meshulemethi binti ya Haruzi kutoka Yotba.
20 Naye akaendelea kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova, kama alivyofanya Manase baba yake.+
21 Naye akaendelea kutembea katika njia yote ambayo baba yake alitembea,+ naye akaendelea kuzitumikia sanamu za mavi+ ambazo baba yake alitumikia na kuziinamia.
22 Basi akamwacha Yehova,+ Mungu wa mababu zake, naye hakutembea katika njia ya Yehova.+
23 Mwishowe watumishi wa Amoni wakampangia hila na kumuua+ mfalme ndani ya nyumba yake mwenyewe.
24 Lakini watu wa nchi wakawapiga na kuwaua wale wote waliompangia hila+ Mfalme Amoni. Kisha watu wa nchi wakamfanya Yosia+ mwana wake kuwa mfalme mahali pake.
25 Na mambo mengine ya Amoni, yale aliyofanya, je, hayakuandikwa katika kitabu+ cha mambo ya siku za wafalme wa Yuda?
26 Kwa hiyo wakamzika katika kaburi lake ndani ya bustani ya Uza;+ na Yosia+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.