2 Mambo ya Nyakati 9:1-31

9  Na malkia wa Sheba+ akasikia habari za Sulemani, naye akaja Yerusalemu ili kumjaribu Sulemani kwa maswali yenye kutatanisha,+ pamoja na msafara wenye kuvutia sana na ngamia+ wenye kuchukua mafuta ya zeri,+ na dhahabu+ nyingi sana, na mawe ya thamani.+ Mwishowe akaingia kwa Sulemani na kumwambia kila jambo lililokuwa moyoni mwake.+  Naye Sulemani akamwambia mambo yake yote,+ hakuna jambo lolote lililofichwa kwa Sulemani ambalo hakumwambia yule malkia.+  Malkia wa Sheba alipoona hekima+ ya Sulemani na ile nyumba aliyokuwa amejenga,+  na chakula cha meza+ yake na kuketi kwa watumishi wake na utumishi wa mezani wa wale wenye kumhudumia na mavazi+ yao na wanyweshaji+ wake na mavazi yao, na dhabihu zake za kuteketezwa+ alizotoa kwa ukawaida katika nyumba ya Yehova,+ basi haikubaki roho yoyote ndani yake.  Kwa hiyo akamwambia mfalme: “Ni la kweli neno lile nililosikia katika nchi yangu kuhusu mambo yako na kuhusu hekima yako.+  Nami sikuyaamini+ maneno yao mpaka nilipokuja ili nijionee kwa macho yangu mwenyewe;+ na, tazama! sikuambiwa hata nusu ya wingi wa hekima yako.+ Umezidi ile habari niliyosikia.+  Watu wako ni wenye furaha,+ na ni wenye furaha hawa watumishi wako wanaosimama mbele yako daima na kuisikiliza hekima yako.+  Na abarikiwe Yehova Mungu wako,+ ambaye amependezwa+ nawe kwa kukuweka juu ya kiti chake cha ufalme+ uwe mfalme kwa ajili ya Yehova Mungu wako;+ kwa sababu Mungu wako alipenda+ Israeli, ili kuisimamisha mpaka wakati usio na kipimo, hivi kwamba akakuweka juu yao uwe mfalme+ ili utende uamuzi wa hukumu+ na uadilifu.”+  Ndipo akampa mfalme talanta 120 za dhahabu,+ na mafuta ya zeri+ kwa wingi sana, na mawe ya thamani;+ na kulikuwa hakujapata kuwa na mafuta ya zeri kama yale ambayo malkia wa Sheba alimpa Mfalme Sulemani.+ 10  Na zaidi ya hayo, watumishi wa Hiramu+ na watumishi wa Sulemani walioleta dhahabu+ kutoka Ofiri walileta mbao za misandali+ na mawe ya thamani.+ 11  Na mfalme akatengeneza kwa zile mbao za misandali ngazi+ kwa ajili ya nyumba ya Yehova na kwa ajili ya nyumba ya mfalme+ na pia vinubi+ na vinanda+ vya waimbaji,+ na vitu kama hivyo havikuwa vimepata kuonekana kabla ya hapo katika nchi ya Yuda. 12  Na Mfalme Sulemani akampa malkia+ wa Sheba vyote vilivyompendeza, ambavyo aliomba, zaidi ya thamani ya vitu alivyomletea mfalme. Basi akageuka, akaenda katika nchi yake, yeye pamoja na watumishi wake.+ 13  Na uzito wa dhahabu iliyoletwa kwa Sulemani katika mwaka mmoja ulijumlika kuwa talanta 666 za dhahabu,+ 14  zaidi ya zile zilizoletwa na wasafiri na wanabiashara+ waliokuwa wakileta na wafalme wote wa Waarabu+ na magavana wa nchi waliokuwa wakimletea Sulemani dhahabu na fedha. 15  Na Mfalme Sulemani akatengeneza ngao kubwa mia mbili za dhahabu iliyochanganywa+ (akaweka shekeli mia sita za dhahabu iliyochanganywa kwenye kila ngao kubwa),+ 16  na ngao ndogo mia tatu za dhahabu iliyochanganywa (akaweka mina tatu za dhahabu kwenye kila ngao ndogo).+ Kisha mfalme akaziweka katika Nyumba ya Msitu wa Lebanoni.+ 17  Tena mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha ufalme cha pembe za tembo na kukifunika kwa dhahabu safi.+ 18  Na kulikuwa na vipandio sita vilivyoelekea kwenye kile kiti cha ufalme, na kulikuwa na kiti cha miguu cha dhahabu kwenye kile kiti cha ufalme, (vilikuwa vimeunganishwa), na kulikuwa na mikono ya kiti upande huu na upande ule kando ya mahali pa kuketi, na simba+ wawili walisimama kando ya ile mikono ya kiti.+ 19  Na kulikuwa na simba+ kumi na wawili waliosimama hapo juu ya vile vipandio sita, upande huu na upande ule. Hakuna ufalme mwingine wowote uliokuwa na kiti kilichotengenezwa hivyo.+ 20  Na vyombo+ vyote vya kunywea vya Mfalme Sulemani vilikuwa vya dhahabu,+ na vyombo vyote vya Nyumba ya Msitu wa Lebanoni+ vilikuwa vya dhahabu safi. Hapakuwa na kitu chochote cha fedha; haikuhesabiwa kuwa kitu+ katika siku za Sulemani. 21  Kwa maana meli za mfalme zilikuwa zikienda Tarshishi+ pamoja na watumishi wa Hiramu.+ Mara moja kila miaka mitatu meli za Tarshishi zilikuja, zikiwa zimebeba dhahabu na fedha,+ pembe za tembo,+ na sokwe na tausi.+ 22  Basi Mfalme Sulemani alikuwa mkuu katika utajiri+ na hekima+ kuliko wafalme wengine wote wa dunia. 23  Na wafalme wote wa dunia walikuwa wakiutafuta+ uso wa Sulemani ili wasikie hekima+ yake, ambayo Mungu wa kweli alikuwa ametia moyoni mwake.+ 24  Nao walikuwa wakileta kila mmoja zawadi yake,+ vyombo vya fedha na vyombo vya dhahabu+ na mavazi,+ silaha na mafuta ya zeri, farasi na nyumbu kama kawaida ya kila mwaka.+ 25  Na Sulemani akawa na vibanda elfu nne vya farasi+ na magari na farasi+ wa vita kumi na mbili elfu, naye akaviweka vitu hivyo katika majiji ya magari+ na karibu na mfalme katika Yerusalemu. 26  Naye akawa mtawala juu ya wafalme wote kuanzia ule Mto hadi kwenye nchi ya Wafilisti na hadi kwenye mpaka wa Misri.+ 27  Tena mfalme akaifanya fedha iliyomo Yerusalemu kuwa kama mawe; naye akaifanya mierezi iwe kama mikuyu+ iliyoko Shefela+ kwa wingi.+ 28  Na kulikuwa na wale waliomletea Sulemani farasi+ kutoka Misri+ na kutoka katika nchi nyingine zote. 29  Na mambo mengine ya Sulemani,+ ya kwanza na ya mwisho, je, hayakuandikwa kati ya maneno ya Nathani+ nabii na katika unabii wa Ahiya+ Mshilo,+ na katika kumbukumbu ya maono ya Ido+ mwonaji kumhusu Yeroboamu+ mwana wa Nebati?+ 30  Na Sulemani akaendelea kutawala katika Yerusalemu juu ya Israeli yote kwa miaka 40. 31  Mwishowe Sulemani akalala pamoja na mababu zake. Basi wakamzika katika Jiji la Daudi baba yake;+ na Rehoboamu+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.+

Maelezo ya Chini