2 Mambo ya Nyakati 7:1-22

7  Basi mara tu Sulemani alipomaliza kusali,+ moto ukashuka kutoka mbinguni,+ ukateketeza lile toleo la kuteketezwa+ na zile dhabihu, na utukufu+ wa Yehova ukaijaza nyumba ile.  Na makuhani hawakuweza kuingia ndani ya nyumba ya Yehova+ kwa sababu utukufu wa Yehova ulikuwa umeijaza nyumba ya Yehova.  Na wana wote wa Israeli walikuwa wakitazama wakati moto uliposhuka na utukufu wa Yehova ulipokuwa juu ya nyumba ile, kisha wakainama+ kifudifudi mara moja, juu ya sakafu ya mawe, wakasujudu+ na kumshukuru Yehova, “kwa maana yeye ni mwema,+ kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.”+  Na mfalme na watu wote walikuwa wakitoa dhabihu mbele za Yehova.+  Na Mfalme Sulemani akatoa dhabihu ya ng’ombe 22,000 na kondoo 120,000.+ Hivyo ndivyo mfalme na watu wote walivyoizindua+ nyumba ya Mungu wa kweli.  Na makuhani+ walikuwa wamesimama katika vituo vyao vya kazi, na Walawi+ wakiwa na vyombo vya nyimbo+ kwa Yehova ambavyo Daudi+ mfalme alikuwa amevitengeneza ili kumshukuru Yehova, “kwa maana fadhili zake zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo,” wakati Daudi alipokuwa akitoa sifa kwa mkono wao; na makuhani walikuwa wakipiga kwa sauti kubwa zile tarumbeta+ mbele zao, huku Israeli wote wakiwa wamesimama.  Kisha Sulemani akatakasa+ sehemu ya katikati ya ua uliokuwa mbele ya nyumba ya Yehova, kwa sababu alitolea hapo yale matoleo ya kuteketezwa+ na vile vipande vya mafuta vya dhabihu za ushirika, kwa maana madhabahu ya shaba+ ambayo Sulemani alikuwa ametengeneza haikuweza kutoshea toleo la kuteketezwa na toleo la nafaka+ na vipande vya mafuta.+  Na Sulemani akaifanya sherehe+ hiyo wakati huo kwa siku saba, na Israeli wote pamoja naye,+ kutaniko kubwa sana+ kuanzia maingilio ya Hamathi+ kushuka mpaka kwenye bonde la mto la Misri.+  Lakini katika siku ya nane wakafanya kusanyiko kuu,+ kwa sababu kule kuzinduliwa kwa madhabahu walikuwa wamekufanya kwa siku saba na ile sherehe kwa siku saba. 10  Na katika siku ya 23 ya mwezi wa 7 akawaruhusu watu waende zao nyumbani kwao, wakiwa na shangwe+ na kuchangamka moyoni kutokana na wema+ ambao Yehova alikuwa amemtendea Daudi na Sulemani na Israeli watu wake.+ 11  Hivyo Sulemani akaimaliza nyumba ya Yehova+ na nyumba ya mfalme;+ na kila jambo ambalo lilikuwa limeingia moyoni mwa Sulemani kufanya kuhusiana na nyumba ya Yehova na nyumba yake mwenyewe yeye alifanikiwa. 12  Sasa Yehova akamtokea+ Sulemani wakati wa usiku na kumwambia: “Nimeisikia sala yako,+ nami nimechagua+ mahali hapa kwa ajili yangu mwenyewe ili pawe nyumba ya dhabihu.+ 13  Ninapofunga mbingu ili mvua isinyeshe+ nami ninapoamuru panzi waile nchi+ nami nikileta tauni katikati ya watu wangu,+ 14  na watu wangu+ ambao jina langu limeitwa+ juu yao wajinyenyekeze+ na kusali+ na kuutafuta uso wangu+ na wageuke kutoka katika njia zao mbaya,+ basi mimi nitasikia nikiwa mbinguni+ na kusamehe dhambi yao,+ nami nitaiponya nchi yao.+ 15  Sasa macho+ yangu yatakuwa wazi na masikio+ yangu yatasikiliza sala katika mahali hapa. 16  Na sasa naichagua+ na kuitakasa nyumba hii ili jina langu+ liwe hapo mpaka wakati usio na kipimo,+ na macho yangu na moyo wangu vitakuwa hapo sikuzote.+ 17  “Na wewe ukitembea mbele zangu, kama Daudi+ baba yako alivyotembea, kwa kutenda kulingana na yote ambayo nimekuamuru,+ nawe uyashike masharti+ yangu na maamuzi yangu ya hukumu+ 18  mimi pia nitakifanya imara kiti cha ufalme wako,+ kama nilivyofanya agano pamoja na Daudi baba yako,+ nikisema, ‘Hakuna mwanamume wa kwako atakayekatiliwa mbali asitawale juu ya Israeli.’+ 19  Lakini mkigeuka+ nyuma na kwa kweli mziache kanuni zangu+ na amri zangu+ ambazo nimeweka mbele yenu, nanyi kwa kweli mwende kuitumikia miungu mingine+ na kuiinamia,+ 20  mimi pia nitawang’oa kutoka katika nchi yangu ambayo nimewapa;+ na nyumba hii ambayo nimeitakasa+ kwa ajili ya jina langu, nitaitupilia mbali kutoka mbele za uso wangu,+ nami nitaifanya kuwa neno la kimethali+ na shutuma kati ya vikundi vyote vya watu.+ 21  Na nyumba hii iliyokuwa marundo ya mabomoko,+ kila mtu anayepita kando yake atatazama kwa mshangao+ na kwa hakika aseme, ‘Kwa sababu gani Yehova aliitendea hivi nchi hii na nyumba hii?’+ 22  Nao watasema, ‘Ni kwa sababu walimwacha Yehova+ Mungu wa mababu zao, aliyekuwa amewatoa katika nchi ya Misri,+ nao wakashikamana na miungu mingine+ na kuiinamia na kuitumikia.+ Ndiyo sababu alileta juu yao msiba huu wote.’”+

Maelezo ya Chini