2 Mambo ya Nyakati 5:1-14
5 Mwishowe kazi yote ambayo Sulemani alipaswa kufanya kwa ajili ya nyumba ya Yehova ikamalizika,+ na Sulemani akaanza kuingiza vitu ambavyo Daudi baba yake alivifanya kuwa vitakatifu;+ naye akaweka fedha na dhahabu na vyombo vyote katika hazina za nyumba ya Mungu wa kweli.+
2 Ndipo Sulemani akaanza kuwakusanya katika Yerusalemu wanaume wazee wa Israeli+ na vichwa vyote vya makabila,+ wakuu wa nyumba za ukoo wa upande wa baba+ za wana wa Israeli, ili kulileta sanduku+ la agano la Yehova kutoka+ katika Jiji la Daudi,+ yaani, Sayuni.+
3 Basi watu wote wa Israeli wakakusanyika kwa mfalme kwenye sherehe, ile ya mwezi wa saba.+
4 Basi wanaume wote wazee wa Israeli wakaja,+ na Walawi wakaanza kulichukua Sanduku.+
5 Nao wakalipandisha Sanduku+ na hema la mkutano+ na vyombo vyote vitakatifu+ vilivyokuwa katika hema. Makuhani Walawi wakavipandisha.+
6 Na Mfalme Sulemani na kusanyiko lote la Waisraeli, waliokutana naye kwa wakati uliowekwa mbele ya lile Sanduku walikuwa wakitoa dhabihu+ za kondoo na ng’ombe ambao hawangeweza kuhesabiwa kwa sababu ya wingi.
7 Ndipo makuhani wakaliingiza sanduku la agano la Yehova mahali pake, ndani ya chumba cha ndani kabisa+ cha nyumba, ndani ya Patakatifu Zaidi,+ chini ya mabawa ya wale makerubi.+
8 Basi makerubi waliendelea kunyoosha mabawa yao juu ya mahali pa lile Sanduku, hivi kwamba makerubi walilifunika Sanduku na miti yake+ kutoka juu.+
9 Lakini ile miti ilikuwa mirefu, hivi kwamba ncha za miti hiyo zilionekana katika Patakatifu mbele ya chumba cha ndani kabisa, lakini hazikuonekana nje, nayo iko hapo mpaka leo hii.+
10 Hamkuwa na chochote ndani ya lile Sanduku ila yale mabamba+ mawili ambayo Musa aliwapa katika Horebu,+ wakati Yehova alipofanya agano+ na wana wa Israeli walipokuwa wakitoka Misri.+
11 Na ikawa kwamba makuhani walipoondoka mahali patakatifu (kwa maana makuhani wote waliopatikana walikuwa wamejitakasa+—hapakuwa na uhitaji wa kufuata ile migawanyo);+
12 na Walawi+ waliokuwa waimbaji wa wote hawa, yaani, wa Asafu,+ wa Hemani,+ wa Yeduthuni+ na wa wana wao na wa ndugu zao, waliovaa mavazi ya kitambaa laini pamoja na matoazi+ na vinanda+ na vinubi,+ walikuwa wamesimama upande wa mashariki wa ile madhabahu na pamoja nao makuhani wenye kufikia hesabu ya 120 wakipiga tarumbeta;+
13 na ikawa kwamba mara tu wapiga-tarumbeta na waimbaji walipokuwa kama mtu mmoja+ kwa kutokeza sauti moja isikike katika kumsifu na kumshukuru Yehova, na mara tu walipopaaza sauti kwa tarumbeta na kwa matoazi na kwa vyombo vya nyimbo+ na kwa kumsifu+ Yehova, “kwa maana yeye ni mwema,+ kwa maana fadhili zake zenye upendo+ ni za mpaka wakati usio na kipimo,” nyumba ile ikajaa wingu,+ nyumba ya Yehova,+
14 na makuhani hawakuweza kusimama ili kuhudumu kwa sababu ya lile wingu;+ kwa maana utukufu+ wa Yehova uliijaza nyumba ya Mungu wa kweli.