2 Mambo ya Nyakati 5:1-14

5  Mwishowe kazi yote ambayo Sulemani alipaswa kufanya kwa ajili ya nyumba ya Yehova ikamalizika,+ na Sulemani akaanza kuingiza vitu ambavyo Daudi baba yake alivifanya kuwa vitakatifu;+ naye akaweka fedha na dhahabu na vyombo vyote katika hazina za nyumba ya Mungu wa kweli.+  Ndipo Sulemani akaanza kuwakusanya katika Yerusalemu wanaume wazee wa Israeli+ na vichwa vyote vya makabila,+ wakuu wa nyumba za ukoo wa upande wa baba+ za wana wa Israeli, ili kulileta sanduku+ la agano la Yehova kutoka+ katika Jiji la Daudi,+ yaani, Sayuni.+  Basi watu wote wa Israeli wakakusanyika kwa mfalme kwenye sherehe, ile ya mwezi wa saba.+  Basi wanaume wote wazee wa Israeli wakaja,+ na Walawi wakaanza kulichukua Sanduku.+  Nao wakalipandisha Sanduku+ na hema la mkutano+ na vyombo vyote vitakatifu+ vilivyokuwa katika hema. Makuhani Walawi wakavipandisha.+  Na Mfalme Sulemani na kusanyiko lote la Waisraeli, waliokutana naye kwa wakati uliowekwa mbele ya lile Sanduku walikuwa wakitoa dhabihu+ za kondoo na ng’ombe ambao hawangeweza kuhesabiwa kwa sababu ya wingi.  Ndipo makuhani wakaliingiza sanduku la agano la Yehova mahali pake, ndani ya chumba cha ndani kabisa+ cha nyumba, ndani ya Patakatifu Zaidi,+ chini ya mabawa ya wale makerubi.+  Basi makerubi waliendelea kunyoosha mabawa yao juu ya mahali pa lile Sanduku, hivi kwamba makerubi walilifunika Sanduku na miti yake+ kutoka juu.+  Lakini ile miti ilikuwa mirefu, hivi kwamba ncha za miti hiyo zilionekana katika Patakatifu mbele ya chumba cha ndani kabisa, lakini hazikuonekana nje, nayo iko hapo mpaka leo hii.+ 10  Hamkuwa na chochote ndani ya lile Sanduku ila yale mabamba+ mawili ambayo Musa aliwapa katika Horebu,+ wakati Yehova alipofanya agano+ na wana wa Israeli walipokuwa wakitoka Misri.+ 11  Na ikawa kwamba makuhani walipoondoka mahali patakatifu (kwa maana makuhani wote waliopatikana walikuwa wamejitakasa+—hapakuwa na uhitaji wa kufuata ile migawanyo);+ 12  na Walawi+ waliokuwa waimbaji wa wote hawa, yaani, wa Asafu,+ wa Hemani,+ wa Yeduthuni+ na wa wana wao na wa ndugu zao, waliovaa mavazi ya kitambaa laini pamoja na matoazi+ na vinanda+ na vinubi,+ walikuwa wamesimama upande wa mashariki wa ile madhabahu na pamoja nao makuhani wenye kufikia hesabu ya 120 wakipiga tarumbeta;+ 13  na ikawa kwamba mara tu wapiga-tarumbeta na waimbaji walipokuwa kama mtu mmoja+ kwa kutokeza sauti moja isikike katika kumsifu na kumshukuru Yehova, na mara tu walipopaaza sauti kwa tarumbeta na kwa matoazi na kwa vyombo vya nyimbo+ na kwa kumsifu+ Yehova, “kwa maana yeye ni mwema,+ kwa maana fadhili zake zenye upendo+ ni za mpaka wakati usio na kipimo,” nyumba ile ikajaa wingu,+ nyumba ya Yehova,+ 14  na makuhani hawakuweza kusimama ili kuhudumu kwa sababu ya lile wingu;+ kwa maana utukufu+ wa Yehova uliijaza nyumba ya Mungu wa kweli.

Maelezo ya Chini