2 Mambo ya Nyakati 4:1-22

4  Kisha akatengeneza ile madhabahu ya shaba,+ urefu wake ukiwa ni mikono 20, na upana wake mikono 20, na kimo chake mikono 10.+  Naye akatengeneza bahari ya kuyeyushwa+ urefu wa mikono 10 kutoka ukingo wake mmoja mpaka ukingo wake mwingine, ikiwa ni mviringo kuzunguka pande zote, na kimo chake kilikuwa mikono 5, na kamba ya mikono 30 ingeweza kuizunguka pande zote.+  Na kulikuwa na mapambo yenye umbo la kibuyu+ chini yake kwenye mviringo wote, yakiizunguka, 10 katika kila urefu wa mkono mmoja, yakiizunguka ile bahari pande zote.+ Yale mapambo yenye umbo la kibuyu yalikuwa katika mistari miwili, yakiwa yamefanyizwa katika myeyusho wake.  Ilikuwa imesimama juu ya ng’ombe-dume kumi na wawili,+ watatu wakitazama kaskazini na watatu wakitazama magharibi na watatu wakitazama kusini na watatu wakitazama mashariki; na bahari ilikuwa juu yao, na sehemu zao za nyuma zote zilielekea upande wa ndani.+  Na unene wake ulikuwa upana wa kiganja kimoja; na ukingo wake ulikuwa kama muundo wa ukingo wa kikombe, ua la yungiyungi.+ Nayo ikiwa kitu cha kuhifadhia, ingeweza kuchukua vipimo elfu tatu vya bathi.+  Tena akatengeneza beseni kumi, akaweka tano upande wa kuume na tano upande wa kushoto,+ ili kuoshea humo.+ Wakawa wakioshea humo vitu vinavyohusiana na toleo la kuteketezwa.+ Lakini ile bahari ilikuwa kwa ajili ya makuhani kuogea humo.+  Kisha akatengeneza vinara vya taa+ vya dhahabu, kumi vya muundo mmoja,+ akaviweka katika hekalu, vitano upande wa kuume na vitano upande wa kushoto.+  Tena akatengeneza meza kumi, akaziweka katika hekalu, tano upande wa kuume na tano upande wa kushoto,+ halafu akatengeneza mabakuli mia moja ya dhahabu.  Kisha akatengeneza ua+ wa makuhani+ na ule ua mkuu na milango ya ule ua,+ akaifunika milango yake kwa shaba. 10  Naye akaweka ile bahari upande wa kuume, upande wa mashariki, kuelekea kusini.+ 11  Mwishowe Hiramu akatengeneza makopo+ na sepetu+ na mabakuli.+ Basi Hiramu akamaliza kuifanya kazi aliyomfanyia Mfalme Sulemani kwenye nyumba ya Mungu wa kweli. 12  Zile nguzo+ mbili na yale makombe ya mviringo+ juu ya zile nguzo mbili na zile kamba mbili za nyavu+ za kufunika yale makombe mawili ya mviringo yaliyokuwa juu ya zile nguzo 13  na yale makomamanga+ mia nne kwa ajili ya zile kamba mbili za nyavu, mistari miwili ya makomamanga kwa kila kamba ya nyavu ili kufunika yale makombe mawili ya mviringo yaliyokuwa juu ya zile nguzo,+ 14  na yale mabehewa+ kumi na zile beseni+ kumi juu ya yale mabehewa; 15  ile bahari+ moja na wale ng’ombe-dume kumi na wawili walio chini yake,+ 16  na makopo na sepetu+ na nyuma+ na vyombo+ vyake vyote ambavyo Hiram-abivu+ alimtengenezea Mfalme Sulemani kwa ajili ya nyumba ya Yehova, vya shaba iliyong’arishwa. 17  Mfalme aliviyeyushia katika Wilaya ya Yordani katika ule udongo mzito kati ya Sukothi+ na Sereda.+ 18  Basi Sulemani akatengeneza vyombo hivyo vyote kwa wingi sana, kwa maana uzito wa ile shaba haukujulikana.+ 19  Na Sulemani akatengeneza vyombo+ vyote vilivyokuwa katika nyumba ya Mungu wa kweli na ile madhabahu ya dhahabu+ na zile meza+ zenye ule mkate wa wonyesho juu yake, 20  na vinara vya taa+ na taa+ zake za dhahabu safi, ili kuziwasha mbele ya chumba cha ndani kabisa+ kulingana na kanuni; 21  na maua na taa na mikasi ya tambi,+ ya dhahabu, (ilikuwa ndiyo dhahabu safi zaidi,) 22  na mikasi ya taa na mabakuli na vikombe na vyetezo, vya dhahabu safi,+ na mwingilio wa nyumba,+ milango yake ya ndani ya Patakatifu Zaidi na milango+ ya nyumba ya hekalu, ya dhahabu.

Maelezo ya Chini