2 Mambo ya Nyakati 36:1-23
36 Kisha watu wa nchi wakamchukua Yehoahazi+ mwana wa Yosia na kumfanya kuwa mfalme mahali pa baba yake katika Yerusalemu.+
2 Yehoahazi alikuwa na umri wa miaka 23 alipoanza kutawala, naye akatawala miezi mitatu katika Yerusalemu.+
3 Hata hivyo, mfalme wa Misri akamwondoa Yerusalemu+ na kuitoza nchi talanta mia moja za fedha+ na talanta moja ya dhahabu.
4 Zaidi ya hayo, mfalme+ wa Misri akamfanya Eliakimu+ ndugu yake kuwa mfalme juu ya Yuda na Yerusalemu na kulibadili jina lake kuwa Yehoyakimu; lakini Neko+ akamchukua Yehoahazi ndugu yake na kumpeleka Misri.+
5 Yehoyakimu+ alikuwa na umri wa miaka 25 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka 11 katika Yerusalemu;+ naye akaendelea kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova Mungu wake.+
6 Nebukadneza+ mfalme wa Babiloni akapanda+ kuja kumshambulia ili amfunge kwa pingu mbili za shaba apate kumchukua mpaka Babiloni.+
7 Na sehemu ya vyombo+ vya nyumba ya Yehova, Nebukadneza+ akavipeleka Babiloni kisha akaviweka katika jumba lake la kifalme kule Babiloni.+
8 Na yale mambo mengine+ ya Yehoyakimu na machukizo+ yake aliyoyatenda na mambo yaliyopatikana juu yake, tazama, yameandikwa katika Kitabu+ cha Wafalme wa Israeli na Yuda; na Yehoyakini+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.
9 Yehoyakini+ alikuwa na umri wa miaka kumi na minane alipoanza kutawala, naye akatawala miezi mitatu+ na siku kumi katika Yerusalemu; naye akaendelea kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova.+
10 Na mwanzoni+ mwa mwaka Mfalme Nebukadneza akatuma watu,+ akamleta Babiloni+ pamoja na vyombo vyenye kutamanika vya nyumba ya Yehova.+ Tena akamfanya Sedekia+ ndugu ya baba yake kuwa mfalme juu ya Yuda na Yerusalemu.+
11 Sedekia+ alikuwa na umri wa miaka 21 alipoanza kutawala, naye akatawala miaka 11 katika Yerusalemu.+
12 Naye akaendelea kufanya yaliyokuwa mabaya+ machoni pa Yehova Mungu wake. Hakujinyenyekeza+ kwa ajili ya nabii+ Yeremia+ kwa agizo la Yehova.
13 Naye akamwasi hata Mfalme Nebukadneza,+ aliyekuwa amemwapisha kwa Mungu;+ naye akaendelea kuifanya shingo yake kuwa ngumu+ na kuufanya moyo wake kuwa mgumu+ ili asirudi kwa Yehova Mungu wa Israeli.
14 Hata wakuu wote wa makuhani+ na watu wenyewe wakatenda kwa ukosefu wa uaminifu kwa kiasi kikubwa, kulingana na machukizo+ yote ya mataifa, hivi kwamba wakaitia unajisi nyumba ya Yehova aliyokuwa ameitakasa katika Yerusalemu.+
15 Na Yehova Mungu wa mababu zao akaendelea kutuma juu yao kupitia kwa wajumbe wake,+ akatuma tena na tena, kwa sababu aliwahurumia watu wake+ na makao yake.+
16 Lakini waliendelea kuwadhihaki+ wale wajumbe wa Mungu wa kweli na kuyadharau maneno+ yake na kuwafanyia mzaha+ manabii wake, mpaka ghadhabu+ ya Yehova ikapanda juu ya watu wake, mpaka kukawa hakuna kuponywa.+
17 Kwa hiyo akaleta juu yao mfalme wa Wakaldayo,+ ambaye aliwaua vijana wao kwa upanga+ katika nyumba ya patakatifu pao,+ wala hakumhurumia kijana wala bikira, mzee wala mkongwe.+ Kila kitu Yeye alikitia mkononi mwake.
18 Na vyombo+ vyote, vikubwa+ kwa vidogo, vya nyumba ya Mungu wa kweli na hazina za nyumba ya Yehova na hazina+ za mfalme+ na za wakuu wake, kila kitu akakipeleka Babiloni.
19 Naye akaiteketeza nyumba ya Mungu wa kweli+ na kuubomoa ukuta+ wa Yerusalemu; na minara yake yote ya makao wakaiteketeza kwa moto na pia vyombo vyake vyote vyenye kutamanika,+ ili kufanya uharibifu.+
20 Tena akawachukua mateka mpaka Babiloni wale waliobaki kutokana na upanga,+ nao wakawa watumishi wake+ na wa wanawe mpaka mamlaka ya kifalme ya Uajemi+ ilipoanza kutawala;
21 ili kulitimiza neno la Yehova kupitia kinywa cha Yeremia,+ mpaka nchi ilipokuwa imelipa sabato zake.+ Siku zote za kukaa ukiwa ilishika sabato, ili kutimiza miaka 70.+
22 Na katika mwaka wa kwanza wa Koreshi+ mfalme wa Uajemi,+ ili neno la Yehova+ kupitia kinywa cha Yeremia+ litimizwe, Yehova aliiamsha roho+ ya Koreshi mfalme wa Uajemi, hivi kwamba akatangaza mwito katika ufalme wake wote, na pia kwa maandishi,+ akisema:
23 “Koreshi mfalme wa Uajemi+ amesema hivi, ‘Yehova Mungu wa mbinguni amenipa falme zote za dunia,+ naye mwenyewe amenipa utume nimjengee nyumba katika Yerusalemu, huko Yuda.+ Yeyote aliye katikati yenu ninyi watu wake wote,+ Yehova Mungu wake na awe pamoja naye.+ Basi apande na kwenda.’”+